Njoo, Unifuate
Januari 14–20. Luka 2; Mathayo 2: Tumekuja Kumsujudia


“Januari 14–20.“Januari 14-20. Luka 2; Mathayo 2: Tumekuja Kumsujudia,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019 (2019)

“Januari 14–20.“Januari 14-20. Luka 2; Mathayo 2,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019

Picha
Mamajusi wakisafiri kwa ngamia.

Njooni Tumuabudu, na Dana Mario Wood

Januari 14–20

Luka 2; Mathayo 2

Tumekuja Kumsujudia

Anza kwa kusoma Luka 2 na Mathayo 2, na zingatia utambuzi wowote wa kiroho unaopokea. Mawazo ya kujifunza katika muhtasari huu yanaweza kukusaidia kutambua baadhi ya kanuni muhimu zaidi na zinazohusika katika sura hizi.

Andika Misukumo Yako

Toka siku ya kuzaliwa Kwake, ilikuwa wazi kwamba Yesu hakuwa mtoto wa kawaida. Haikuwa tu nyota mpya mbinguni au tangazo la shangwe la kimalaika ambalo lilifanya uchanga wa Yesu kuwa wa kipekee. Ilikuwa pia kweli kwamba makundi haya ya watu waaminifu—kutoka mataifa tofauti, taaluma, na historia—yalihisi mara moja kuvutwa Kwake. Hata kabla Hajatamka mwaliko Wake wa “njoo, unifuate,” walikuja (Luka 18:22). Sio kila mmoja alikuja Kwake, ndiyo—kulikuwa na wengi ambao hawakumjali, na mtawala mwenye wivu hata alitafuta uhai wake. Lakini wanyenyekevu, wasafi, wenye kuitafuta haki kwa bidii walipata walichokuwa wakitafuta Kwake. Bidii yao hutia msukumo ya kwetu, kwani “habari njema ya furaha kuu” iliyoletwa kwa wachungaji ilikuwa kwa “watu wote,” na “Mwokozi, ambaye ni Kristo Bwana” alizaliwa siku ile kwetu sote (ona Luka 2:10–11).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

Luke 2:1–7

Yesu Kristo alizaliwa katika mazingira ya unyeyekevu

Japokuwa Yesu Kristo alikuwa na utukufu na Mungu Baba “kabla ya ulimwengu kuwako” (Yohana 17:5), Alikuwa tayari kuzaliwa katika mazingira ya chini na kuishi kati yetu duniani. Unaposoma Luka 2:1–7, unapata taarifa gani kuhusu mazingira ya unyenyekevu ya kuzaliwa Kwake? Jaribu kutambua maelezo au umaizi katika hadithi hii ambao hukuutambua mwanzo. Unajifunza nini kuhusu Mwokozi kutoka kwenye mazingira ya kuzaliwa Kwake? Ni kwa jinsi gani umaizi huu huathiri hisia zako kwake?

Ona pia filamu “The Nativity” (LDS.org).

Luka 2:8–38; Mathayo 2:1–12

Kuna mashahidi wengi wa kuzaliwa kwa Kristo.

Kuzaliwa na uchanga wa Kristo kulisherekewa na mashahidi na waabuduo wenye weledi—wachungaji wanyenyekevu waliotembelea hori la ng’ombe, Mamajusi matajiri walioleta zawadi nyumbani Kwake, mjane aliyetumikia hekaluni, na mfuasi mwaminifu ambaye kwa wasiwasi alitazamia ujio wa Masiya. Unapopitia kwa undani hadithi zao, unajifunza nini kuhusu njia za kuabudu na kumshuhudia Kristo?

Mashahidi wa Kristo

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kushuhudia?

Mashahidi wa Kristo

Wachungaji (Luka 2:8–20)

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kushuhudia?

Mashahidi wa Kristo

Simioni (Luka 2:25–35)

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kushuhudia?

Mashahidi wa Kristo

Ana (Luka 2:36–38)

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kushuhudia?

Mashahidi wa Kristo

Mamajusi (Mathayo 2:1–12)

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kushuhudia?

Ona pia 1 Nefi 11:13–23; 3 Nefi 1:5–21; “Wachungaji wanajifunza kuhusu Kuzaliwa kwa Kristo” na “Mtoto Kristo Analetwa Hekaluni” (filamu, LDS.org).

Mathayo 2:13–23

Wazazi wanaweza kupokea ufunuo kuzilinda familia zao.

Yusufu kamwe asingeweza kufanya kile alichotakiwa kufanya—kumlinda Yesu katika utoto Wake—bila msaada wa mbinguni. Kama Mamajusi, alipokea ufunuo ambao ulimuonya dhidi ya hatari. Unaposoma kuhusu uzoefu wa Yusufu, fikiria kuhusu hatari za kimwili na kiroho ambazo hukabili familia leo. Tafakari uzoefu wakati ulipohisi muongozo wa Mungu katika kukulinda na familia yako au wapendwa wako. Fikiria kushiriki uzoefu huu na wengine. Unaweza kufanya nini kupokea mwongozo kama huo siku za baadaye?

Kwa kuongezea, unaweza kufikiria kuangalia video “The First Christmas Spirit” (LDS.org) kwa ufafanuzi wa namna gani Yusufu anaweza kuwa alihisi alipokutana na changamoto ya kumtunza Mwana wa Mungu.

Luka 2:40–52

Hata kama kijana, Yesu alizingatia kwenye kutenda mapenzi ya Baba Yake.

Kama kijana mdogo, Mwokozi alifundisha injili kwa nguvu kwamba hata walimu hekaluni walishangazwa na “uelewa na majibu” Yake (Luke 2:47). Unajifunza nini kutoka kwenye mistari hii kuhusu Mwokozi kama kijana mdogo? Ni kwa jinsi gani vijana wadogo unaowajua wanajaribu “kuwamo katika nyumba ya Baba [yao]”? (Luka 2:49). Ni kwa jinsi gani vijana na watoto wamekusaidia kupata uelewa mpana wa injili? Nini kingine unajifunza kutoka kwenye mfano wa utoto wa Yesu katika Luka 2:40–52 na katika Tafsiri ya Joseph Smith, Mathayo 3:24–26 (katika kiambatisho cha Biblia)?

Picha
Yesu kama mvulana mdogo na walimu hekaluni

“Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?” (Luka 2:49).

Tafsiri ya Joseph Smith ni Nini?

Kwa sababu kweli “nyingi rahisi na za thamani” zilipotea kutoka kwenye Biblia kwa karne nyingi (1 Nefi 13:28; ona pia Musa 1:41), Bwana alimuamuru Joseph Smith kufanya masahihisho yenye ufunuo ya Biblia, yajulikanayo kama Tafsiri ya Joseph Smith. Masahihisho mengi yaliyofanywa na Nabii yamejumuishwa kwenye kiambatisho cha toleo la maandiko ya Watakatifu wa Siku za Mwisho. Toleo la Biblia la King James la Watakatifu wa Siku za Mwisho pia lina marejeo pamoja na masahihisho ya Nabii. Tafsiri ya Joseph Smith ya Mathayo 24, ijulikanayo kama Joseph Smith—Mathayo, inaweza kupatikana katika Lulu ya Thamani Kuu. Kwa maelezo zaidi, ona Kamusi ya Biblia, “Tafsiri ya Joseph Smith”; “Bible, Inerrancy of,” Mada za Injili, topics.lds.org.

Picha
ikoni ya kujifunza kwa familia

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Kwa Familia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mapendekezo:

Luka 2

Waalike wanafamilia kuchagua mtu aliyeelezewa katika Luka 2, soma mistari michache kuhusu muingiliano wa mtu huyo na Mwokozi, na shiriki kitu ambacho wamejifunza ambacho huongeza imani yao katika Yesu Kristo. Imbeni pamoja “Mary’s Lullaby” au “The Nativity Song,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 44–45, 52–53. Unajifunza nini kutoka kwenye nyimbo hizi kuhusu kuzaliwa kwa Mwokozi?

Luka 2:49

Ni nini “mapenzi ya Baba”? (ona Musa 1:39). Tunajifunza nini kuhusu mapenzi hayo kutoka kwenye hadithi hii na kutoka kwenye mambo mengine Yesu aliyofanya na kufundisha maisha Yake yote? Fikiria kuandika baadhi ya njia familia yako inaweza kushiriki katika mapenzi ya Baba na kuziweka katika chupa kubwa. Wiki inayofuata, familia yako inapotafuta njia za kufanya kazi ya Baba wa Mbinguni, wanaweza kuchagua mawazo kutoka kwenye chupa kubwa. Panga muda ambapo mtashiriki uzoefu wenu.

Luka 2:52

Tunaweza kujifunza nini kutoka Luka 2:52 kuhusu jinsi Yesu aliendelea katika maisha Yake? Ni kwa njia zipi wanafamilia wanaweza kuongezeka “katika hekima na kimo, na kumpendeza Mungu na wanadamu”?

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Tumia vielelezo vya kujifunza maandiko. Kupata umaizi zaidi unaposoma maandiko, tumia nyenzo kama marejeo, Mwongozo wa Mada, Kamusi ya Biblia, Mwongozo kwenye Maandiko, na vielelezo vingine vya kujifunza kama vile LDS.org na Kitabu cha Kiada cha Mwanafunzi cha Agano Jipya (kitabu cha kiada cha Mfumo wa Elimu wa Kanisa, 2014).

Picha
Mariamu, Yusufu, na mtoto mchanga Yesu.

Mwokozi wa Ulimwengu alikuja duniani katika mazingira ya unyenyekevu.

Chapisha