Njoo, Unifuate
Oktoba 28–Novemba 3. 1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni: ‘Uwe Kielelezo kwao Waaminio’


“Oktoba 28–Novemba 3. 1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni: ‘Uwe Kielelezo kwao Waaminio’” Njoo, unifuate—kwa msingi:Agano Jipya 2019 (2019)

“Octoba 28–Novemba 3. 1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2019

Picha
Wanawake watatu wamesimama nje ya hekalu

Oktoba 28–Novemba 3

1 na 2 Timotheo; Tito; Filemoni

“Uwe Kielelezo kwao Waaminio”

Kwa maombi jifunze 1 na 2 Timotheo; Tito; na Filemoni ili kujifunza jinsi unavyoweza kutumia nyaraka hizi kufundisha watoto katika haki (ona 2 Timotheo 3:16).

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waombe watoto kuzungumza kuhusu mtu fulani ambaye ni “kielelezo cha waaminio” kwao. Wao wanafanya nini ili kuwa mifano mizuri kwa wengine”?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wadogo

1 Timotheo 3:1–2; Tito 1:7–9

Maaskofu wanaongoza kata kama watumishi wa Mungu.

Paulo alimfundisha Timotheo na Tito kuhusu umuhimu wa maaskofu. Unawezaje kuwafundisha watoto askofu anafanya nini? (Rais wa tawi analinganishwa na askofu.)

Shughuli Yamkini

  • Chora picha ya kawaida ya askofu wako ubaoni. Waombe watoto wataje baadhi ya vitu wananvyojua kuhusu askofu. Je, yeye yukoje? Je, anafanya nini? Je, anabariki vipi kata? Unaweza kupata baadhi ya sifa za askofu katika 1 Timotheo 3:1–2 na Tito 1:7–9.) Wakati watoto wanashiriki mawazo yao, yaandike kwenye vipande za karatasi na waache watoto waviweke kwenye ubao karibu na mchoro.

    Picha
    Askofu katika ofisi yake akizungumza na kijana

    Maaskofu wanaitwa kutoa mwongozo wa kiroho kwa waumini wa kata.

  • Andika kazi za askofu kwenye vipande vya karatasi—kama vile kupokea zaka na matoleo ya mfungo, kutoa miito, kusaili waumini, kuwasaidia masikini na wenye shida, na kuwaombea wengine. Weka vipande hivi katika bakuli, na mtake kila mtoto achukue kimoja. Kisha msaidie mtoto kuiga kazi hizi pamoja nawe. Shiriki ushuhuda wako kwamba askofu wako ameitwa na Mungu.

  • Waombe watoto kuchora picha ya askofu akihudumia waumini wa kata. Pendekeza kwamba watoe michoro yao kwake kama kumshukuru. Tunaweza kufanya nini ili kumsaidia?

1  Timotheo 4:12.

Ninaweza kuwa “kielelezo kwao Waaminio.”

Unaweza kufanya nini ili kuwavutia watoto kujiamini katika uwezo wao kuwa “ vielelezo kwao waaminio”?

Shughuli Yamkini

  • Imba pamoja na watoto “Do as I’m Doing.” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 276). Waombe watoto kufuata mfano wako kwa kufanya vitendo unavyofanya. Acha watoto wachukue zamu kuongoza darasa zima katika kufuata matendo yao. Soma 1 Timotheo 4:12, na waulize watoto nini wanaweza kufanya kuwa mifano mizuri kwa wengine.

  • Shiriki uzoefu wakati ulipojaribu kuwa mfano mzuri kwa mtu fulani au wakati mtu fulani alikuwa mfano mzuri kwako. Wasaidie watoto kuelewa kwamba wakati wanapokuwa mifano mizuri, wanaweza kuwasaidia wanafamilia zao na marafiki.

2 Timotheo 3:14–17

Maandiko yatanisaidia kujifunza ukweli.

Kama unaweza kuwasaidia watoto kujifunza kupenda maandiko, utabariki maisha yao kwa miaka ijayo.

Shughuli Yamkini

  • Onyesha seti ya maandiko, na wasaidie watoto kuwa na mazoea nayo kwa kuwaonesha majina ya kurasa za Biblia, Kitabu cha Mormoni, Mafundisho na Maagano, na Lulu ya Thamani Kuu. Mwalike mtoto avishike vitabu hivi unaposoma 2 Timotheo 3:15–17. Eleza kwamba Baba wa Mbinguni amewaamuru manabii katika historia yote kuandika ukweli ambao anaufunua kwao. Tunaweza kujifunza ukweli huu tunaposoma maandiko.

  • Waombe watoto wazungumzie kuhusu mali yao yenye thamani kubwa. Wanaifanyia nini? Acha watoto wachukue zamu kuyashika maandiko na kwa uangalifu kugeuza kurasa. Tunatumia maandiko kwa ajili ya nini? Kwa nini tuyatunze kwa uangalifu ? Wasaidie watoto kufanya matendo yanayoendana na nyimbo kuhusu maandiko, kama vile “Search, Ponder, and Pray” au ‘Book of Mormon Stories” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 109 118).

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wakubwa

1  Timotheo 4:12.

Ninaweza kuwa “kielelezo kwao Waaminio.”

Timotheo alikuwa kiasi mdogo kwa ajili ya kuwa kiongozi wa Kanisa, lakini Paulo alimtaka ajue kwamba bado anaweza kuwa kielelezo. Unaweza kuwasaidia watoto unaowafundisha kujiamini katika uwezo wao wa kuweka mfano mzuri.

Shughuli Yamkini

  • Someni pamoja 1 Timotheo 4:12, na waombe watoto kutafuta njia sita Paulo alisema tunaweza kuwa “kielelezo kwa waaminio.” Wagawanye watoto katika majozi, na omba kila kundi kufikiria hali ambayo wanaweza kuwa mfano wa waaminio. Waombe waigize hali yao kwa ajili ya darasa zima.

  • Waulize watoto kama watapenda kushiriki uzoefu wowote wakati walipojaribu kuwa mfano mzuri kwa wengine. Waeleze jinsi wamekuwa mifano ya waaminio kwako na jinsi ulivyowaona wakiweka mifano mizuri kwa wengine.

1 Timotheo 6:7–12

Ninapaswa kupenda mambo ya milele zaidi kuliko pesa.

Katika ulimwengu ambao unaokuwa wa anasa zaidi na zaidi, utawezaje kuwasaidia watoto kuweka lengo lao na upendo uliolenga juu ya Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wazungumze kuhusu wangenunua nini kama wangekuwa na pesa zote za ulimwenguni. Mwalike mtoto asome 1 Timotheo 6:7–12, na waombe watoto wengine kufanya muhtasari wa nini Paulo alimfundisha Timotheo kuhusu pesa. Kisha waalike watoto kusoma mistari hii tena, wakitafuta vitu ambavyo Paulo alivitaja kama vina thamani zaidi kuliko pesa.

  • Panga picha za vitu vya ulimwengu (kama vile pesa, mwanasesere, au burudani) na vitu vya milele (kama vile familia au mahekalu). Waalike watoto wachambue picha kwenye mafungu mawili—vitu ambavyo vinatuleta karibu zaidi na Kristo na vitu ambavyo vinaweza kutuvuta kutoka kwa Kristo kama tutavipenda zaidi kuliko tunavyompenda Yeye. Kwa nini “kupenda pesa … chanzo cha uovu wote”?

2 Timotheo 3:14–17

Baba wa Mbinguni alitupa maandiko ili kutusaidia kujua ukweli na makosa.

Watoto wanaweza kupata uzoefu wa baraka za kusoma maandiko. Unawapofundisha watoto kuhusu maandiko, tafuta njia za kuwatia moyo kuwa na uzoefu wao wenye nguvu wa neno la Mungu.

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kusoma 2 Timotheo 3:15—17. Lete picha zinazoonesha hadithi kutoka kila moja ya vitabu vitakatifu, na weka hizo picha katika sanduku lililofunikwa. Waalike watoto kadhaa kuchukua picha hizo na kusimulia hadithi. Waombe watoto kama wanaweza kushiriki kitu kingine kuhusu kitabu kile cha maandiko. Je, ni kwa jinsi gani maandiko” yanaweza kutufanya [sisi] tuwe na hekima hata kupata wokovu?

  • Waalike watoto kushiriki aya ya maandiko wanayoipenda au tukio wakati ukweli katika maandiko ulipowasaidia. Unaweza kutaka kushiriki aya yako binafsi au uzoefu wako.

  • Muombe mtoto asome Moroni 10:4–5. Moroni aliahidi nini katika aya hizi? Waulize watoto nini walichofanya ili kupata ushuhuda kwamba maandiko ni ya kweli. Waalike kusoma au kusikiliza maandiko kila siku.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki na familia zao kile walichojifunza kuhusu maandiko na kutafuta aya moja ya maandiko ambayo wanaweza kushiriki na darasa wiki ijayo (na msaada kutoka kwa wazazi wao, kama unahitajika).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tohoa shughuli kutosheleza mahitaji. Badala ya kuichukulia mihutasari hii kama maelekezo ambayo ni lazima uyafuate, itumie kama chanzo cha mawazo kuanzisha mwongozo wako wa kiungu unapotafakari mahitaji ya watoto unaowafundisha. Unaweza kutohoa shughuli ili kuwafundisha watoto wa umri wowote.

Chapisha