Agano Jipya 2023
Desemba 4–10. Ufunuo 1–5: “Utukufu, na Ukuu, Una … Mwana Kondoo Milele’”


“Desemba 4–10. Ufunuo 1–5: ‘Utukufu, na Ukuu, Una … Mwana Kondoo Milele’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

“Desemba 4–10. Ufunuo 1–5,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
mwanakondoo ameketi juu ya nyasi

Desemba 4–10

Ufunuo 1–5

“Utukufu, na Ukuu, Una … Mwana Kondoo Milele”

Fikiria kuandika maswali uliyonayo kuhusu kile unachosoma katika Ufunuo. Kisha unaweza kutafuta majibu ya maswali yako au kuyajadili na mwanafamilia au katika madarasa ya kanisani.

Andika Misukumo Yako

Je, umewahi kutatizika kuwaelezea wengine kile ulichohisi wakati wa tukio lenye nguvu za kiroho? Lugha kila siku inaweza kuonekana isiyotosheleza kuelezea hisia na misukumo ya kiroho. Pengine hii ndiyo sababu Yohana alitumia ishara nyingi kama hizo na tamathali za semi kuelezea ufunuo wake mtukufu. Angeweza kiurahisi kuelezea kwamba alimuona Yesu Kristo, lakini kutusaidia kuelewa tukio lake hili, alimuelezea Mwokozi kwa kutumia maneno kama haya: “macho yake yalikuwa kama mwali wa moto,” “kwenye kinywa chake kulitoka upanga mkali wenye makali kuwili,” na “uso wake kama jua liking’aa kwa nguvu zake” (Ufunuo 1:14–16). Unaposoma kitabu cha Ufunuo, jaribu kugundua jumbe ambazo Yohana alitaka ujifunze na kuhisi, hata kama huelewi maana iliyoko ndani ya kila ishara. Kwa nini aliweza kufananisha mikusanyiko ya Kanisa na vinara vya mshumaa, Shetani na mnyama, na Yesu Kristo na mwana kondoo? Hatimaye, siyo lazima kuelewa kila ishara katika Ufunuo ili kuelewa dhamira yake muhimu, ikijumuisha dhamira yake kuu kuliko zote: Yesu Kristo na wafuasi Wake watashinda dhidi ya falme za watu na dhidi ya Shetani.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Ono la Yohana linatufundisha kuhusu mpango wa Baba wa Mbinguni wa kuwaokoa watoto Wake.

Kitabu cha Ufunuo kinaweza kuwa kigumu kukielewa, lakini usikate tamaa. Ahadi ya Yohana inaweza kukushawishi kuendelea kujaribu: “Heri wasomao, na wao wayasikiao na kuelewa maneno ya unabii huu, na kuyashika yale mambo yaliyoandikwa humo, kwa maana wakati wa kurudi kwa Bwana u karibu” (Tafsiri ya Joseph Smith, Ufunuo 1:3 [katika kielezo cha Biblia], msisitizo umeongezwa).

Njia mojawapo ya kujifunza Ufunuo ni kutafuta muunganiko kwenye mpango wa wokovu. Muhtasari huu wa jumla unaweza kukusaidia:

Unaposoma, jiulize mwenyewe, “Hili linanifundisha nini kuhusu mpango wa Mungu? Mungu amefanya nini ili kunisaidia kushinda uovu na kurudi Kwake? Je, ahadi Zake ni zipi kwa walio waaminifu?

Ingeweza pia kuwa msaada kujua kwamba Mafundisho na Maagano 77 huelezea baadhi ya ishara zilizotumiwa katika Ufunuo. Kwa nyongeza, Tafsiri ya Joseph Smith hufafanua vifungu kadhaa katika Ufunuo, kwa hiyo angalia tanbihi na kiambatisho cha Biblia mara kwa mara.

Ona pia Kamusi ya Biblia, “Yohana” na “Ufunuo wa Yohana

Ufunuo 1

Yesu Kristo ni Mwana aliye Hai wa Mungu aliye Hai.

Sura ya kwanza ya Ufunuo huelezea Yesu Kristo akimtokea Yohana katika ono. Pengine ungeweza kutengeneza orodha ya kila kitu ambacho sura hii inasema kuhusu Yesu Kristo, ikijumuisha Yeye ni nani, Yeye hutufanyia nini, na jinsi Yeye alivyo.

Baadhi ya vitu unavyojifunza vitatokana na ishara hizi. Tafakari kile ambacho Bwana yaweza kuwa anajaribu kukufundisha kuhusu Yeye Mwenyewe kupitia ishara hizi. Kwa mfano, kumbuka kwamba Mwokozi hujiita Mwenyewe “mwanzo na mwisho” na “wa kwanza na wa mwisho.” Kwa nini unafikiri majina haya ni muhimu? Je, majina haya hukufundisha nini wewe kuhusu Mwokozi?

Ufunuo 2–3

Yesu Kristo ananijua mimi binafsi na atanisaidia kushinda changamoto zangu.

Maneno ya Mwokozi katika Ufunuo 2–3 hufunua kwamba Yesu alielewa mafanikio na masumbuko ya kipekee kwa kila tawi la Kanisa katika siku ya Yohana. Yeye alisifu juhudi za Watakatifu na pia kuwaonya wao juu ya vitu walivyohitaji kubadilika. Unajifunza nini kutokana na kusifu na maonyo ya Mwokozi?

Mwokozi pia anaelewa kufanikiwa kwako na mahangaiko yako, na anataka kukusaidia. Tazama ahadi za kila mara Yeye anazotoa kwa wale wanaoshinda. Kitu gani kinakuvutia kuhusu ahadi hizi? Ni kitu gani yawezekana Bwana anataka wewe ukishinde? Unaweza kufanya nini ili kupokea msaada Wake?

Ufunuo 4–5

Ni Yesu Kristo pekee ambaye angeweza kufanya mpango wa Baba wa Mbinguni uwezekane.

Je, unajifunza nini juu ya Baba wa Mbingu kutoka kwenye Ufunuo 4 na kuhusu Yesu Kristo kutoka kwenye Ufunuo 5? Fikiria vile ambavyo ilikuwa wakati sisi wote tulipotambua kwamba Yesu Kristo (“Mwana Kondoo”) angefanya mpango wa Baba wa Mbinguni uwezekane (Mwokozi angeweza “kufungua kitabu, na … kuvunja ile mihuri saba” [Ufunuo 5:5]). Kwa nini Yesu Kristo pekee ndiye angeweza kufanya hili? Ni kwa jinsi gani unaweza kuonyesha imani yako Kwake kama Mwokozi wako?

Ona pia Ayubu 38:4–7; Mafundisho na Maagano 77:1–7.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Ufunuo 1:20.Kwa nini Yesu alilinganisha Kanisa Lake na vinara vya taa? (ona Mathayo 5:14–16.) Imbeni pamoja wimbo kuhusu jinsi gani tunaweza kuwa nuru kwenye kinara cha taa, kama vile “Shine On” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 144).

Ufunuo 2– 3.Jifanye kana kwamba Yohana aliombwa kutoa ujumbe kwa familia yako kama ule alioutoa kwa makanisa wakati wa kipindi chake. Je, nini ambacho angesema kinakwenda vizuri? Je, ni kwa namna gani mngeweza kuboresha?

Ufunuo 3:15–16.Baada ya kusoma aya hizi, familia yako ingeweza kunywa kinywaji cha uvuguvugu ambacho kinanoga vizuri kinapokuwa moto au baridi. Inamaanisha nini kuwa vuguvugu kiroho?

Ufunuo 3:20.Onyesha picha ya Mwokozi akibisha mlangoni (ona mwisho wa muhtasari huu) wakati familia yako inaposoma Ufunuo 3:20. Kwa nini Yesu anabisha badala ya kuingia ndani moja kwa moja? Wanafamilia wangeweza kupeana zamu ya kubisha mlangoni. Kisha mtu mwingine katika familia angependekeza jinsi tunayoweza “kufungua mlango” kwa Mwokozi na kumruhusu mwanafamilia yule aingie ndani. Ni kwa jinsi gani tungejisikia kuwa na Mwokozi nyumbani kwetu?

Ufunuo 4:10–11.Inamaanisha nini kumwabudu Baba wa Mbinguni? Tunajua nini kumhusu Yeye ambacho kinatufanya sisi kutaka kumwabudu?

Ufunuo 5: 6, 6–13.Kwa nini Yesu Kristo anaitwa “Mwanakondoo”? Jina hili linatufundisha nini kumhusu Yeye?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Jesus, Once of Humble Birth,” Nyimbo za Kanisa, na. 196.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Himiza maswali. Maswali ni kiashirio kwamba wanafamilia wako tayari kujifunza na kutoa umaizi wa jinsi wanavyoitikia katika kile wanachofundishwa. Wafundishe familia yako jinsi ya kutafuta majibu katika maandiko. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26.)

Picha
Kristo akibisha mlangoni

Mkaribishe ndani, na Greg K. Olsen

Chapisha