Njoo, Unifuate
Novemba 4–10. Waebrania 1–6: ‘Yesu Kristo, ‘Sababu ya Wokovu wa Milele’’


“Novemba 4–10. Waebrania 1–6: ‘Yesu Kristo, ‘Sababu ya Wokovu wa Milele’’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2019 (2019)

“Novemba 4–10. Waebrania 1–6,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Yesu amesimama na msichana na mwanaume

Marhamu ya Giliadi na Anne Henrie

Novemba 4–10.

Waebrania 1:-6

“Yesu Kristo, ‘Sababu ya Wokovu wa Milele’”

Kuandika misukumo ya kiroho hukusaidia wewe kutambua kile ambacho Roho Mtakatifu anataka kukufundisha. Kufanyia kazi misukumo yako huonyesha imani yako kwamba ushawishi huo ni halisi.

Andika Misukumo Yako

Wote tunatakiwa kuacha kitu fulani ili tuweze kuikubali injili ya Yesu Kristo—iwe ni mazoea mabaya, imani zisizo sahihi, mahusiano yasiyo mazuri, au kitu kingine chochote. Kwa Wayunani, uongofu mara nyingi ilimaanisha kuiacha miungu ya uongo. Kwa Waebrania (Wayahudi), hata hivyo, uongofu ulithibitisha kuwa, kama si vigumu zaidi, ni wa kutatanisha kidogo. Hata hivyo, imani na tamaduni zao walizozipenda sana zilikuwa zimekita mizizi katika kuabudu Mungu wa kweli na mafundisho ya manabii Wake, ikirudi nyuma maelfu ya miaka. Bado Mitume walifundisha kwamba sheria ya Musa ilitimizwa katika Yesu Kristo na kwamba sheria ya juu zaidi sasa ilikuwa ndiyo kiwango kwa waaminio. Je, kuukubali Ukristo ingemaanisha kwamba Waebrania lazima waache imani na historia zao za mwanzo? Waraka kwa Waebrania ulitafuta kusaidia kumaliza maswali kama hayo kwa kufundisha kwamba sheria ya Musa, manabii, na ibada ni muhimu, lakini Yesu Kristo ni mkuu zaidi (ona Waebrania 1:1–4; 3:1–6; 7:23–28). Hata hivyo, mambo haya yote yanaelekeza kwa, na kushuhudia juu ya Kristo kama Mwana wa Mungu na Masiya mwahidiwa ambaye Wayahudi walikuwa wakimsubiri. Ujumbe kwa Waebrania, na kwetu sote, ni kwamba wakati mwingine lazima tuache tamaduni ili kumfanya Yesu Kristo kiini cha kuabudu kwetu na maisha yetu—kwani ni kupitia kwa Kristo “tunapata neema” (Waebrania 4:16).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

Waebrania

Nani aliandika Waraka huu kwa Waebrania?

Baadhi ya wasomi wametia shaka ikiwa Paulo aliandika Waraka huu kwa Waebrania. Mtindo wa maandishi wa Waebrania kwa kiasi fulani ni tofauti na barua zingine za Paulo, na matoleo ya maandishi ya mwanzo kabisa hayakutaja mwandishi. Hata hivyo, kwa sababu mawazo yaliyoelezewa katika Waebrania ni sawa na mafundisho mengine ya Paulo, Watakatifu wa Siku za Mwisho, katika kuendeleza utamaduni wa Ukristo, kwa ujumla wamekubali kwamba Paulo alijihusisha kwa kiasi fulani katika kuandika waraka huu.

Ona pia Kamusi ya Biblia, “Nyaraka za Paulo.”

Waebrania 1–5

Yesu Kristo ni “mfano dhahiri” wa Baba wa Mbinguni.

Wayahudi wengi waliona vigumu kumkubali Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu. Waraka kwa Waebrania hufundisha kwamba kila kitu kuhusu Yesu hushuhudia na ni mfano wa Baba Yake. Unaposoma sura tano za kwanza za Waebrania, unaweza kuweka orodha ya vyeo vya Yesu Kristo, majukumu, sifa, na kazi zilizotajwa. Je, mambo haya hukufundisha nini kuhusu Mwokozi? Je, yanakufundisha nini kuhusu Baba wa Mbinguni?

Je, kauli ifuatayo kutoka kwa Mzee Jeffrey R. Holland huongezea nini kwenye uelewa wako wa mafundisho katika sura hizi? “Yesu … alikuja kuboresha mtazamo wa mwanadamu juu ya Mungu na kuwaomba kumpenda Baba yao wa Mbinguni kama ambavyo Yeye daima amewapenda na daima atawapenda. … Hivyo kulisha wenye njaa, kuponya wagonjwa, kukemea unafiki, kuomba kwa ajili ya imani—huyu alikuwa ni Kristo akituonyesha njia ya kwenda kwa Baba” (“Sifa Kuu ya Mungu,” Ensign au Liahona, Nov. 2003, 72).

Waebrania 2:9–18; 4:12–16; 5:7–8

Yesu Kristo aliteseka majaribu na udhaifu ili kwamba Aweze kuelewa na kunisaidia mimi.

Je, unahisi kwamba unaweza “kukikaribia kwa ujasiri kiti cha neema” na kupata rehema? (Waebrania 4:16). Ujumbe mmoja wa Waraka kwa Waebrania ni kwamba bila kujali dhambi na udhaifu wetu, Mungu anaweza kufikiwa na neema Yake inapatikana. Je, unapata nini katika Waebrania 2:9–18; 4:12–16; 5:7–8 ambacho huimarisha kujiamini kwako kwamba Yesu Kristo atakusaidia kwenye changamoto zako za maisha? Fikiria kuandika katika shajara yako mawazo na hisia zako kuhusu yale ambayo Mwokozi amefanya kwa ajili yako.

Ona pia Mosia 3:7–11; Alma 7:11–1334.

Waebrania 3:7–4:11

Ili kupokea baraka za Mungu, lazima “nisifanye moyo wangu kuwa mgumu.”

Japokuwa walikuwa waongofu kwenye Ukristo, baadhi ya Watakatifu wa Kiyahudi waliona vigumu kukubali kikamilifu injili ya Yesu Kristo na baraka zake. Kwa kusimulia tena hadithi ya Waisraeli wa kale, Paulo alitumaini kuwashawishi Wayahudi kuepuka makosa waliyofanya mababu zao—kukataa baraka za Mungu kwa sababu ya kutokuamini. (Unaweza kusoma hadithi Paulo aliyogusia katika Hesabu 14:1–12, 26–35.)

Fikiria jinsi gani Waebrania 3:7–4:11 inavyoweza kutumika kwako. Ili kufanya hili, unaweza kutafakari maswali kama haya:

  • Ni kwa jinsi gani Waisraeli walimkasirisha Bwana? (Ona Waebrania 3:8–11). Je, matokeo ya kuwa na moyo mgumu ni nini ?

  • Je, ni wakati gani nimeruhusu moyo wangu kuwa mgumu? Je, kuna baraka zozote ambazo Mungu anataka kunipa ambazo sizipokei kwa sababu ya kukosa imani?

  • Je, ninaweza kufanya nini ili kukuza moyo laini na uliopondeka? (ona Etheri 4:15; Mithali 3:5–6; Alma 5:14–15).

Ona pia 1 Nefi 2:16; 15:6–11; Yakobo 1:7–8; Alma 12:33–36.

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Hapa kuna baadhi ya mapendekezo:

Waebrania 1:8–9

Ni kwa njia gani Yesu ameonyesha kwamba Anapenda haki na kuchukia uovu? Kama tuna matamanio yasiyo ya haki, tunaweza kufanya nini ili kuyabadilisha?

Waebrania 2:1–4

Je unaweza kufikiria juu ya somo la vitendo ili kusaidia familia yako kuelewa inamaanisha nini kushika kwa uthabiti kweli za injili “ambazo tumezisikia”? Unaweza kuelezea hili kwa mfano kwa kutumia kitu ambacho ni vigumu kukishikilia. Je, ni kwa jinsi gani juhudi zetu za kudumisha ushuhuda zinafanana na kushika na kung’ang’ania kitu hiki? Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kuhakikisha kwamba “mambo tuliyosikia” “hayaondoki” kwetu? (mstari 1).

Waebrania 2:9–10

Kutafiti kirai “kiongozi mkuu wa wokovu,” unaweza kuanza kwa kujadili kiongozi ni nani. Kiongozi ana kazi gani? Je, ni kwa kwa jinsi gani Yesu Kristo ni sawa na kiongozi kwetu sisi na wokovu wetu?

Waebrania 5:1–5

Mistari hii inaweza kukusaidia kuwa na majadiliano kuhusu inamaanisha nini kuitwa na Mungu kuwa na ukuhani au kutimiza miito mingine ya Kanisa na mtu mwenye mamlaka. Je, tunaweza kujifunza nini kutoka katika mfano wa Yesu Kristo kuhusu kupokea na kutimiza miito?

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Jaribu mbinu zingine. Badala ya daima kujifunza maandiko katika njia inayofanana, fikiria mawazo tofauti ya kujifunza. Kwa baadhi ya mawazo, ona “Mawazo ya Kuboresha Kujifunza Kwako Binafsi Maandiko” mwanzoni mwa nyenzo hii.

Picha
Kristo anawatokea Wanefi

Kristo Akitembelea Ulimwengu Mpya, na Walter Rane

Chapisha