Sura ya 31
Kapteni Moroni anamshinda Zerahemna
Zerahemna, kiongozi wa Walamani, alitaka watu wake waendelee kuwachukia Wanefi na kuwafanya watumwa wao.
Wanefi walitaka kuiweka huru nchi yao na familia zao. Pia walitaka kuwa huru kumwabudu Mungu.
Kapteni Moroni alikuwa kiongozi wa jeshi la Wanefi. Wakati Walamani walipokuja kupigana, Moroni na jeshi lake walikutana nao katika nchi ya Jershoni.
Kapteni Moroni aliandaa jeshi lake kwa silaha, ngao, mavazi ya kivita na nguo nzito.
Walamani walikuwa na jeshi kubwa lakini waliogopa wakati walipoona mavazi ya kivita ya Wanefi—Walamani walikuwa wamevaa nguo chache sana.
Jeshi la Walamani halikuthubutu kupigana na jeshi la Kapteni Moroni. Walamani walikimbilia nyikani na kuamua kushambulia mji mwingine wa Wanefi.
Moroni alituma wapelelezi kuwapeleleza Walamani. Pia alimuomba Alma asali kwa Bwana kwa ajili ya msaada. Bwana alimwambia Alma wapi Walamani wangeshambulia.
Wakati Moroni alipopokea ujumbe wa Alma, aliacha baadhi ya wanajeshi kulinda Jershoni na akasonga na waliobaki kukutana na Walamani.
Wanajeshi wa Kapteni Moroni walijificha kwenye pande zote mbili za mto Sidoni, wakisubiri kulitia mtegoni jeshi la Walamani.
Vita vilianza, Walamani walijaribu kutoroka kwa kuvuka mto, lakini wanefi wengi zaidi walikuwa wakisubiri upande mwingine wa mto.
Wakipigana kwa nguvu kuliko hapo awali, Zerahemna na jeshi lake waliwauwa wanefi wengi. Wanefi walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada.
Bwana aliliimarisha jeshi la Wanefi. Jeshi liliwazunguka Walamani, na Moroni aliamuru vita kusimama.
Moroni alimwambia Zerahemna kwamba Wanefi hawakutaka kuwauwa Walamani au kuwafanya watumwa wao.
Moroni alisema walamani wasingeweza kuiua imani ya Wanefi katika Yesu Kristo. Alisema Mungu angeendelea kuwasaidia Wanefi kupigana kama wangekuwa waaminifu.
Moroni alimwamuru Zerahemna kusalimisha silaha zake. Walamani wasingeuwawa kama wangeahidi kutopigana na Wanefi tena.
Zerahemna alimpa Moroni silaha zake lakini hakuahidi kutopigana. Moroni alimrudishia silaha zake ili walamani wajilinde.
Zerahemna kwa haraka alikwenda kwa Moroni ili kumuua, lakini askari wa Wanefi alimpiga na kuuvunja upanga wa Zerahemna.
Kisha askari alitoa ngozi ya kichwa cha Zerahemna na, akakiweka kwenye ncha ya upanga, na kuinyanyua juu.
Walamani wangeanguka ardhini kama ngozi ya kichwa ilivyoanguka, aliwaambia, isipokuwa wasalimishe silaha zao na kuahidi kamwe kutopigana tena.
Wengi wa Walamani waliweka silaha zao miguuni pa Moroni na kuahidi kutopigana tena. Waliruhusiwa kwenda huru.
Kwa hasira, Zerahemna aliwahamasisha askari waliobaki kupigana. Askari wa Moroni waliwauwa wengi wao.
Wakati Zerahemna alipoona yeye na watu wake wangeuwawa, alimuomba Moroni kutowauwa. Aliahidi kutopigana tena na Wanefi.
Moroni alisimamamisha vita na kuchukua silaha za Walamani. Baada ya kuwa wameahidi kutopigana, walamani waliondoka.