Mafundisho na Maagano 2021
Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako


“Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Mawazo kwa ajili ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu binafsi na Familia: 2021

Picha
familia zikisoma maandiko

Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Maandiko kwa Familia Yako

Kujifunza kila mara maandiko kwa familia ni njia yenye nguvu zaidi katika kuisaidia familia yako kujifunza injili. Ni kiasi gani na kwa muda gani mnasoma kama familia siyo muhimu kama vile kuwa thabiti katika jitihada zenu. Unapofanya kujifunza kwako maandiko kuwa sehemu muhimu ya maisha ya familia yako, utawasaidia wanafamilia yako kuja karibu na Yesu Kristo na kujenga shuhuda zao juu ya msingi wa neno Lake.

Fikiria maswali yafuatayo:

  • Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuwatia moyo wanafamilia kusoma maandiko peke yao?

  • Je, unaweza kufanya nini cha kuwatia moyo wanafamilia kushiriki kile wanachojifunza?

  • Je, ni kwa jinsi gani unaweza kusisitiza kanuni unazojifunza katika Mafundisho na Maagano katika nyakati za kila siku za kufundisha?

Kumbuka kwamba nyumbani ni mahali bora pa kujifunza injili. Unaweza kujifunza na kufundisha injili nyumbani katika njia ambazo haziwezekani katika darasa la Kanisani. Kuwa mbunifu unapofikiria njia za kuisaidia familia yako kujifunza kutoka kwenye maandiko.

Mawazo ya Shughuli

Fikiria baadhi ya mawazo yafuatayo ili kuboresha kujifunza maandiko kwa familia yako:

Tumia muziki

Imbeni nyimbo zinazoimarisha kanuni zinazofundishwa katika maandiko. Wimbo uliopendekezwa au wimbo wa watoto umeorodheshwa katika kila muhtasari wa wiki. Unaweza kuuliza maswali kuhusu maneno au virai katika maneno ya nyimbo. Kwa kuongezea kwenye kuimba, familia yako inaweza kutenda vitendo vinavyoendana na nyimbo au kusikiliza nyimbo zikiimbwa taratibu wakati wakifanya shughuli zingine.

Shiriki maandiko yenye maana zaidi

Wape wanafamilia muda wa kuelezea vifungu vya maandiko ambavyo wameona vina maana zaidi wakati wa kujifunza kwao binafsi.

Tumia maneno yako mwenyewe

Waalike wanafamilia kufanyia muhtasari kwa maneno yao wenyewe kile wanachojifunza kutoka kwenye maandiko mnayojifunza.

Tumia maandiko katika maisha yako

Baada ya kusoma kifungu cha maandiko, waalike wanafamilia kuelezea jinsi kifungu hicho kinavyohusiana na maisha yao.

Uliza swali

Waalike wanafamilia kuuliza swali la injili, na kisha tumieni muda kutafuta mistari inayoweza kusaidia kujibu swali hilo.

Onesha andiko

Chagua mstari unaoona una maana, na ubandike mahali ambapo wanafamilia watauona mara kwa mara. Waalike wanafamilia wengine kufanya zamu ya kuchagua andiko la kubandika.

Tengeneza orodha ya maandiko

Kama familia, chagueni mistari kadhaa ambayo mngependa kujadili katika wiki itakayofuatia.

Kariri maandiko

Chagua kifungu cha maandiko ambacho kina maana kwa familia yako, na waalike wanafamilia kukikariri kwa kukirudia kila siku au kucheza mchezo wa kukariri.

Shiriki masomo ya vitendo

Tafuta vitu ambavyo vinahusiana na sura na mistari ambayo mnasoma kama familia. Waalike wanafamilia kuongelea jinsi kila kitu kinavyohusiana na mafundisho katika maandiko.

Chagua mada

Waalike wanafamilia kufanya zamu za kuchagua mada ambayo familia itajifunza pamoja. Tumia Mwongozo wa Mada, Kamusi ya Biblia, au Mwongozo kwenye Maandiko (scriptures.lds.org) ili kutafuta vifungu vya maandiko kuhusu mada.

Chora picha

Someni mistari michache kama familia, na kisha toa muda kwa wanafamilia kuchora kitu kinachohusiana na kile mnachokisoma. Tumieni muda kujadili mchoro wa kila mmoja.

Igiza hadithi

Baada ya kusoma hadithi, waalike wanafamilia kuiigiza. Baadaye, zungumzieni kuhusu jinsi hadithi inavyohusiana na mambo mnayopitia kibinafsi na kama familia.

Kufundisha Watoto

Kama una watoto wadogo katika familia yako, hizi ni baadhi ya shughuli zinazoweza kuwasaidia kujifunza:

Imba

Nyimbo za Kanisa na nyimbo kutoka Kitabu cha Nyimbo za Watoto zinafundisha injili kwa nguvu zaidi. Kila muhtasari katika nyenzo hii una wimbo uliopendekezwa. Unaweza pia kutumia faharasa ya mada nyuma ya Kitabu cha Nyimbo za Watoto kutafuta nyimbo zinazohusiana na kanuni za injili unazozifundisha. Wasaidie watoto wako kuhusianisha jumbe za nyimbo na maisha yao.

Sikiliza au igiza hadithi

Watoto wadogo wanapenda hadithi—kutoka kwenye maandiko, kutoka kwenye maisha yako, kutoka kwenye historia ya Kanisa, au kutoka kwenye magazeti ya Kanisa. Tafuta njia za kuwashirikisha kwenye usimuliaji wa hadithi. Wanaweza kushikilia picha au vitu, kuchora picha ya kile wanachokisikia, kuigiza hadithi, au hata kusaidia kusimulia hadithi. Wasaidie watoto wako kutambua kweli za injili katika hadithi unazowasimulia.

Soma andiko

Watoto wadogo wanaweza kushindwa kusoma mengi, lakini bado unaweza kuwahusisha katika kujifunza kutoka kwenye maandiko. Unaweza kuhitaji kujikita kwenye mstari mmoja, kifungu muhimu, au neno moja.

Tazama picha au angalia video

Uliza maswali kuhusu picha au video yenye uhusiano na kanuni ya injili mnayoijadili. Kwa mfano, unaweza kuuliza, “Je, ni nini kinatokea katika picha hii? Kinakufanya ujisikie vipi?” Gospel Library app, Gospel Media Library kwenye ChurchofJesusChrist.org, na children.ChurchofJesusChrist.org ni sehemu nzuri za kutafuta picha na video.

Buni

Watoto wanaweza kujenga, kuchora, au kupaka rangi kitu kinachohusiana na hadithi au kanuni wanazojifunza.

Shiriki katika masomo ya vitendo

Somo rahisi la vitendo linaweza kuwasaidia watoto wako kuelewa kanuni ya injili ambayo ni ngumu kueleweka. Unapotumia masomo ya vitendo, tafuta njia za kuwafanya watoto wako washiriki. Watajifunza zaidi kutoka kwenye matukio ya kuchangamana kuliko kwenye kuangalia tu onyesho likifanyika.

Igiza-nafasi

Watoto wanapoigiza-nafasi ya aina fulani watakayokutana nayo katika maisha halisi, wanaelewa vizuri zaidi jinsi kanuni ya injili inavyohusika kwenye maisha yao.

Rudia shughuli

Watoto wadogo wanaweza kuhitaji kusikia mawazo mara nyingi ili kuyaelewa. Kwa mfano, unaweza kusimulia hadithi ya maandiko mara nyingi katika njia tofauti—kusoma kutoka kwenye maandiko, kufanya muhtasari kwa maneno yako mwenyewe, kuwaacha watoto wako wakusaidie kusimulia hadithi, kuwaalika waigize hadithi, na kadhalika.

Fanya mahusiano kwenye kukuza malengo yao binafsi

Mafunzo ya maandiko kifamilia yanaweza kutoa msukumo kwa ajili ya vijana na watoto kuweka malengo kwa ajili yao kiroho, kimwili, kiakili, na ukuaji wa kijamii (ona Luka 2:52).

Picha
familia ikitabasamu pamoja

Kufundisha Vijana

Kama una vijana katika familia yako, hizi ni baadhi ya shughuli zinazoweza kuwasaidia kujifunza:

Waalike kufundisha

Tunajifunza zaidi tunapofundisha kitu fulani kuliko tunaposikia tu kukihusu. Wape vijana wako fursa kuongoza majadiliano ya familia kuhusu maandiko.

Fanya mahusiano kwenye seminari

Mwaka huu wanafunzi wa seminari wanajifunza Mafundisho na Maagano. Kama vijana wako wanahudhuria seminari, waalike kushiriki kile wanachojifunza huko.

Fananisha maandiko

Wakati mwingine vijana wanapata shida kuona jinsi mafundisho na kanuni katika maandiko yanavyohusiana na maisha yao. Wasaidie waone jinsi hadithi na mafundisho katika maandiko yanavyofanana na hali wanazokabiliana nazo nyumbani, shuleni, au na rafiki zao.

Uliza Maswali yanayohimiza kutafakari

Vijana wengi hujibu vyema maswali yanayowaruhusu kueleza mawazo yao na hisia kuhusu maandiko badala ya kurudia tu kile maandiko yanachosema. Kwa mfano, unaweza kuuliza, “Ni nini Bwana anaweza kuwa anafundisha katika mistari hii?” au “Kwa nini unafikiri ufunuo huu ungeweza kuwa wenye maana kwa Watakatifu katika miaka ya 1830?”

Fanya mahusiano kwenye kukuza malengo yao binafsi

Mafunzo ya maandiko kifamilia yanaweza kutoa msukumo kwa ajili ya vijana na watoto kuweka malengo kwa ajili yao kiroho, kimwili, kiakili, na ukuaji wa kijamii (ona Luka 2:52).

Kuwa muwazi kwa maswali yao

Swali kutoka kwa kijana ni fursa ya thamani ya kushiriki ukweli na kutafuta kuelewa juu ya mada ambayo yeye kwa dhahiri anaipenda. Usiwe mwoga wa maswali au kuyapuuza, hata kama yanaonekana hayana uhusiano na mada ya majadiliano. Ni sawa kama huna majibu yote. Nyumbani ni sehemu bora kwa ajili ya kutafuta majibu kwa pamoja.

Wahimize kushiriki utambuzi wao

Vijana wana mitazamo na utambuzi wa kipekee katika kuchangia kwenye mafunzo ya maandiko kifamilia. Wafanye wajue kwamba unapendelea kile Roho anachowafundisha kuhusu maandiko. Ungeweza hata kuwaomba kushiriki utambuzi kutoka kwenye kujifunza kwao binafsi.

Kuwa mwenye kubadilika kulingana na hali

Kama una kijana ambaye hayupo tayari kushiriki katika mafunzo ya maandiko kifamilia, tafuta njia nyingine ya mahusiano naye. Kwa mfano, je, unaweza kuitumia injili katika njia ya kawaida katika mazungumzo yenu au kushiriki andiko lenye maana katika njia ambayo haionekani kuwa ya kimahubiri au ya kulazimisha? Mafunzo ya maandiko hayatakiwi yaonekane ni yale yale katika kila familia. Baadhi ya watoto wanaweza kuitikia vizuri zaidi kwenye kujifunza maandiko wakiwa mmoja mmoja. Kuwa mwenye kusali na kufuata misukumo ya Roho.

Rais Russell M. Nelson alisema: “Ninakuahidi ya kwamba utakapofanya bidii kupanga upya nyumba yako kuwa kituo cha kujifunza injili, baada ya muda siku zako za Sabato zitakuwa za kupendeza sana. Watotowako watafurahia kujifunza na kuishi mafunzo ya Mwokozi, na ushawishi wa adui katika maisha yako na katika nyumba yako utapungua. Mabadiliko katika familia yako yatakuwa ya kuvutia na endelevu” (“Kuwa Mtakatifu wa Siku za Mwisho wa Mfano,” Ensign au Liahona, Nov. 2018, 113).

Chapisha