Njoo, Unifuate
Oktoba 26–Novemba 1. Mormoni 1–6: “Ningetaka Kwamba Ningeshawishi Kila Mtu … Atubu”


“Oktoba 26–Novemba 1. Mormoni 1–6: Ningetaka Kwamba Ningeshawishi Kila Mtu … Atubu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Oktoba 26–Novemba 1. Mormoni 1–6,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2020

Picha
Mormoni akiandika kwenye bamba za dhahabu

Mormon Akifupisha Maandishi ya Mabamba, na Tom Lovell

Oktoba 26–Novemba 1

Mormoni 1–6

“Ningetaka Kwamba Ningeshawishi Kila Mtu … Atubu”

Unaposoma Mormoni 1–6, tafakari kile ambacho unaweza kujifunza kutokana na mfano wa Mormoni. Andika kile unachohisi umetiwa msukumo kufanya.

Andika Misukumo Yako

Mormoni alitunza kwa ajili yetu “maelezo kamili” ya “mandhari ya kutisha ” ya uovu na umwagaji damu ambao aliona miongoni mwa Wanefi (Mormoni 2:18; 5:8). Lakini kile alichoandika katika Mormoni 1–6 ni cha kutosha kutukumbusha ni kiasi gani watu wenye haki wanaweza kuanguka. Katika uovu uliokithiri kiasi hiki, hakuna anayeweza kumlaumu Mormoni kwa kuchoka na hata kufa moyo. Ilhali kupitia yote ambayo aliona na kupitia, hakupoteza ufahamu wake wa rehema kuu ya Mungu na msimamo wake kwamba toba ndiyo njia ya kuipokea. Na ingawa watu wa Mormoni wenyewe walikataa mialiko yake ya kuwasihi kutubu, alijua kwamba alikuwa na wasikilizaji wengi wa kushawishi. “Tazama,” alitangaza, “Nawaandikia wote wanaoishi ulimwenguni.” Kwa maneno mengine, alikuandikia wewe (ona Mormoni 3:17–20). Na ujumbe wake kwako, leo hii, ni ujumbe sawa na ule ambao ungewaokoa Wanefi katika siku zao: “Amini injili ya Yesu Kristo. … Atubu na ajitayarishe kusimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo” (Mormoni 3:21–22).

Picha
ikoni ya kujifunza kibinafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kibinafsi

Mormoni 1

Naweza kuishi kwa haki licha ya uovu unaonizunguka.

Ukianzia na sura ya kwanza ya Mormoni, utagundua tofauti kubwa kati ya Mormoni na watu wanaomzunguka. Unaposoma Mormoni1, fikiria kulinganisha sifa na tamaa za Mormoni na zile za watu wake. Angalia matokeo yaliyomjia yeye na wao (utapata mfano mmoja katika mistari 14–15). Unajifunza nini kinachokutia msukumo kuishi kwa haki katika ulimwengu wenye uovu?

Unaposoma Mormoni 2–6, endelea kutafuta jinsi Mormoni alivyoonyesha imani yake katika Baba ya Mbinguni na Yesu Kristo licha ya ushawishi muovu uliomzunguka.

Picha
Wanefi na Walamani wakipigana

Vita, na Jorge Cocco

Mormoni 2:10–15

Huzuni kwa jinsi ya Mungu inaelekeza kwenye badiliko la kweli na la kudumu.

Wakati Mormoni alipoona huzuni ya watu wake, alitumaini wangetubu. Lakini “huzuni yao haikuwa ya toba” (Mormoni 2:13)—haikuwa huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu inayoelekeza kwenye badiliko la kweli (ona 2 Wakorintho 7:8–11). Badala yake, Wanefi walihisi huzuni ya kiulimwengu (ona Mormoni 2:10–11). Ili kuelewa tofauti kati ya huzuni kwa jinsi ya Mungu na huzuni ya kiulimwengu, fikiria kutengeneza jedwali ambalo unaweza kuandika kile unachojifunza kutoka Mormoni 2:10–15 kuhusu aina hizi mbili za huzuni. Jedwali lako laweza kufanana na kitu kama hiki:

Huzuni kwa jinsi ya Mungu

Huzuni ya kiulimwengu

Huzuni kwa jinsi ya Mungu

Njoo kwa Yesu (mstari wa 14)

Huzuni ya kiulimwengu

Laani Mungu (mstari wa 14)

Huzuni kwa jinsi ya Mungu

Huzuni ya kiulimwengu

Huzuni kwa jinsi ya Mungu

Huzuni ya kiulimwengu

Unapopiga taswira ya kile unachojifunza, fikiria jinsi kinavyoweza kushawishi juhudi zako za kushinda dhambi na kuwa zaidi kama Baba wa Mbinguni na Mwokozi.

Ona pia Dieter F. Uchtdorf, “Unaweza Kufanya Hivyo Sasa!Ensign au Liahona, Nov. 2013, 55–57.

Mormoni 3:3, 9

Ninapaswa siku zote kutambua mkono wa Mungu katika maisha yangu.

Mormoni aliandika udhaifu aliouona kwa Wanefi: walikosa kutambua njia ambazo Bwana alikuwa amewabariki. Rais Henry B. Eyring alitusihi “kutafuta njia za kutambua na kukumbuka ukarimu wa Mungu. … Sali na utafakari, ukiuliza maswali: Je, Mungu alituma ujumbe ambao ulikuwa kwa ajili yangu? Je, niliuona mkono Wake katika maisha yangu au maisha ya watoto wangu? … Ninashuhudia ya kwamba anatupenda na anatubariki, zaidi ya vile wengi wetu bado hatujatambua ” (“Ee Kumbuka, Kumbuka,” Ensign au Liahona, Nov. 2007, 67, 69).

Unaposoma Mormoni 3:3, 9, unaweza kutafakari jinsi unavyotambua ushawishi wa Mungu katika maisha yako. Ni baraka zipi huja wakati unatambua ushawishi Wake? Ni nini matokeo ya kukosa kumtambua Yeye? (ona Mormoni 2:26).

Mormoni 5:8–24; 6:16–22

Yesu Kristo anasimama na mikono iliyonyooka kunipokea.

Wanefi walikataa mafunzo ya Mormoni, lakini alikuwa na tumaini kwamba kumbukumbu yake ingekushawishi wewe. Unaposoma Mormoni 5:8–24 na 6:16–22, unajifunza nini kuhusu matokeo ya dhambi? Unajifunza nini kutokana na vifungu hivi kuhusu hisia za Baba wa Mbinguni na Yesu kwako wewe, hata wakati unapotenda dhambi? Ni kwa jinsi gani umehisi Yesu Kristo akikukujia na mikono iliyonyooka? Je, unahisi msukumo wa kufanya nini kama matokeo yake?

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mawazo.

Mormoni 1:2

Inamaanisha nini kuwa “mwepesi kwa kuchunguza”? Unaweza kupata umaizi katika hotuba ya Mzee David A. Bednar “Mwepesi wa Kuchunguza” (Ensign, Des. 2006, 30–36). Ni kwa jinsi gani kipawa cha kuwa mwepesi chunguza kilikuwa baraka kwa Mormoni? Kinawezaje kuwa baraka kwetu?

Mormoni 1:1–6, 15; 2:1–2

Je, watoto katika familia yako wanaelewa kwamba wanaweza kukuza sifa kuu na uwezo wa kiroho hata ingawa wao ni wadogo? Mfano wa Mormoni unaweza kuwasaidia. Fikiria kutengeneza ratiba ya wakati wa utotoni na ujana wa Mormoni, ukitumia umri na matukio yaliyotolewa katika Mormoni 1:1–6, 15 na 2:1–2. Unapojadili sifa na uzoefu wa Mormoni, zungumzia sifa ambazo watoto wako wanazo ambazo zinakutia msukumo pamoja na wengine wanao wazunguka.

Mormoni 2:18–19

Ni maneno gani Mormoni alitumia kuelezea ulimwengu alimoishi? Ni namna gani alidumisha tumaini licha ya uovu ulimzunguka? Ni jinsi gani familia yetu inaweza kufanya sawa na hivyo?

Mormoni 3:12

Je, Mormoni alihisi vipi kuhusu watu walikuwa karibu naye, hata kama walikuwa waovu? Je, tunaweza kufanya nini ili kukuza upendo kama aliokuwa nao?

Mormoni 5:2

Je, ni kwa nini tuwaweza kusita kumwita Baba wa Mbinguni wakati tunapokuwa kwenye mapambano? Je, tunaweza kufanya nini ili kumtegemea Baba wa Mbinguni zaidi?

Mormoni 5:16–18

Kuisaidia familia yako kupata taswira ya maana ya “kupeperushwa kama makapi mbele ya kimbunga” (mstari wa 16), chana kipande cha karatasi katika vipande vidogo na uwaruhusu wanafamilia wavipulize kuzunguka kote. Waelezee kwamba makapi ni maganda yanayotoka kwenye mbegu, na ni mepesi vya kutosha kupeperushwa. Ni jinsi gani kuwa “bila Kristo na Mungu katika ulimwengu” (mstari wa 16) ni kuwa kama vumbi litimuliwalo mbele ya kimbunga.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fundisha kwa uwazi na mafundisho rahisi. Injili ya Bwana ni nzuri kwa urahisi wake (ona MM 133:57). Kuliko kujaribu kuwafurahisha familia yako kwa masomo yanayohitaji maandalizi mengi, hakikisha kwamba kile unachofundisha ni kitovu cha mafundisho halisi na rahisi.

Picha
Mormoni akitazama uwanja wa vita vya Wanefi na Walamani

Kitabu cha Miujiza cha Mormoni, na Joseph Brickey

Chapisha