Njoo, Unifuate
Januari 6–12. 1 Nefi 1–7: “Nitaenda na Kutenda”


“Januari 6–12. 1 Nefi 1–7: ‘Nitaenda na Kutenda,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Januari 6–12. 1 Nefi 1–7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2020

Picha
Familia ya Lehi ikisafiri jangwani

Lehi Akisafiri Karibu na Bahari ya Shamu, na Gary Smith

Januari 6–12

1 Nefi 1–7

“Nitaenda na Kutenda”

Maandalizi yako kama mwalimu wa Shule ya Jumapili yanaanza na kujifunza kwako binafsi maandiko. Zingatia na andika misukumo ya kiroho unayopokea . Nnjoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia inaweza kuongezea kwenye kujifunza kwako.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Wengi wa washiriki wa darasa lako yawezekana wanafahamu 1 Nefi 1–7, lakini kila wakati tunaposoma maandiko, tunaweza kujifunza kweli ambazo zinahusika kwenye hali zetu za sasa. Kwa kuanza majadiliano yako, pengine ungeweza kuwauliza washiriki wa darasa kile walichojifunza au walichokumbushwa walipojifunza wiki hii.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

1 Nefi 1; 3–6

Maandiko ni ya thamani kubwa.

  • Ujumbe mmoja mashuhuri katika Kitabu cha Mormoni ni thamani kubwa ya neno la Mungu. Huu unaweza kuwa ujumbe mzuri kushiriki wakati darasa lako linapoanza kujifunza Kitabu cha Mormoni. Ungeweza kuanza kwa kumuomba kila mshiriki wa darasa kuchagua sura kutoka 1 Nefi 1; 3–6 na kuichunguza, akitafuta njia ambazo neno la Mungu moja kwa moja au zisizo za moja kwa moja lilibariki wanafamilia wa Lehi. (Washiriki wa darasa wanaweza kunufaika kwa kufanya shughuli hii katika makundi madogo.) Kisha waalike washiriki binafsi kushiriki kile wanachopata. Maelezo haya yanatufundisha nini kuhusu umuhimu wa maandiko?

  • Moja ya malengo yako kama mwalimu ni kuwatia moyo watu binafsi na familia kujifunza injili nje ya darasa. Labda ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kuchunguza jinsi Lehi alivyochunguza bamba za shaba (ona 1 Nefi 5:10–19), na kisha ungeweza kuuliza maswali kama yafuatayo: Nini ulikuwa mtazamo wa Lehi kuhusu maandiko? Alipata nini cha thamani ndani yake? Washiriki wa darasa wangeweza pia kuchunguza ujumbe wa Mzee Richard G. Scott “Nguvu ya Maandiko” (Ensign au Liahona, Nov. 2011, 6–8) au kusoma dondoo kutoka kwenye ujumbe huu katika “Nyenzo za Ziada.” Tunawezaje kutumia mafundisho ya Mzee Scott tunapojifunza Kitabu cha Mormoni mwaka huu?

  • Kama darasa, mngeweza kuimba wimbo kuhusu maandiko, kama vile “As I Search the Holy Scriptures” (Nyimbo za Kanisa, na. 277). Kisha ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki jinsi gani usomaji wao binafsi wa maandiko umebariki maisha yao. Wangeweza pia kushiriki jinsi maandiko yalivyowapa msukumo “kuja kwa … Mungu … na kuokolewa” (1 Nefi 6:4).

1 Nefi 2:11–19; 3:28–31

Tunaweza kupata shuhuda zetu wenyewe pale tunapolainisha mioyo yetu.

  • Nefi anajulikana kwa imani yake yenye nguvu katika Bwana, lakini inaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kutambua kwamba ilibidi afanye kazi ili kupata ushuhuda wake—kama vile sisi sote tunavyofanya. Labda washiriki wa darasa wangeweza kutambua katika 1 Nefi 2:16–19 kile kilichofanya iwezekane kwa Nefi kupata ushahidi wake. Wangeweza pia kurejea mistari 11–14 kuchunguza kwa nini Lamani na Lamueli hawakupata ushahidi. Huu unaweza kuwa wakati mzuri kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki jinsi walivyopata shuhuda zao.

  • Wakati mwingine tunaweza kutaka kuwa na uzoefu wa kimiujiza ili tuweze kupata au kuimarisha shuhuda zetu. Lakini Lamani na Lamueli walikutana na malaika, na bado imani yao ilionekana kuathirika kwa kiasi kidogo. Washiriki wa darasa wanaweza kujifunza nini kutokana na uzoefu huu, ulioelezwa katika 1 Nefi 3:28–31, kuhusu nini kinaimarisha shuhuda zetu? (Ona pia 1 Nefi 2:16). Fikiria kushiriki dondoo kutoka kwa Rais Harold B. Lee katika ”Nyenzo za Ziada.” Tunaweza kufanya nini ili kuweka shuhuda zetu imara?

1 Nefi 3–4

Mungu atatayarisha njia kwa ajili yetu kufanya mapenzi Yake.

  • Uzoefu wa wana wa Lehi katika 1 Nefi 3–4 unaweza kuonekana ni wa kipekee, lakini wengi wetu tumekuwa na uzoefu ambapo tulifuata mapenzi ya Mungu hata kama ilionekana ni vigumu. Wakati washiriki wa darasa wanaposoma 1 Nefi 3–4 wiki hii, ni kweli zipi walizozipata ambazo ziliwakumbusha juu ya uzoefu binafsi? Labda ungeweza kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki mistari ambayo ilifundisha kweli hizi, na waalike kushiriki uzoefu wao. Ni kwa jinsi gani kweli hizi zinatusaidia wakati tunategemewa na Mungu kufanya kitu ambacho kinaonekana kigumu?

  • Ungeweza kuligawanya darasa katika makundi matatu na kulipangia kila kundi kujifunza moja ya majaribio ya kupata bamba za shaba kutoka kwa Labani (ona 1 Nefi 3:9–21; 1 Nefi 3:22–31; 4:1–4; na 1 Nefi 4:5–38). Kisha ungeweza kualika kila kundi kushiriki kile ambacho kila moja ya majaribu haya hutufundisha kuhusu kutimiza mapenzi ya Bwana. Ni kwa jinsi gani mifano hii inahusika kwenye juhudi zetu wenyewe za kufanya mapenzi ya Mungu?

Picha
Lehi na Saria wakiwasalimia Nefi na kaka zake

Shangwe Yao Ilikuwa Imetimia, na Walter Rane

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Kuwatia moyo washiriki wa darasa kusoma 1 Nefi 8–10, ungeweza kushiriki maelezo haya kutoka kwa Rais Dieter F. Uchtdorf: “Kwa kani nyingi zinazojaribu kutuvuta mbali, ni kwa jinsi gani tunaendelea kuweka mtazamo wetu imara kwenye furaha tukufu iliyoahidiwa kwa waaminifu? Ninaamini jibu linaweza kupatikana kwenye ndoto ambayo nabii aliipata maelfu ya miaka iliyopita. Jina la nabii ni Lehi, na ndoto yake imeandikwa kwenye Kitabu cha thamani na cha kupendeza cha Mormoni” (“Akina Dada Watatu,” Ensign au Liahona, Nov. 2017, 18–19).

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Video za Kitabu cha Mormoni.

Tafuta video ambazo zinaonesha maelezo kutoka 1 Nefi 1–7 katika mkusanyiko wa Video za Kitabu cha Mormoni kwenye ChurchofJesusChrist.org au Gospel Library app.

Maandiko yana uwezo wenye nguvu.

Mzee Richard G. Scott alishuhudia juu ya thamani ya maandiko:

“Maandiko ni kama pakiti za nuru ambazo zinaangaza akili zetu na kutoa nafasi kwa mwongozo na uvuvio kutoka juu. Yanaweza kuwa ufunguo wa kufungua njia ya ushirika na Baba yetu wa Mbinguni na Mwanae Mpendwa, Yesu Kristo.

“Maandiko … yanaweza kuwa marafiki waaminifu ambao hawazuiliwi na jiografia au kalenda. Siku zote yanapatikana yanapohitajika. Matumizi yake yanatoa msingi wa ukweli ambao unaweza kuzinduliwa na Roho Mtakatifu. Kujifunza, kutafakari, kutafuta, na kukariri maandiko ni kama kujaza kabati la faili kwa marafiki, maadili, na kweli ambazo zinaweza kutumika wakati wowote, mahali popote duniani. …

“Kutafakari kifungu cha maandiko kunaweza kuwa ufunguo wa kufungua ufunuo na mwongozo na ushawishi wa Roho Mtakatifu. Maandiko yanaweza kutuliza roho iliyofadhaika, kutoa amani, tumaini, na urejesho wa kujiamini katika uwezo wa mtu wa kushinda changamoto za maisha. Yana uwezo wenye nguvu kuponya changamoto za kihisia wakati kuna imani katika Mwokozi. Yanaweza kuharakisha uponyaji wa kimwili” (“Nguvu ya Maandiko,” Ensign au Liahona, Nov. 2011, 6).

Shuhuda zetu lazima zifanywe upya kila siku.

Rais Harold B. Lee alifundisha, “Kile ambacho unacho leo katika ushuhuda hakitakuwa chako kesho isipokuwa kama utafanya kitu fulani kukihusu” (Mafundisho ya Marais wa Kanisa: Harold B. Lee [2000], 43).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tumia hadithi na mifano kufundisha kanuni za injili. Kweli nyingi za milele katika maandiko zinafundishwa kupitia uzoefu au hadithi zilizomo. Unapojiandaa kufundisha, fikiria uzoefu uliowahi kuwa nao ambao ungeweza kuongeza ushahidi wa pili kwenye maelezo katika maandiko na kanuni ambazo uzoefu huo unaelezea. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 22.)

Chapisha