Agano Jipya 2023
Mpangilio wa Kufundisha


“Mpangilio wa Kufundisha,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2023 (2023)

“Mpangilio wa Kufundisha,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2023

Picha
mwalimu wa Msingi na mtoto

Mpangilio wa Kufundisha

Katika nyenzo hii, utapata mpangilio ufuatao wenye hatua tatu zinazojirudia katika kila muhtasari: alika kushiriki, fundisha mafundisho, na himiza kujifunza nyumbani. Mara nyingi, unapofundisha, vipengele vya mpangilio huu vinaweza kuingiliana au kutokea kwa utaratibu tofauti. Kwa mfano, fikiria kwamba kushiriki na wengine ni fursa ya kufundisha mafundisho, na kufundisha mafundisho kunapaswa kuhusishe mialiko ya kushiriki. Vivyo hivyo, kuhimiza kujifunza nyumbani kunaweza kutokea katika mjadala mzima wa darasa. Ruhusu marekebisho katika mpangilio huu yatokee kiuhalisia, ukifuata ushawishi wa Roho ili kukidhi mahitaji ya watoto unaowafundisha.

Alika Kushiriki

Kama sehemu ya kila darasa, waalike watoto kushiriki hisia zao, umaizi, na uzoefu wao juu ya kanuni unazofundisha. Maoni yao yanaweza kujumuisha uzoefu ambao wamepata walipojifunza nyumbani. Unaweza pia kurejelea kile walichojifunza wiki iliyopita na kuwauliza jinsi kilivyogusa maisha yao.

Fundisha Mafundisho

Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia inaweza kukusaidia kuelewa vizuri zaidi mafundisho ambayo utawafundisha watoto. Fikiria ni mistari gani ya maandiko, dondoo, uzoefu, maswali, na nyenzo zingine ambazo unaweza kuzitumia ili kuwasaidia watoto kuelewa na kutenda juu ya kanuni za injili wanazojifunza. Wasaidie kutambua ushawishi wa Roho Mtakatifu wakati Yeye anaposhududia juu ya ukweli. Tafuta njia za ubunifu na zenye mwongozo wa kiungu ili kuwasaidia wawe na msisimko juu ya kile wanachojifunza.

Kwa mawazo kuhusu jinsi ya kutumia muziki kufundisha mafundisho, angalia sehemu za “Kutumia Muziki ili Kufundisha Mafundisho” na “Kuwasaidia Watoto Kujifunza na Kukumbuka Nyimbo za Msingi pamoja na Nyimbo za Kanisa” katika kiambatisho cha kitabu hiki cha kiada.

Himiza Kujifunza Nyumbani

Kwa sababu nyumbani ni kitovu cha kujifunza injili, mojawapo ya malengo yako kama mwalimu wa Msingi ni kuhimiza kujifunza nyumbani. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia watoto kushiriki na familia zao kile walichojifunza darasani? Ni kwa jinsi gani unaweza kuwahimiza watoto na wazazi wao kuendelea kujifunza kutoka katika Agano Jipya huko nyumbani?

Chapisha