Scripture Stories
Sura ya 20: Alma na Nehori


Sura ya 20

Alma na Nehori

Picha
Alma mdogo na wengine

Kabla Mfalme Mosia hajafa, Wanefi walichagua waamuzi kuwaongoza. Alma mdogo alikuwa mwamuzi mkuu wa kwanza. Pia alikuwa ni kiongozi wa Kanisa.

Picha
Nehori akifundisha uongo

Mtu mmoja mkubwa, mwenye nguvu aliyeitwa Nehori alianza kufundisha uongo. Alisema kila mtu angeokolewa bila kujali walikuwa wema au waovu. Watu wengi walimwamini Nehori.

Picha
Gideoni na Nehori

Nehori alifundisha kinyume na Kanisa la Mungu, lakini mtu mwenye haki aliyeitwa Gideoni alitetea Kanisa. Nehori alibishana na Gideoni, lakini Gideoni aliongea kwa maneno ya Mungu.

Picha
Nehori akimuua Gideoni

Nehori alikasirika na akatoa upanga wake na kumuua Gideoni.

Picha
Nehori akipelekwa kwa Alma

Nehori alipelekwa kwa Alma kuhukumiwa. Nehori kwa ujasiri alijitetea.

Picha
Alma na Nehori

Lakini Alma alisema Nehori alikuwa na hatia kwa sababu alikuwa amewafundisha watu kuwa waovu na alimuua Gideoni.

Picha
Alma

Alma alisema Nehori alitakiwa kuadhibiwa kwa kumuua Gideoni. Kulingana na sheria, Nehori lazima afe.

Picha
Nehori akiuwawa

Nehori alipelekwa kwenye mlima ulioko karibu na akauliwa. Kabla hajafa alisema kila kitu alichokifundisha kilikuwa cha uongo. Lakini watu wengi bado waliyaamini mafundisho ya uongo ya Nehori.

Picha
watu wakidhihakiwa

Watu hawa walipenda utajiri na wasingetii amri za Mungu. Waliwadhihaki waumini wa Kanisa na kubishana na kupigana nao.

Picha
Wanandoa wakidhihakiwa

Watu wema waliendelea kutii amri na hawakunung’unika hata wakati wafuasi wa Nehori walipowaumiza.

Picha
Watu wakishirikiana

Waumini wa Kanisa walishiriki kila kitu walichokuwa nacho na masikini, na waliwajali wagonjwa. Walitii amri, na Mungu aliwabariki.

Chapisha