Scripture Stories
Sura ya 31: Kapteni Moroni anamshinda Zerahemna


Sura ya 31

Kapteni Moroni anamshinda Zerahemna

Picha
Walamani wakizungumza

Zerahemna, kiongozi wa Walamani, alitaka watu wake waendelee kuwachukia Wanefi na kuwafanya watumwa wao.

Picha
Askari wa Wanefi

Wanefi walitaka kuiweka huru nchi yao na familia zao. Pia walitaka kuwa huru kumwabudu Mungu.

Picha
Kapteni Moroni

Kapteni Moroni alikuwa kiongozi wa jeshi la Wanefi. Wakati Walamani walipokuja kupigana, Moroni na jeshi lake walikutana nao katika nchi ya Jershoni.

Picha
Kapteni Moroni akiwa na Jeshi

Kapteni Moroni aliandaa jeshi lake kwa silaha, ngao, mavazi ya kivita na nguo nzito.

Picha
Jeshi la Walamani

Walamani walikuwa na jeshi kubwa lakini waliogopa wakati walipoona mavazi ya kivita ya Wanefi—Walamani walikuwa wamevaa nguo chache sana.

Picha
Walamani wakijificha nyikani

Jeshi la Walamani halikuthubutu kupigana na jeshi la Kapteni Moroni. Walamani walikimbilia nyikani na kuamua kushambulia mji mwingine wa Wanefi.

Picha
Alma akisali

Moroni alituma wapelelezi kuwapeleleza Walamani. Pia alimuomba Alma asali kwa Bwana kwa ajili ya msaada. Bwana alimwambia Alma wapi Walamani wangeshambulia.

Picha
Moroni akisonga na Jeshi lake

Wakati Moroni alipopokea ujumbe wa Alma, aliacha baadhi ya wanajeshi kulinda Jershoni na akasonga na waliobaki kukutana na Walamani.

Picha
Wanajeshi wa Moroni wakijificha

Wanajeshi wa Kapteni Moroni walijificha kwenye pande zote mbili za mto Sidoni, wakisubiri kulitia mtegoni jeshi la Walamani.

Picha
Vita katika mto

Vita vilianza, Walamani walijaribu kutoroka kwa kuvuka mto, lakini wanefi wengi zaidi walikuwa wakisubiri upande mwingine wa mto.

Picha
Wanefi wakirusha mishale

Wakipigana kwa nguvu kuliko hapo awali, Zerahemna na jeshi lake waliwauwa wanefi wengi. Wanefi walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada.

Picha
Wanefi wakikabiliana na Walamani

Bwana aliliimarisha jeshi la Wanefi. Jeshi liliwazunguka Walamani, na Moroni aliamuru vita kusimama.

Picha
Moroni akiongea na Zerahemna

Moroni alimwambia Zerahemna kwamba Wanefi hawakutaka kuwauwa Walamani au kuwafanya watumwa wao.

Picha
Moroni akizugumza

Moroni alisema walamani wasingeweza kuiua imani ya Wanefi katika Yesu Kristo. Alisema Mungu angeendelea kuwasaidia Wanefi kupigana kama wangekuwa waaminifu.

Picha
Moroni akimwamuru Zerahemna

Moroni alimwamuru Zerahemna kusalimisha silaha zake. Walamani wasingeuwawa kama wangeahidi kutopigana na Wanefi tena.

Picha
Zerahemna akimpa Moroni silaha

Zerahemna alimpa Moroni silaha zake lakini hakuahidi kutopigana. Moroni alimrudishia silaha zake ili walamani wajilinde.

Picha
Askari wa Wanefi akiuvunja upanga wa Zerahemna

Zerahemna kwa haraka alikwenda kwa Moroni ili kumuua, lakini askari wa Wanefi alimpiga na kuuvunja upanga wa Zerahemna.

Picha
Askari akitoa ngozi ya kichwa cha Zerahemna

Kisha askari alitoa ngozi ya kichwa cha Zerahemna na, akakiweka kwenye ncha ya upanga, na kuinyanyua juu.

Picha
Ngozi ya kichwa cha Walamani

Walamani wangeanguka ardhini kama ngozi ya kichwa ilivyoanguka, aliwaambia, isipokuwa wasalimishe silaha zao na kuahidi kamwe kutopigana tena.

Picha
Walamani wakisalimisha silaha zao

Wengi wa Walamani waliweka silaha zao miguuni pa Moroni na kuahidi kutopigana tena. Waliruhusiwa kwenda huru.

Picha
Walamani wakipigana

Kwa hasira, Zerahemna aliwahamasisha askari waliobaki kupigana. Askari wa Moroni waliwauwa wengi wao.

Picha
Zerahemna akimsihi Moroni

Wakati Zerahemna alipoona yeye na watu wake wangeuwawa, alimuomba Moroni kutowauwa. Aliahidi kutopigana tena na Wanefi.

Picha
Walamani wakiwaacha Wanefi

Moroni alisimamamisha vita na kuchukua silaha za Walamani. Baada ya kuwa wameahidi kutopigana, walamani waliondoka.

Chapisha