Sura ya 45
Yesu Kristo Anatufundisha kuhusu Sakramenti na Sala
Yesu Kristo aliwatuma wafuasi wake waende wakalete mkate na divai. Aliwaambia Wanefi waketi chini.
Baada ya wanafunzi kurejea, Mwokozi aliumega mkate katika vipande vipande na kuubariki. Aliwapa wanafunzi wake na kuwataka wawapatie watu wengine pia.
Yesu alisema kwamba watu wanaoshiriki sakramenti wanaahidi daima kumkumbuka Yeye na dhabihu Yake. Kisha wanapokea Roho Wake.
Yesu Kristo alibariki divai na kutoa kiasi kwa wanafunzi Wake. Wanafunzi waliwapa watu divai kiasi.
Yesu alisema wale wanaoshiriki sakramenti wanaahidi kutii amri Zake.
Yesu tena aliwaambia wanafunzi Wake kwamba kila mtu anayeshiriki sakramenti na kumkumbuka daima atakuwa na Roho Wake.
Aliwaambia mitume wake wangebarikiwa kama wangetii amri Zake.
Aliwaambia wasali kila wakati na wasali jinsi walivyokuwa wamemuona akisali.
Mwokozi aliwaambia Wanefi wote wasali kwa Baba wa Mbinguni kwa jina Lake. Pia aliwaamuru wasali pamoja na familia zao.
Alisema watu lazima wakutane pamoja mara kwa mara. Wanapaswa kuwakaribisha wengine katika mikutano yao, kusali kwa niaba yao, na kuwa mifano mizuri kwao.
Yesu aliwapatia wanafunzi Wake uwezo kutoa Roho Mtakatifu. Kisha mawingu yakawafunika watu kwa hivyo ni wanafunzi tu waliomuona Yesu Kristo akienda juu mbinguni.