Njoo, Unifuate
Novemba 2–8. Mormon 7–9: “Ninawazungumzia kama Vile Mko Hapa”


“Novemba 2–8. Mormon 7–9: ‘Ninawazungumzia kama Vile Mko Hapa,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Novemba 2–8. Mormon 7–9,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2020

Picha
Moroni akiandika kwenye bamba za dhahabu

Moroni Akiandika kwenye Bamba za Dhahabu, na Dale Kilborn

Novemba 2–8

Mormoni 7–9

“Ninawazungumzia kama Vile Mko Hapa”

Unaposoma Mormoni 7–9, fikiria kuhusu kile unachotamani zaidi watoto unaowafundisha wakijue. Weka mipango ya kufundisha kweli unazohisi zitabariki maisha yao.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Pitisha nakala ya Kitabu cha Mormoni. Waalike watoto, ikifika zamu yao kushikilia kitabu, kushiriki jambo moja walilojifunza kutoka kwenye Kitabu cha Mormoni. Ikiwa wanahitaji usaidizi, wakumbushe kuhusu mambo waliyojifunza darasani hivi karibuni.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mormoni 7:8–10

Kitabu cha Mormoni na Biblia vyote vinashuhudia juu ya Yesu Kristo.

Mormoni alifundisha kwamba Kitabu cha Mormoni kiliandikwa kutusaidia kuamini Biblia na kwamba wale wote wanaoamini Biblia wataamini Kitabu cha Mormoni.

Shughuli za Yakini

  • Waonyeshe watoto ukurasa wa jina wa Kitabu cha Mormoni, na uonyeshe maneno ya kichwa cha habari wakati ukikisoma, ukisisitiza neno mwingine. Wasaidie watoto kufikiria vitabu vingine vya maandiko ambavyo hutufundisha kuhusu Yesu. Waonyeshe kwamba Biblia ina Agano la Kale na Agano Jipya. Wasaidie watoto kusema “Agano la Kale, Agano Jipya” wakati unapoonyesha Biblia na “Ushuhuda Mwingine” wakati unapoonyesha Kitabu cha Mormoni.

  • Onyesha ramani ya ulimwengu au ukurasa wa shughuli wa muhtasari huu, pamoja na Biblia na Kitabu cha Mormoni. Tumia vitu hivi kuwafundisha watoto kwamba Biblia ni kumbukumbu ya mafundisho ya Yesu katika na kuzunguka Yerusalemu na Kitabu cha Mormoni ni kumbukumbu ya mafundisho Yake katika Amerika.

  • Chagua matukio na kweli kadhaa ambazo vyote Biblia na Kitabu cha Mormoni hushuhudia, kama vile kuzaliwa kwa Yesu, kifo, na Ufufuo. Onyesha picha kutoka kwenye Kitabu cha Sanaa ya Injili ambazo zinaelezea matukio na kweli hizi. Waombe watoto waelezee kile wanachoona katika picha, na waambie kwamba vyote Biblia na Kitabu cha Mormoni hufundisha kuhusu vitu hivi.

Mormoni 8:3

Ninaweza kuchagua mema hata wakati ninapohisi nipo peke yangu.

Moroni alikuwa Mnefi wa mwisho mwenye haki, lakini alibaki mwaminifu kwenye ushuhuda wake. Wasaidie watoto kujifunza kutoka kwenye mfano wake.

Shughuli za Yakini

  • Soma Mormoni 8:3, ukisisitiza kwamba Moroni alikuwa peke yake, lakini bado alitii amri, ikijumuisha amri ya kumalizia Kitabu cha Mormoni. Shiriki wakati ambapo ulikuwa mwaminifu hata wakati ulipohisi kuwa peke yako.

  • Baada ya kujadili mfano wa Moroni, shiriki baadhi ya mazingira ambapo mtoto lazima afanye uamuzi wa kuchagua mema au la, hata kama hakuna anayetazama. Moroni alifanya nini?

  • Imba pamoja na watoto wimbo kuhusu kuchagua mema, kama vile “Stand for the Right” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 159). Kwa nini ni muhimu kuchagua mema wakati wote, hata wakati uko peke yako?

Mormoni 9:7–21

Mungu ni “Mungu wa miujiza.”

Wasaidie watoto kuelewa kwamba miujiza ni muhimu katika kazi ya Mungu na kwamba Mungu atafanya miujiza pale watu Wake wanapokuwa na imani.

Shughuli za Yakini

  • Elezea kwamba muujiza ni jambo ambalo Mungu hufanya kuonyesha nguvu Zake na kubariki maisha yetu (ona Kamusi ya Biblia, “Miujiza”). Soma maneno na vifungu vya maneno kutoka Mormoni 9:11–13, 17 ambavyo huelezea baadhi ya miujiza ya Mungu. Wasaidie watoto kufikiria miujiza mingine inayopatikana katika maandiko (picha kutoka Kitabu cha Sanaa ya Injili, kama vile na. 26, 40, 41, na 83, zinaweza kusaidia). Shuhudia kwamba Mungu alitenda miujiza nyakati za kale na Yeye bado anatenda miujiza leo.

  • Shiriki uzoefu wako wakati ulipoona miujiza Kanisani katika siku hizi au katika maisha yako mwenyewe. Toa ushuhuda wako kwamba Mungu ni “Mungu wa miujiza” (Mormon 9:11).

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mormoni 7:8–10

Kitabu cha Mormoni na Biblia vyote vinashuhudia juu ya Yesu Kristo.

Mormoni alifundisha kwamba “injili ya Kristo … itawekwa mbele [yetu]” kwenye vyote Biblia na Kitabu cha Mormoni. Fikiria ni kwa jinsi gani utawafundisha watoto kwamba vitabu vyote viwili vitakatifu ni muhimu kwetu.

Shughuli za Yakini

  • Andika Mormoni 7:9 ubaoni, lakini acha nafasi zilizo wazi sehemu zenye maneno haya na hayo. Pia andika ubaoni haya = Kitabu cha Mormoni na hayo = Biblia. Waalike watoto wasome Mormoni 7:9 kwa sauti na kutumia vifungu vya maneno ubaoni kujaza nafasi zilizo wazi. Ni nini tunajifunza kuhusu Biblia na Kitabu cha Mormoni kutoka kwenye mistari hii?

  • Onyesha Kitabu cha Mormoni pamoja na Biblia. Shiriki hadithi kadhaa kutoka kwenye kila kitabu, ukionyesha picha kama zipo (ona Kitabu cha Sanaa ya Injili). Waalike watoto waonyeshe kitabu ambamo hadithi inapatikana. Kwa nini tunahitaji vitabu vyote viwili?

  • Andika kila neno la makala ya nane ya imani katika vipande tofauti vya karatasi. Toa neno moja au mawili kwa kila mtoto, na waalike watoto kufanya kazi pamoja ili kuweka maneno katika mpangilio sahihi. Kisha waombe warudie makala hiyo ya imani mara kadhaa. Je, makala hiyo inatufundisha nini?

    Picha
    Nakala za Kitabu cha Mormoni katika lugha tofauti

    Kitabu cha Mormoni kinashuhudia juu ya Yesu Kristo.

Mormoni 8:1–7

Ninaweza kuchagua mema hata wakati ninapohisi nipo peke yangu.

Kujitolea kwa Mormoni “kumaliza amri ya baba [yake],” japokuwa baba yake alikuwa amefariki, kunaweza kuwapatia msukumo watoto kutii amri za Mungu.

Shughuli za Yakini

  • Soma Mormoni 8:1–7 pamoja na watoto, na waalike washiriki ni kwa jinsi gani wangehisi kama wangekuwa Moroni. Waombe kutafuta tena kwenye mstari wa 1, 3, na 4 kupata kile Moroni alichoamriwa kufanya. Ni kwa jinsi gani Moroni “alimaliza amri ya baba [yake]”? Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwa zaidi kama Moroni?

  • Waalike watoto kila mmoja kuandika mazingira ambapo wanapaswa kufanya uchaguzi kati ya mema na mabaya wakati ambapo hakuna anayetazama. Weka mawazo yao ndani ya chombo, na waruhusu watoto kufanya zamu kuchagua mazingira na kushiriki kile ambacho wangefanya kuwa kama Moroni.

Mormoni 8:24–26; 9:7–26

Mungu ni “Mungu wa miujiza.”

Kuna watu wengi leo ambao hawaamini kwamba miujiza bado inatendeka. Tumia mafundisho ya Moroni katika mistari hii kuwafundisha watoto kwamba wakati tunapokuwa na imani, tunaweza kuona Mungu akitenda miujiza katika maisha yetu.

Shughuli za Yakini

  • Waonyeshe watoto maelezo ya upishi. Nini kingetokea kama ungesahahu kiungo muhimu? Waalike watoto kutafuta Mormoni 8:24 na 9:20–21 kupata “kiungo” muhimu tunachopaswa kuwa nacho kabla ya Mungu kutenda miujiza. Shiriki mifano ya miujiza—mikubwa au midogo—ambayo umeiona Kanisani au katika maisha yako. Waalike watoto kushiriki mifano yao.

  • Wagawe watoto katika timu mbili. Alika kila timu kutafuta mifano ya miujiza katika maandiko haya au baadhi ya haya: Mormoni 8:24; 9:11–13, 16–18, 21–25. Ni nini tunaweza kumwambia mtu anayedhani miujiza haitendeki tena? (ona Mormoni 9:9, 15–21).

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wahimize watoto kumuuliza mwana familia kuelezea muujiza ambao umeimarisha ushuhuda wake.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Watoto wanaweza kutambua ushawishi wa Roho. Wafundishe watoto kwamba hisia za amani, upendo, na ukunjufu walizonazo wakati wanapoongea au kuimba kuhusu Yesu Kristo na injili Yake zinatoka kwa Roho Mtakatifu (ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 11).

Chapisha