Agano Jipya 2023
Aprili 17–23. Mathayo 18; Luka 10: “Nifanye Nini ili Kurithi Uzima wa Milele?’”


Aprili 17–23. Mathayo 18; Luke 10: ‘Nifanye Nini Ili Kurithi Uzima wa Milele?,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2023 (2022)

Aprili 17–23. Mathayo 18; Luka 10 “ Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2023

Picha
Msamaria mwema

Msamaria mwema, na Dan Burr

Aprili 17–23

Mathayo 18; Luka 10

“Nifanye Nini Ili Kurithi Uzima wa Milele?”

Kweli gani katika Mathayo 18 na Luka 10 watoto wanahitaji kujifunza? Sikiliza misukumo kutoka kwa Roho Mtakatifu unaposoma sura hizi. Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia inaweza kusaidia kuelekeza kujifunza kwako kwa sura hizi, na muhtasari huu unaweza kukupa mawazo ya kufundishia.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waombe watoto washiriki kitu walichojifunza kuhusu Yesu Kristo nyumbani au katika Msingi.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Mathayo 18:21–35

Daima ninapaswa kuwasamehe wengine.

Unaposoma Mathayo 18:21–35, zingatia uzoefu wako mwenyewe katika kutoa msamaha na kile ambacho watoto wanahitaji kujua kuhusiana na kanuni hii.

Shughuli Yamkini

  • Simulia hadithi ya mtumishi asiye na huruma (ona Mathayo 18:23–35). Elezea kwamba wakati mtu amekuwa sio mkarimu au anatenda jambo lisilo zuri kwetu, yawezekana tukasikia hasira au huzuni mwanzoni. Lakini msamaha unamaanisha tunaweza kuhisi amani tena. Tunapomsamehe mtu, tunaamua kutokumkasirikia tena. (Wasaidie watoto kuelewa kwamba kama mtu fulani anakuwa sio mkarimu kwao au anawatendea sivyo, wanapaswa kuwaambia wazazi wao au kuomba msaada kwa mtu mwingine mzima anayeaminiwa.)

  • Andika nimekusamehe ubaoni, na waambie watoto kwamba maneno haya yanaweza kuwasaidia kugeuza nyakati za huzuni kuwa za furaha. Chora sura yenye huzuni ubaoni, na shiriki baadhi ya mifano ya watoto wakisameheana. Baada ya kila mfano, mwalike mtoto kubadilisha sura yenye huzuni kuwa yenye furaha.

  • Imba pamoja na watoto wimbo kuhusu msamaha, kama vile “Help Me, Dear Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99). Toa ushuhuda wako kwamba Baba wa Mbinguni atatusaidia kuwasamehe wengine.

Luka 10:25–37

Yesu alinifundisha kuwaona watu wote kama majirani zangu na kuwapenda.

Fumbo la msamaria mwema linaweza kuwaonyesha watoto majirani zetu ni akina nani na tunapaswa kuwatendea vipi. Fikiria juu ya njia unazoweza kuwashawishi watoto “kwenda, na kufanya … vivyo hivyo” (Luka 10:37).

Shughuli Yamkini

  • Muulize kila mtoto, “Jirani yako ni nani?” Fupisha hadithi hii katika Luka 10:25–37, na simulia jinsi Yesu alivyojibu hilo swali. Yesu alifundisha nini kuhusu jinsi tunavyopaswa kuwatendea majirani zetu?

  • Soma Luka 10:25–37 watoto wanapoigiza fumbo la Msamaria mwema. Wasaidie kufikiria juu ya njia ambazo wao wanaweza kuwa kama Msamaria mwema kwa kuonyesha upendo na ukarimu kwa wengine.

  • Andika mifano michache ya hali ambazo mtu fulani angehitaji msaada, na ficha karatasi hizo humo chumbani. Waombe watoto watafute karatasi hizo. Soma hali hizo, na waalike watoto kuelezea jinsi gani wao wangeweza kuonyesha ukarimu kwa mtu aliye katika hali hiyo.

  • Imba na watoto wimbo unaohusu ukarimu, kama vile “Jesus Said Love Everyone” au “Kindness Begins with Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 61, 145). Wasaidie watoto wafikirie njia chache wanazoonyesha upendo na ukarimu kwa wengine. Wangeweza pia kuchora picha zao wenyewe wakifanya mambo haya.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Mathayo 18:21–35

Baba wa Mbinguni atanisamehe ninapowasamehe wengine.

Fumbo la mtumishi asiye na huruma linaweza kuwa njia ya kukumbukwa kuwafundisha watoto kwamba Baba wa Mbinguni anatutaka tumsamehe kila mmoja.

Shughuli Yamkini

  • Soma Mathayo 18:23–35 pamoja na watoto. Eleza kwamba mfalme au bwana inawakilisha Baba wa Mbinguni, mtumishi inatuwakilisha sisi, na mtumishi mwenzetu anawakilisha wale wanaotukosea. Waulize watoto maswali kama “Je, hadithi hii inatufundisha nini kuhusu jinsi tunavyopaswa kuwatendea wengine? Je, ni lini ulijisikia vigumu kumsamehe mtu? Je, uliachiaje hizo hisia zenye uchungu? Je, ni lini wewe ulihitaji kusamehewa kwa uchaguzi mbaya uliofanya?

  • Onyesha video ya “Forgive Every One Their Trespasses: The Parable of the Unmerciful Servant” (ChurchofJesusChrist.org) ili kuwasaidia watoto kuvuta taswira ya fumbo hili.

  • Andika katika ubao hesabu ya kuzidisha 70 x 7, na wasaidie watoto kuitatua. Muombe mmoja asome Mathayo 18:21–22, na eleza kwamba Yesu alitumia hesabu hii ili kutufundisha kwamba daima tunapaswa kusamehe.

  • Waombe watoto kukusaidia ufikirie hali chache ambapo mtu atahitaji kumsamehe mtu mwingine. Waalike watoto kuigiza jinsi ambavyo wangeweza kuonyesha msamaha katika hali hizo.

  • Imba pamoja na watoto wimbo kuhusu msamaha, kama vile “Help Me, Dear Father” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 99). Wasaidie watoto kuelewa wimbo huu unafundisha nini kuhusu kuwasamehe wengine.

Luka 10:30–37

Ninaweza kuwapenda na kuwatumikia wengine, hususani wale wenye shida.

Tafakari nyakati katika maisha yako mwenyewe ambapo mtu fulani alikuwa “Msamaria mwema” kwako. Unawezaje kuwashawishi watoto kuwa “Wasamaria wema” kwa wengine?

Shughuli Yamkini

  • Mpangie kila mtoto kusoma kimya kimya sehemu ya fumbo la Msamaria mwema. Waalike watoto kusimulia sehemu zao za fumbo katika mpangilio sahihi wa matukio yalivyotokea.

  • Eleza kwa watoto kwamba Wayahudi hakuwapenda Wasamaria kabisa kiasi kwamba walisafiri kutoka Yerusalemu hadi Galilaya, walikuwa wakipita kuzunguka nje ya Samaria ili kuepuka kuingiliana na Msamaria ye yote. Ili kufafanua hili, onyesha ramani ya 1 ya Biblia, “Ramani ya Nchi Takatifu.” Kwa nini Yesu Alimtumia Msamaria kama mfano wa ukarimu katika fumbo? Hii hadithi inatufundisha nini kuhusu kuwasaidia wengine wenye shida? (Ona pia Mosia 4:16–22.)

  • Waombe watoto kushiriki uzoefu ambapo mtu fulani alikuwa kama Msamaria mwema kwao.

  • Wape changamoto watoto kuweka lengo la kuwa kama Msamaria mwema wiki hii. Kwa mfano, je, wanamfahamu mtu fulani ambaye ni mgonjwa au mpweke au mtu fulani ambaye hahudhurii kanisani kila mara? Waulize watoto ni jinsi gani wanaweza kumsaidia mtu huyo. Wasaidie watoto kuelewa jinsi gani kuwatumikia wengine kunawasaidia wao kushika ahadi walizofanya wakati walipobatizwa (ona Mosia 18:8–10).

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki pamoja na familia kile wanachopanga kufanya ili kuwa wenye kusamehe zaidi au kuwa kama yule Msamaria mwema wiki hii.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wafundishe watoto kuandika misukumo wanayopata. Kama watoto watajifunza tabia ya kuandika misukumo yao, itawasaidia kumtambua na kumfuata Roho Mtakatifu. Watoto wanaweza kuandika misukumo yao kwa kuwekea alama maandiko, kuchora picha, au kuweka kumbukumbu rahisi katika shajara zao.

Chapisha