Agano Jipya 2023
Septemba 11–17 2 Wakorintho 1–7: “Na Mpatanishwe na Mungu”


“Septemba 11–17. 2 Wakorintho 1–7:”Na Mpatanishwe na Mungu’”. Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2023 (2022)

“Septemba 11–17. 2 Wakorintho 1–7” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2023

Picha
Yesu Kristo

Septemba 11–17

2 Wakorintho 1–7

“Na Mpatanishwe na Mungu”

Anza maandalizi yako kwa kusoma 2 Wakorintho 1–7. Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia inaweza kukusaidia kuelewa hizi sura, na huu muhtasari unaweza kukupa mawazo ya kufundishia.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Baadhi ya watoto katika darasa lako yawezekana kuwa wameandika barua wiki hii kuhusu jinsi mwanafamilia alivyo mfano mzuri wa mfuasi wa Yesu Kristo (ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia). Kama walifanya hivyo, waombe kabla ya muda kushiriki barua darasani. Au waombe watoto washiriki jambo lingine walilojifunza.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

2 Wakorintho 1:3–4

Baba wa Mbinguni ananifariji, na mimi naweza kuwafariji wengine.

Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuwapa watoto kujiamini kwamba Baba wa Mbinguni atawafariji? Je, ni kwa jinsi gani unaweza kuwatia moyo kuwafariji wengine?

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto baadhi ya vitu ambavyo vinatoa faraja, kama vile blanketi au bendeji. Waulize watoto nini kinawafariji wakati wana huzuni au hofu au wana matatizo mengine. Soma 2 Wakorintho 1:3–4 pamoja na watoto, na eleza kwamba “dhiki” ni neno lingine kwa ajili ya matatizo magumu. Elezea baadhi ya njia ambazo Baba wa Mbinguni amekufariji wewe, na shuhudia kwamba atawafariji watoto vile vile.

  • Onyesha picha za watu wakiwa wanabatizwa (ona Kitabu Cha Sanaa za Injili, na.103–4) unaposoma 2 Wakorintho 1:4 kwa watoto. Eleza kwamba tunapobatizwa, tunaahidi kuwafariji wengine. Je, ni kwa jinsi gani sisi tunaweza kufuata ushauri wa Paulo wa “kuwafariji walio katika dhiki yo yote” ?

2 Wakorintho 2:7–8, 10

Mimi Naweza Kuwasamehe Wengine.

Chagua kutoka shughuli zifuatazo—au lete yako mwenyewe—ili kusaidia kuimarisha matamanio ya watoto ya kuwasamehe wengine.

Shughuli Yamkini

  • Waelezee watoto kwamba Paulo alitaka Watakatifu wa Korintho kumsamehe mtu aliyefanya dhambi. Soma 2 Wakorintho 2:7–8, 10, na waalike watoto kuweka mikono yao juu ya mioyo yao kila wakati wanaposikia maneno samehe na alisamehe.

  • Waalike watoto waigize jinsi watakavyoitika katika hali ya mtu akifanya jambo la kikatili. Acha watoto wachukue zamu kusema “Samahani” na “Ninakusamehe.” Tunawasaidiaje watu kujua kwamba tunawasamehe? Eleza kwamba njia moja inaweza kuwa “kuthibitisha upendo wako,” au kuonyesha upendo kwao (2 Wakorintho 2:8).

2 Wakorintho 4:1–2

Ninaamini katika kuwa mwaminifu.

Paulo alifundisha kwamba watumishi wa Kristo “wamekataa vitu vilivyojificha vya kutokuwa waaminifu.” Tafakari jinsi unavyoweza kuimarisha hamu za watoto za kutaka kuwa waaminifu katika mambo yote.

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kukariri kirai “Tunaamini katika kuwa waaminifu” (Makala ya Imani 1:13). Andika kirai hiki kwenye bangili za karatasi watoto wanaweza kuziremba na kuzivaa. Elezea kwamba kuwa mwaminifu inajumuisha kusema ukweli.

  • Waombe watoto wainue mikono yao unaposema kitu ambacho ni cha kweli na waishushe unaposema kitu ambacho sio cha kweli. Toa kauli rahisi lakini ya dhahiri, kama vile “Leo ni Jumapili” au “Nina pua tatu.” Rudia shughuli hii mara kadhaa, ukiwaacha watoto wachukue zamu kuwa yule anayefanya kauli za kweli na za uongo. Je, ni kwa nini Baba wa Mbinguni anatutaka sisi kusema ukweli?

  • Onyesha video ya “A Visit with Elder Ulisses Soares” (ChurchofJesusChrist.org). Kijana Mzee Soares alijifunza nini kuhusu uaminifu? Wahimize watoto kujianda kwa ajili ya agano la ubatizo wao kwa kuwa waaminifu.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

2 Wakorintho 1:3–4

Baba wa Mbinguni hunifariji, na mimi naweza kuwafariji wengine.

Kukumbuka jinsi Mungu alivyotufariji sisi kunaweza kuwavutia watoto kutoa faraja kwa wengine.

Shughuli Yamkini

  • Unaposoma 2 Wakorintho 1;3–4, waombe watoto kusikiliza jibu la swali “Mungu anafanya nini kwa ajili yetu sisi?” Wasaidie watoto kuorodhesha njia ambazo Mungu anatufariji. Waalike watoto washiriki uzoefu wakati walipokuwa wamehuzunika au kuwa na wasiwasi au na hofu na Mungu akawafariji.

  • Waalike watoto kushiriki njia tunazoweza kushika agano la ubatizo wetu la kuwafariji wengine (ona Mosia 18:9). Wape muda wa kumfikiria mtu wanayemjua anayehitaji faraja na kufanya mpango wa kumfikia mtu huyo.

2 Wakorintho 2:5–11

Mimi ninaweza kuwasamehe wengine.

Inaweza kuwa vigumu kuwasamehe wengine wakati wao ni wakatili kwetu. Lakini watoto unaowafundisha watapata uzoefu wa upendo, amani, na furaha wanapojifunza kusamehe.

Shughuli Yamkini

  • Waambie watoto kwamba mtu fulani huko Korintho alikuwa amefanya dhambi na “alisababisha huzuni” kwa Watakatifu (ona 2 Wakorintho 2:5). Waombe watoto kupekua 2 Wakoritho 2:7–8 na watafute kile ambacho Paulo aliwataka Watakatifu wafanye.

  • Shiriki uzoefu ambapo wewe ulimsamehe mtu —au mtu fulani alipokusamehe wewe—na jinsi ulivyohisi baadaye. Au onyesha video ya “The Goal: A Story of Faith, Friendship and Forgiveness” (ChurchofJesusChrist.org). Waalike watoto kushiriki uzoefu wao juu ya msamaha.

2 Wakorintho 5:6–7

“Ninatembea kwa imani, sio kwa kuona.”

Fikiria jinsi unavyoweza kuwatia moyo watoto kutii amri za Mungu hata wasipoona baraka wanazotamani mara moja.

Shughuli Yamkini

  • Soma 2 Wakorimtho 5:6–7 na Alma 32:21 pamoja na watoto, na uwaombe watafute maneno na virai ambavyo vinasaidia kueleza imani ni nini. Waombe waandike maelezo yao na kushiriki mmoja na mwingine.

  • Mwalike mmoja wa watoto kufumba macho, na waombe watoto wengine kutoa maelekezo ya kumsaidia kukamilisha kazi kama vile kujenga mnara kwa matofali, au kutembea humo chumbani. Ni kwa jinsi gani shughuli hii inatusaidia kuelewa kile inamaanisha “kutembea kwa imani” katika Mungu?

  • Onyesha video “Reunited by faith” (ChurchofJesusChrist.org), na wauliza watoto jinsi gani msichana katika video alitembea kwa imani. Shiriki uzoefu ambapo wewe ulitembea kwa imani, na uwatie moyo watoto kuelezea uzoefu wao.

2 Wakorintho 7:8–10

Huzuni ya kimungu huniongoza kutubu.

Ni kawaida kuona haya au aibu wakati tunaposhikwa tukifanya kitu kisicho sahihi. Wasaidie watoto kutofautisha hisia hizi na huzuni ya kimungu, ambayo huongoza kwenye toba ya kweli.

Shughuli Yamkini

  • Eleza kwamba katika 2 Wakorintho 7:8–10, Paulo alirejelea barua aliyoiandika mwanzoni kwa Watakatifu, kwa ujasiri akiwaonya kuhusu dhambi zao. Someni mistari hii pamoja. Kwa nini Paulo alifurahi kwamba Watakatifu walikuwa na huzuni? Toa angalizo kwamba aina hii ya huzuni inaitwa huzuni ya kimungu.

  • Waombe watoto kufikiri kuhusu wakati walipofanya kitu kisicho sahihi na wakajisikia vibaya kuhusu kitu hicho. Waalike kujiuliza wenyewe, “Kwa nini nilijisikia vibaya?” na kisha washiriki majibu yao. Andika majibu yao ubaoni (kwa mfano, “niliogopa ningeingia katika matatizo” au “nilijua nilimhuzunisha Baba wa Mbinguni” au “nilimfanya mtu alie”). Lipi kati ya majibu ubaoni linaonekana kama ni “huzuni ya kimungu”? (2 Wakorintho 7:10). Kwa nini huzuni ya kimungu ni bora kuliko aina zingine za huzuni tunazoweza kuhisi baada ya kufanya kitu kisicho sahihi?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kushiriki na familia zao mojawapo ya shughuli ya kutoka katika darasa la leo, labda wakati wa jioni ya familia nyumbani.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Onyesha andiko. Chagua mstari wa maandiko ambao unaona ukiwa na maana na uutundike katika darasa lako ambapo watoto watauona mara kwa mara. Pengine watoto wangeweza kupeana zamu kuchagua andiko la kutundikwa.

Chapisha