Scripture Stories
Sura ya 45: Yesu Kristo Anafundisha kuhusu Sakramenti na Sala


Sura ya 45

Yesu Kristo Anatufundisha kuhusu Sakramenti na Sala

Picha
kikundi cha wanaume wakitembea

Yesu Kristo aliwatuma wafuasi wake waende wakalete mkate na divai. Aliwaambia Wanefi waketi chini.

Picha
Yesu akigawa mkate

Baada ya wanafunzi kurejea, Mwokozi aliumega mkate katika vipande vipande na kuubariki. Aliwapa wanafunzi wake na kuwataka wawapatie watu wengine pia.

Picha
Yesu akizungumza

Yesu alisema kwamba watu wanaoshiriki sakramenti wanaahidi daima kumkumbuka Yeye na dhabihu Yake. Kisha wanapokea Roho Wake.

Picha
watu wakigawa divai

Yesu Kristo alibariki divai na kutoa kiasi kwa wanafunzi Wake. Wanafunzi waliwapa watu divai kiasi.

Picha
Yesu akifundisha

Yesu alisema wale wanaoshiriki sakramenti wanaahidi kutii amri Zake.

Picha
Yesu akizungumza na wanafunzi

Yesu tena aliwaambia wanafunzi Wake kwamba kila mtu anayeshiriki sakramenti na kumkumbuka daima atakuwa na Roho Wake.

Picha
Yesu akizungumza na watu

Aliwaambia mitume wake wangebarikiwa kama wangetii amri Zake.

Picha
Yesu akizungumza na wanafunzi

Aliwaambia wasali kila wakati na wasali jinsi walivyokuwa wamemuona akisali.

Picha
Mwokozi akizungumza na kila mtu

Mwokozi aliwaambia Wanefi wote wasali kwa Baba wa Mbinguni kwa jina Lake. Pia aliwaamuru wasali pamoja na familia zao.

Picha
watu wakimsikiliza Kristo

Alisema watu lazima wakutane pamoja mara kwa mara. Wanapaswa kuwakaribisha wengine katika mikutano yao, kusali kwa niaba yao, na kuwa mifano mizuri kwao.

Picha
Yesu akienda juu mbinguni

Yesu aliwapatia wanafunzi Wake uwezo kutoa Roho Mtakatifu. Kisha mawingu yakawafunika watu kwa hivyo ni wanafunzi tu waliomuona Yesu Kristo akienda juu mbinguni.

Chapisha