Agano Jipya 2023
Novemba 27–Desemba 3. 1–3 Yohana; Yuda: “Mungu ni Pendo”


“Novemba 27–Desemba 3. 1–3 Yohana; Yuda: ‘Mungu ni Pendo’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2023)

“Novemba 27–Desemba 3. 1–3 Yohana; Yuda,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
Yesu Kristo akitabasamu akiwa amekaa na watoto wanaotabasamu

Upendo Mkamilifu, na Del Parson

Novemba 29–Desemba 3

1–3 Yohana; Yuda

“Mungu ni Pendo”

Unaposoma nyaraka za Yohana na Yuda, tafuta mwongozo wa kiungu kuhusu jinsi unavyoweza kuonyesha upendo wako kwa Mungu. Andika misukumo hii na uifanyie kazi.

Andika Misukumo Yako

Wakati Yohana na Yuda walipokuwa wakiandika nyaraka zao, mafundisho potofu tayari yalikuwa yameanza kuwaongoza Watakatifu wengi kwenye ukengeufu. Baadhi ya walimu wa uongo walikuwa hata wakitia shaka kama kweli Yesu Kristo alikuwa amekuja “katika mwili” (ona, kwa mfano, 1 Yohana 4:1–3; 2 Yohana 1:7). Je, kiongozi wa Kanisa angefanya nini katika hali kama hii? Hivyo Mtume Yohana alijibu kwa kushiriki ushahidi wake binafsi juu ya Mwokozi: “Huu ni ushuhuda ambao tunatoa wa lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima” (Tafsiri ya Joseph Smith, 1 Yohana1:1 [katika 1 Yohana 1:1, tanbihi a]). Na kisha Yohana akafundisha kuhusu upendo: upendo wa Mungu kwetu na upendo tunaopaswa kuwa nao Kwake na kwa watoto Wake wote. Hata hivyo, Yohana alikuwa shahidi wa hayo pia. Yeye alikuwa amepata uzoefu binafsi wa upendo wa Mwokozi (ona Yohana 13:23; 20:2), na alitaka Watakatifu kuhisi upendo huo huo. Ushuhuda na mafundisho ya Yohana juu ya upendo ndiyo tunayohitaji tu leo, wakati imani katika Yesu Kristo inapotiliwa shaka na mafundisho ya uongo kukithiri. Kusoma nyaraka za Yohana kunaweza kutusaidia kukabiliana na dhiki za leo kwa ujasiri, kwani “hamna hofu; lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu” (1 Yohana 4:18).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

1 Yohana; 2 Yohana

Mungu ni nuru, na Mungu ni pendo.

Kama ingebidi uchague neno moja au mawili kumuelezea Mungu, maneno hayo yangekuwa yapi? Katika nyaraka zake, Yohana alitumia maneno “nuru” na “pendo” (ona, kwa mfano, 1 Yohana 1:5; 2:8–11; 3:16, 23–24; 4:7–21). Unaposoma nyaraka mbili za kwanza za Yohana, tafakari uzoefu ambao Yohana alikuwa nao kuhusu nuru na upendo wa Mwokozi. Kwa mfano, fikiria kile Yohana alichojifunza kutokana na mafundisho ya Yesu katika Yohana 3:16–17; 12:35–36, 46; 15:9–14; 19:25–27. Je, unaona mifanano yoyote kati ya mafundisho haya na kile ambacho 1 Yohana hufundisha kuhusu nuru na upendo wa Mungu? Ni jambo gani limekufundisha kwamba Mungu ni nuru na upendo?

1 Yohana 2–4; 2 Yohana

“Kama tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu.”

Utapata pia maneno kama “kaa” na “ishi” yakirudiwa kote katika nyaraka za Yohana. Tafuta maneno haya, hasa unaposoma 1 Yohana 2–4 na 2 Yohana. Unafikiri inamaanisha nini “kukaa” au “kuishi” katika Mungu na Mafundisho Yake? (ona 2 Yohana 1:9). Inamaanisha nini kwako wewe kuwa na Mungu “akikaa” au “kuishi” ndani yako?

1 Yohana 2:243:3

Ninaweza kuwa kama Yesu Kristo.

Je, lengo la kuwa kama Kristo limewahi kuonekana kuwa la juu sana kwako? Fikiria ushauri wa Yohana wa kutia moyo: “Watoto wadogo, kaeni ndani yake; ili kusudi, atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri … [na] tutafanana naye” (1 Yohana 2:28; 3:2). Ni kitu gani unakipata katika 1 Yohana 2:243:3 ambacho kinakupa kujiamini na faraja kama mfuasi wa Yesu Kristo? Unapojifunza nyaraka za Yohana, tafuta kanuni zingine au ushauri unaoweza kukusaidia katika juhudi zako za kuwa zaidi kama Kristo.

Ona pia Moroni 7:48; Mafundisho na Maagano 88:67–68; Scott D. Whiting, “Kuwa kama Yeye,” Liahona, Nov. 2020, 12–14.

1 Yohana 4:12.

Hakuna “mtu … aliyemwona Mungu wakati wowote”?

Tafsiri ya Joseph Smith, 1 Yohana 4:12 hufafanua kwamba “hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote, isipokuwa wale wanaoamini” (katika 1 Yohana 4:12, tanbihi a; ona pia Yohana 6:46; 3 Yohana 1:11). Maandiko yana matukio kadhaa ambapo Mungu Baba amejionyesha Mwenyewe kwa watu waaminifu, akiwemo Yohana mwenyewe (ona Ufunuo 4; ona pia Matendo ya Mitume 7:55–56; 1 Nefi 1:8; Mafundisho na Maagano 76:23; Joseph Smith—Historia ya 1:16–17).

1 Yohana 5

Ninapoonyesha imani katika Yesu Kristo na nimezaliwa upya, ninaweza kuushinda ulimwengu.

Unaposoma 1 Yohana 5, tafuta nini tunapaswa kufanya ili kuushinda ulimwengu na kupata uzima wa milele. Kuushinda ulimwengu kunaweza kuonekanaje katika maisha yako? Unaweza pia kupata majibu na umaizi katika ujumbe wa Mzee Neil L. Andersen “Kuushinda Ulimwengu” (Liahona, Mei 2017, 58–62).

Yuda 1

[Jijengeni] juu ya imani yenu iliyo takatifu sana.”

Je, Yuda 1:10–19 inakufundisha nini kuhusu wale wanaopigana dhidi ya Mungu na kazi Yake? Unajifunza nini kutoka kwenye mstari wa 20–25 kuhusu jinsi ya kuweka imani yako katika Kristo kuwa imara?

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

1 Yohana 2:8–11.Ili kuisaidia familia yako kutafakari mafundisho ya Yohana, kusanyikeni katika chumba chenye giza ili wanafamilia waweze kupata uzoefu wa tofauti kati ya kutembea “gizani” na kutembea “nuruni.” Je, ni kwa jinsi gani chuki hutusababisha kutembea gizani na kujikwaa? Je, ni kwa jinsi gani kupendana sisi kwa sisi huleta nuru katika maisha yetu?

1 Yohana 3:21–22.Ni kipi katika mistari hii huongeza “ujasiri” ambao tunao katika Mungu na katika uwezo wetu wa kupokea majibu ya sala zetu?

Picha
familia ikiwa imepiga magoti pamoja katika sala

Kutii amri za Mungu hutusaidia kuushinda ulimwengu.

1 Yohana 5:2–3.Je, kuna amri zozote ambazo tunadhani kuwa ni “nzito” au ngumu kuzifuata? Ni jinsi gani upendo wetu kwa Mungu hubadilisha jinsi tunavyohisi kuhusu amri Zake?

3 Yohana 1:4.Inamaanisha nini “kutembea katika kweli”? Ungeweza kuchukua fursa hii kuwaambia wanafamilia jinsi wewe ulivyowaona wakitembea katika kweli na uzungumze kuhusu furaha iletwayo na hili. Wanafamilia wangeweza kufurahia kuandika kuhusu au kuchora kweli walizojifunza kwenye karatasi iliyochorwa nyayo za miguu na kuzitumia kutengeneza njia ambazo familia yako itaweza kutembelea kwa pamoja.

Yuda 1:3–4.Je, kuna hatari zozote za kiroho ambazo “zimepenyeza ndani” ya maisha yetu na familia zetu? (Yuda 1:4). Ni kwa jinsi gani tunaweza kufuata onyo la Yuda la “kwa bidii kuishindania imani” na kuepukana na hatari hizi? (Yuda 1:3). Je, tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba “amani, na upendo, vinaongezeka” katika familia yetu? (Yuda 1:2).

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Where Love Is,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 138–39.

Kuboresha Kujifunza Binafsi.

Tafuta upendo wa Mungu. Rais M.Russell Ballard alifundisha, “[Hii] injili ni injili ya upendo—upendo kwa Mungu na upendo kwetu sisi kwa sisi” (“Upendo wa Mungu kwa Watoto Wake,” Ensign, Mei 1988, 59). Unaposoma maandiko, fikiria kuandika ushahidi wa upendo wa Mungu.

Picha
Kristo akitembea ufukoni mwa ziwa

Tembea Nami, na Greg K. Olsen

Chapisha