Scripture Stories
Sura ya 23: Amoni: Mtumishi Mkuu


Sura ya 23

Amoni: Mtumishi Mkuu

Picha
wana wa Mosia wakiondoka

Wana wanne wa Mosia waliondoka Zarahemla kwenda kufundisha Walamani injili. Kila mmoja alikwenda katika mji tofauti.

Picha
Amoni akikamatwa

Amoni alikwenda katika nchi ya Ishmaeli. Alipokuwa akiingia kwenye mji, Walamani walimfunga kamba na wakamchukua mpaka kwa mfalme, Lamoni.

Picha
Lamoni na Amoni

Amoni alimwambia Mfalme Lamoni kwamba alitaka kuishi kati ya Walamani. Lamoni alifurahi na akawaambia watu wake wamfungue Amoni.

Picha
Amoni akichunga mifugo

Amoni alisema angekuwa mmoja wa watumishi wa mfalme. Mfalme alimtuma aende kuchunga mifugo.

Picha
Walamani wakitawanya mifugo

Siku moja wakati Amoni na baadhi ya watumishi wengine walikuwa wakipeleka mifugo kunywa maji, Walamani wezi waliitawanya mifugo na kujaribu kuiiba.

Picha
Watumishi wakiwa na Amoni

Watumishi waliokuwa na Amoni waliogopa. Mfalme Lamoni alikuwa amewauwa watumishi wake wengine waliopoteza mifugo.

Picha
Amoni

Amoni alijua hii ilikuwa ni fursa ya kutumia nguvu za Bwana kuvutia mioyo ya Walamani. Kisha wangesikiliza mafundisho yake.

Picha
Amoni akiongea na watumishi

Amoni aliwaambia watumishi kwamba kama wangeikusanya mifugo iliyotawanywa, mfalme asingewaua.

Picha
Amoni akiikusanya mifugo

Amoni na watumishi wengine haraka waliipata mifugo na kuirudisha katika sehemu ya kunyweshea.

Picha
Amoni akizungumza na watumishi

Walamani wezi walirudi tena. Amoni aliwaambia watumishi wengine kuichunga mifugo wakati akipigana na wezi.

Picha
wezi

Walamani wezi hawakumwogopa Amoni. Walifikiri wangemuua kiurahisi.

Picha
Amoni akiwauwa wezi

Nguvu za Mungu Zilikuwa pamoja na Amoni. Aliwapiga na kuwauwa baadhi ya wezi kwa mawe, kitu ambacho kiliwafanya wezi waliosalia kupata hasira sana.

Picha
Amoni akipigana na wezi

Walijaribu kumuua Amoni kwa rungu zao, lakini kila mara mwizi aliponyanyua rungu kumpiga, Amoni alikata mkono wa mwizi. Kwa kuogopa, wezi walikimbia.

Picha
Watumishi wakizungumza na mfalme

Watumishi walipeleka mikono iliyokatwa kwa Mfalme Lamoni na kumwambia ambacho Amoni alikuwa amekifanya.

Picha
Mfalme Lamoni

Mfalme alishangazwa na nguvu kuu ya Amoni. Alitaka kumuona Amoni lakini aliogopa kwa sababu alidhani Amoni alikuwa ni Roho Mkuu.

Picha
mfalme akitafakari

Wakati Amoni alipokwenda ndani kumuona, Mfalme Lamoni hakujua nini cha kusema. Hakuongea kwa muda wa saa moja.

Picha
Amoni akihubiri

Roho Mtakatifu alimsaidia Amoni kujua nini mfalme alikuwa akiwaza. Amoni alifafanua kwamba yeye hakuwa Roho Mkuu. Alikuwa ni mtu.

Picha
Mfalme Lamoni akiongea na Amoni

Mfalme alimuahidi Amoni chochote alichotaka kama angemwabia ni nguvu gani alitumia kuwashinda wezi na kujua mawazo ya mfalme.

Picha
Amoni akiongea na mfalme Lamoni

Amoni alisema kitu pekee alichokitaka ni Mfalme Lamoni kuamini kile ambacho angekisema. Mfalme alisema angeamini chochote ambacho Amoni angemwambia.

Picha
Amoni akizungumza na Mfalme Lamoni

Amoni alimuuliza Mfalme Lamoni kama aliamini katika Mungu. Mfalme alisema kwamba aliamini katika Roho Mkuu.

Picha
Amoni akimfundisha Lamoni

Amoni alisema kwamba Roho Mkuu ni Mungu, ambaye aliumba kila kitu mbinguni na duniani, na kwamba anajua mawazo ya watu.

Picha
Amoni akimfundisha Lamoni

Amoni alisema watu waliumbwa kwa mfano wa Mungu. Pia alisema Mungu alimwita kufundisha injili kwa Lamoni na watu wake.

Picha
Amoni akifundisha kwa kutumia maandiko

Akitumia maandiko, Amoni alimfundisha Mfalme Lamoni kuhusu Uumabji, Adamu, na Yesu Kristo.

Picha
Lamoni akisali

Mfalme Lamoni alimwamini Amoni na alisali ili kusamehewa dhambi zake. Kisha alianguka ardhini na kuonekana kama mfu.

Picha
Watumishi wa mfalme

Watumishi walimbeba mfalme mpaka kwa mke wake na kumlaza kitandani. Baada ya siku mbili watumishi walidhani alikuwa amekufa na walitaka kumzika.

Picha
malkia akiongea na Amoni

Malkia hakuamini kwamba mume wake alikuwa amekufa. Akiwa amesikia kuhusu nguvu kuu ya Amoni, alimuomba amsaidie mfalme.

Picha
Amoni akiongea na malkia

Amoni alijua Lamoni alikuwa chini ya nguvu za Mungu. Alimwambia malkia kwamba Lamoni angeamka siku iliyofuata.

Picha
Lamoni akiamka

Malkia alikaa pembeni mwa Lamoni usiku mzima. Siku iliyofuata Lamoni aliamka na alisema alimuona Yesu Kristo. Mfalme na malkia walijazwa na Roho Mtakatifu.

Picha
Lamoni akibatizwa

Lamoni aliwafundisha watu wake kuhusu Mungu na Yesu Kristo. Wale walioamini walitubu dhambi zao na walibatizwa.

Chapisha