Njoo, Unifuate
Oktoba 26–Novemba1. Mormoni 1–6: “Ningetaka Kwamba Ningewashawishi Wote … Kutubu”


“Oktoba 26–Novemba1. Mormoni 1–6: ‘Ningetaka Kwamba Ningewashawishi Wote … Kutubu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Oktoba 26–Novemba1. Mormoni 1–6,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2020

Picha
Mormoni akiandika kwenye bamba za dhahabu

Mormon Akifupisha Maandishi ya Mabamba, na Tom Lovell

Oktoba 26–Novemba1

Mormoni 1–6

“Ningetaka Kwamba Ningewashawishi Wote … Kutubu”

Matukio yaliyoelezewa katika Mormoni 1–6 yanaweza kuwa magumu kwa watoto kuelewa kikamilifu, lakini bado wanaweza kujifunza kutoka kwenye maelezo ya Mormoni ya kuishi kwa haki katika ulimwengu wenye uovu. Ni kwa jinsi gani unaweza kutumia uzoefu wake kuwafundisha watoto jinsi ya kubaki wakwelli kwenye injili?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Je, watoto wanajua nini kuhusu Mormoni? Waalike kushiriki kile wanachojua au kile walichojifunza pamoja na familia zao. Kuonyesha picha ya Mormoni, kama ile iliyoko kwenye muhtasari wa wiki iliyopita katika Njoo Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia ingeweza kusaidia.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mormoni 1:1–3

Ninaweza kuwa mwenye haki kama Mormoni.

Japokuwa watoto unaowafundisha ni wadogo, wanaweza kujenga sifa za kiroho na kuishi kwa haki.

Shughuli za Yakini

  • Soma Mormoni 1:1–3 kwa watoto, au tumia “Mlango wa 49: Mormoni na Mafundisho Yake” (Hadithi za Kitabu cha Mormoni, 138-42, au video inayohusiana kwenye ChurchofJesusChrist.org). Waalike wasikilize Mormoni alikuwa na umri gani wakati Amaroni alipomkabidhi jukumu maalumu. Kisha waombe kunyanyua idadi hiyo ya vidole. Kuwasaidia watoto kupata taswira ya jinsi gani Mormoni alivyokuwa mdogo, waonyeshe picha ya mtu mwenye miaka 10. Wasaidie kuelewa sifa ambazo Amaroni aliziona kwa Mormoni wakati alipokuwa mdogo, na shuhudia kwamba watoto wanaweza kuwa kama Mormoni wakati wanapomfuata Yesu Kristo.

  • Chezeni mchezo ambapo watoto wanarudia matendo muhimu unayofanya. Kisha onyesha picha ya mambo ambayo Yesu alifanya, na zungumza kuhusu jinsi tunavyoweza Kumfuata Yeye (ona Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 33–35, 41–42). Jadili jinsi ambavyo Mormoni alimfuata Yesu Kristo—kwa mfano, kwa kufundisha injili, kuwahimiza watu kumtii Mungu, na kuwapenda wengine.

Mormoni 3:3, 9

Baba wa Mbinguni hunipa baraka nyingi.

Mafundisho ya Mormoni yanaweza kuwasaidia watoto kutambua baraka ambazo Baba wa Mbinguni amewapatia.

Shughuli za Yakini

  • soma Mormoni 3:3 na 9 kwa watoto, na elezea kwamba Wanefi hawakuwa wametambua kwamba Baba wa Mbinguni alikuwa amewabariki. Wasaidie watoto kufikiria baraka ambazo Baba wa Mbinguni amewapatia. Onyesha picha au vitu kuwapa mawazo. Nini tunaweza kufanya leo kuonyesha tuna shukrani kwa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya baraka zetu?

  • Wasaidie watoto kufikiria baraka Baba wa Mbinguni alizowapatia, na waombe wachore picha za baadhi ya baraka hizi. Waalike kutundika picha zao mahali fulani nyumbani ambapo wanaweza kuziona na kukumbuka kwamba Baba wa Mbinguni anawabariki katika njia nyingi. Ungeweza pia kuwaalika kutambua baraka ambazo huja kutoka kwa Baba wa Mbinguni wakati wakiimba aya ya kwanza ya “I Thank Thee, Dear Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 7).

Mormoni 3:12

Baba wa Mbinguni ananitaka kumpenda kila mtu.

Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kuwa na hamu ya kuhisi upendo kwa wale walio karibu nao?

Shughuli za Yakini

  • Muombe kila mtoto achore mtu ubaoni, na onyesha jinsi kila mtu waliyemchora ana muonekano tofauti na wengine. Chora moyo mkubwa kuzunguka michoro yote. Wasaidie watoto kuelewa kwamba Baba wa Mbinguni anataka tuwapende watu wote. Soma Mormoni 3:12, ukisisitiza maneno “upendo” na “niliwapenda.” Je, ni nini Mormoni alifanya kuonyesha upendo wake kwa wengine?

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu kuwapenda wengine, kama vile “Jesus Said Love Everyone“ (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 61), wakati ukionyesha picha za watoto kutoka ulimwenguni kote. Shuhudia juu ya upendo wa Mungu kwa watoto Wake wote. Malizia ukurasa wa shughuli ya wiki hii pamoja na watoto.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mormoni 1:1–3; 2:1, 23–24; 3:1–3, 12, 17–22

Ninaweza kuwa mwenye haki kama Mormoni.

Mormoni alikuwa mdogo wakati Amaroni alipotambua kwamba angeweza kuwajibika vya kutosha kutunza kumbukumbu takatifu. Ni sifa zipi za haki unaziona kwa watoto unaowafundisha?

Shughuli za Yakini

  • Mwalike kila mtoto kusoma moja ya vifungu vya maneno vifuatavyo, na wasaidie kushiriki kile wanachojifunza kuhusu Mormoni: Mormoni 1:1–3; 2:1, 23–24; na 3:1–3, 12, 20–22. Kisha shiriki sifa za haki unazoziona kwa kila mtoto.

  • Onyesha picha ya Mormoni (ona picha kwenye muhtasari wa wiki hii katika Njoo Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia). Wasaidie watoto kuona kwamba kwa sababu Mormoni alikuwa mwenye kuwajibika na mwaminifu vya kutosha kuandika na kuhifadhi kumbukumbu ya Wanefi, tuna Kitabu cha Mormoni leo. Zungumza na watoto kuhusu kile inachomaanisha kuwa mwenye kuwajibika na mwaminifu. Waalike watafakari jinsi wanavyoweza kuwa zaidi wenye kuwajibika.

    Picha
    Mormoni akiwa mvulana mdogo

    Mormoni, Miaka 10, na ScottM. Snow

Mormoni 2:8–15; 5:10–11

Huzuni kwa jinsi ya mungu huongoza kwenye badiliko halisi.

Mormoni aliona kwamba Wanefi waovu walikuwa na huzuni, lakini huzuni yao haikuwa aina ile ambayo ingewasukuma kutubu (ona Mormoni 2:13). Unawezaje kuwasaidia watoto kuelewa tofauti kati ya huzuni kwa jinsi ya ulimwengu na huzuni kwa jinsi ya mungu ambayo huongoza kwenye toba?

Shughuli za Yakini

  • Andika vichwa vya habari vifuatavyo ubaoni: huzuni inayoongoza kwenye toba na huzuni ambayo haiongozi kwenye toba. Waalike watoto wafanye zamu kusoma mistari kutoka Mormoni 2:8, 10–15. Wasaidie kuandika mambo wanayojifunza kuhusu huzuni chini ya kichwa cha habari sahihi ubaoni. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuhakikisha kwamba huzuni tunayohisi kwa ajili ya dhambi zetu hutuongoza kwenye kubadilika?

  • Mwalike mshiriki wa uaskofu au mzazi wa mmoja wa watoto kushiriki na darasa jinsi huzuni kwa jinsi ya Mungu inavyoweza kutusaidia kubadilika kuwa zaidi kama Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Kwa nini ni muhimu kutambua ikiwa tunahisi huzuni kwa jinsi ya mungu au huzuni kwa jinsi ya ulimwengu? Waalike watoto kutafuta Mormoni 2:12 ili kupata sababu kwa nini toba inapaswa kuifanya “mioyo yetu … iwe na furaha” (Mormoni 2:12).

Mormoni 3:12

Ninaweza kuhisi upendo wa Baba wa Mbinguni kwa wengine.

Mara nyingi ni rahisi kuwapenda wale wanaotupenda na walio kama sisi, lakini Mormoni alionyesha kwa mfano kwamba kwa msaada wa Baba wa Mbinguni, tunaweza kuwapenda wale wanaoamini na kutenda tofauti na sisi.

Shughuli za Yakini

  • Msaidie mtoto asome Mormoni 3:12, na waalike watoto kuandika sentensi moja ambayo inatoa ufupisho wa kile wanachojifunza kutoka kwa Mormoni kuhusu kuwapenda wengine. Waalike watoto kushiriki kile walichoandika. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuhisi upendo ambao Mungu anao kwa wengine? (ona Moroni 7:48). Je, tunaweza kufanya nini kuonyesha upendo wetu kwa watu katika darasa letu na katika familia zetu?

  • Waalike watoto kukamilisha ukurasa wa shughuli ya wiki hii. Wasaidie kufikiria njia zenye maana za kuwafikia kwa upendo wale wanaoweza kuwa tofauti na sisi.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wahimize watoto kuweka ukurasa wa shughuli ya wiki hii mahali fulani nyumbani ili kwamba waweze kukumbushwa kuonyesha upendo kwa wengine. Wapatie nafasi katika darasa lijalo kushiriki kile walichofanya.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Badilisha shughuli ili kukidhi umri wa watoto unaowafundisha. Watoto wadogo wanahitaji maelezo ya kina na hujifunza kutokana na mbinu rahisi za kufundishia. Wanapopevuka, watoto wanaweza kuchangia zaidi na kuwa bora katika kushiriki mawazo yao. Wape watoto wote kulingana na umri wao fursa za kushiriki, kushuhudia, na toa msaada kadiri inavyohitajika. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 25–26.)

Chapisha