Njoo, Unifuate
Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko Kwako Binafsi


“Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko Kwako Binafsi,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko Kwako Binafsi,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2020

Picha
mwanamke akisoma maandiko

Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko Kwako Binafsi

Hizi ni baadhi ya njia rahisi za kuboresha kujifunza kwako neno la Mungu katika maandiko:

Tafuta Ukweli kuhusu Yesu Kristo

Maandiko hutufundisha kwamba vitu vyote vinamshuhudia Kristo (ona 2 Nefi 11:4; Musa 6:63), kwa hivyo mtafute Yeye katika matukio, hadithi, na mafundisho ya Kitabu cha Mormoni. Fikiria kuandika au kuwekea alama mistari inayofundisha kuhusu Mwokozi na jinsi ya kumfuata.

Tafuta Maneno na Vifungu Vyenye Mwongozo

Unaweza kukuta kwamba maneno na vifungu fulani katika maandiko hukugusa wewe, kana kwamba yaliandikwa mahususi kwa ajili yako. Yanaweza kuwa na maana kwako binafsi na kukushawishi na kukuhamasisha. Fikiria kuyawekea alama katika maandiko yako au kuyaandika katika shajara ya kujifunzia.

Tafuta Ukweli wa Injili

Wakati mwingine ukweli wa injili (mara nyingi huitwa mafundisho au kanuni) unasemwa wazi, na wakati mwingine unatolewa kupitia mfano au hadithi. Jiulize, “Ni ukweli upi wa milele unafundishwa katika mistari hii?”

Msikilize Roho

Kuwa makini na mawazo na hisia zako, hata kama hayahusiani na kile unachosoma. Mawazo hayo yanaweza kuwa mambo hasa ambayo Mungu anakutaka ujifunze.

Linganisha Maandiko na Maisha Yako

Fikiria jinsi hadithi na mafundisho unayosoma yanavyohusiana na maisha yako. Kwa mfano, unaweza kujiuliza, “Je ni uzoefu gani niliopata ambao unafanana na hiki ninachosoma?” au “Ni kwa jinsi gani ninaweza kufuata mfano wa mtu huyu katika maandiko?”

Uliza Maswali Unapojifunza

Unapojifunza maandiko, maswali yanaweza kuja akilini. Maswali haya yanaweza kuhusiana na kile unachosoma au maisha yako kwa ujumla. Tafakari maswali haya na tafuta majibu kadiri unavyoendelea kujifunza maandiko.

Tumia Misaada ya Kujifunza Maandiko.

Ili kupata umaizi wa ziada katika mistari unayosoma, tumia marejeo, Mwongozo wa Mada, Kamusi ya Biblia, Mwongozo wa Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org), na misaada mingine ya kujifunza.

Zingatia Muktadha wa Maandiko

Unaweza kupata umaizi wa maana kuhusu maandiko kama utazingatia muktadha wake—hali au mazingira katika maandiko. Kwa mfano, kufahamu chimbuko na imani ya watu ambao nabii alizungumza nao kunaweza kukusaidia kuelewa dhamira ya maneno yake.

Andika Mawazo na Hisia zako

Kuna njia nyingi za kuandika mawazo ambayo hukujia unapojifunza. Kwa mfano, unaweza kuwekea alama neno lenye maana au kifungu na kuandika mawazo yako kama neno la kukumbuka katika maandiko yako. Unaweza pia kutunza shajara ya umaizi, hisia, na mawazo unayopata.

Jifunze Maneno ya Manabii na Mitume wa Siku za Mwisho

Soma kile ambacho manabii na mitume wa siku za mwisho wamefundisha kuhusu kanuni unazopata ndani ya maandiko (kwa mfano, ona conference.ChurchofJesusChrist.org na magazeti ya Kanisa).

Shiriki Umaizi

Kujadili umaizi kutokana na kujifunza kwako binafsi sio tu ni njia nzuri ya kuwafundisha wengine, bali pia husaidia kuimarisha uelewa wako katika kile ambacho umesoma.

Ishi kwa Kile Unachojifunza

Kujifunza maandiko hakupaswi tu kutupatia sisi msukumo lakini pia kunapaswa kutuongoza kwenye kubadilisha jinsi tunavyoishi. Sikiliza kile ambacho Roho anakushawishi kufanya unaposoma, na uweke sharti la kuufanyia kazi ushawishi huo.

Picha
mwanaume akisoma maandiko

Rais Russell M. Nelson alisema: “Kwa hivyo, kama tutasonga mbele, tukila na kusherehekea neno la Kristo, na tuvumilie hadi mwisho, … [sisi] tutapokea uzima wa milele’ [2 Nefi 31:20].

“Kusherehekea inamaanisha zaidi ya kuonja. Kusherehekea inamaanisha kufurahia. Tunafurahia maandiko kwa kujifunza kwayo katika moyo wa ugunduzi mwema na utii aminifu. Wakati sisi tunaposherehekea maneno ya Kristo, yanaingia ‘katika vibao ambavyo ni mioyo ya nyama.’ [2 Wakorintho 3:3]. Yanakuwa sehemu muhimu ya asili yetu” (“Kuishi Kulingana na Mwongozo wa Maandiko,” Ensign, Nov. 2000, 17).

Chapisha