Njoo, Unifuate
Februari 17–23. 2 Nefi 11–25: “Tunafurahi Katika Kristo”


“Februari 17–23. 2 Nefi 11–25: ‘Tunafurahi Katika Kristo,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Februari 17–23. 2 Nefi 11–25,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2020

Picha
Isaya akiandika kwenye hati za kukunja

Februari 17–23

2 Nefi 11–25

“Tunafurahi katika Kristo”

Kwa kuongezea kwenye kulinganisha 2 Nefi 11–25 kwako mwenyewe, fikiria jinsi unavyoweza kuwasaidia watu unaowafundisha kulinganisha sura hizi kwao wenyewe (ona 2 Nefi 11:8). Pale Roho anapokupa msukumo na mawazo, yaandike.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kabla ya kujadili vifungu maalumu vya maneno kutoka 2 Nefi 11–25, ingeweza kuwa yenye msaada kuwaomba washiriki wa darasa kufikiria kwamba wana rafiki anayejitahidi sana kutafuta chochote chenye maana au kuvutia katika maandiko ya Isaya. Ni mistari gani wangeshiriki na rafiki huyu?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

2 Nefi 11–24

Isaya alishuhudia juu ya Yesu Kristo.

  • Inaweza kuwa rahisi sana kuelewa unabii wa Isaya wakati tunapojua kwa nini uliandikwa. Kuanza majadiliano ya unabii wa Isaya katika 2 Nefi, ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kuchunguza Mlango wa 11 na kuorodhesha baadhi ya malengo ya Nefi ya kumnukuu Isaya kwa upana sana. Wangeweza pia kushiriki vifungu vya maneno walivyovipata katika kujifunza kwao binafsi au na familia kwa 2 Nefi 12–24 ambavyo wanahisi vilifanikisha malengo hayo. Ni kwa jinsi gani kuelewa malengo ya Nefi kuliwasaidia washiriki wa darasa kupata zaidi kutoka kwenye maandishi ya Isaya? Watie moyo kuweka malengo haya katika akili zao pale wanapojadili maandishi ya Isaya darasani.

  • Kwa sababu Isaya alitumia sana lugha ya ishara, inaweza kuwa rahisi kutotilia maanani ushahidi wake wenye nguvu wa Yesu Kristo. Hii hapa ni shughuli ambayo inaweza kusaidia darasa lako kulenga kwenye ushahidi huu. Ungeweza kutayarisha karatasi kadhaa zenye marejeleo ya maandiko yaliyoandikwa juu yake kutoka 2 Nefi 12–24 ambayo yanafundisha kuhusu Mwokozi (kwa mfano, 2 Nefi 13:13; 14:4–6; 15:1–7; 16:1–7; 17:14; 18:14–15; 19:6–7; 21:1–5; 22:2). Kila mshiriki wa darasa angeweza kuchagua mojawapo ya karatasi, kujifunza maandiko yaliyoandikwa juu yake, na kuandika juu ya karatasi kile alichojifunza kuhusu Yesu Kristo. Kisha washiriki wa darasa wangeweza kubadilishana karatasi na mtu mwingine na kuongeza mawazo mengine yoyote au utambuzi waliojifunza kuhusu Mwokozi kutoka kwenye mistari hiyohiyo. Kisha ungeweza kuwapa washiriki wa darasa nafasi ya kushiriki kile walichojifunza kutoka kwa Isaya na kutoka kwa kila mmoja wao ambacho kiliongeza shukrani zao kwa ajili ya Yesu Kristo.

  • Unabii katika 2 Nefi 19:6 unaorodhesha majina kadhaa ya Yesu Kristo. Fikiria kumuomba mtu fulani kuyaorodhesha ubaoni na waalike washiriki wa darasa kujadili kwa nini kila moja ya majina haya lina maelezo yanayostahili ya Mwokozi. Ni kwa jinsi gani ametimiza majukumu haya katika maisha yetu? Ili kujifunza zaidi kuhusu baadhi ya majina haya, ingeweza kuwa yenye msaada kuangalia marejeleo katika tanbihi ya 2 Nefi 19:6.

2 Nefi 12:2–5; 21:10–1222

Katika siku za mwisho, watu wa Mungu watakusanywa na kufurahia amani.

  • Sehemu fulani za unabii wa Isaya ni mahsusi hasa kwetu sisi kwa sababu unaelezea vipengele vya kazi ya Mungu ya siku za mwisho. Kwa mfano, mngeweza kuchunguza 2 Nefi 21:10–12, ambayo inaelezea “bendera” (beramu au bango) ambalo litainuliwa kukusanya watu wa Mungu. Ni kwa jinsi gani tumemwona Bwana akikusanya watu Wake kiroho? pengine baadhi ya washiriki wa darasa wangeweza kuzungumza kuhusu nini kinachowafanya kutaka kukusanyika au kujiunga na watu wa Mungu Kanisani. Wangeweza hata kufurahia kuunda mabango yao wenyewe ambayo yanaorodhesha au kuelezea baadhi ya kweli za injili ambazo wanahisi watu “wanazitafuta” na zitasaidia “kuleta pamoja “ na “kukusanya pamoja” (mstari wa 10 na 12) watoto wa Mungu katika siku yetu. Ni kwa jinsi gani tunasaidia katika kukusanyika?

  • Njia nyingine ya kujadili mafundisho haya ni kuandika dhamira zifuatazo ubaoni: Kutawanyika kwa Israeli, kukusanyika kwa Israeli, na Unabii wa Kristo. Ungeweza kupanga sura kutoka 2 Nefi 12–24 kwa makundi ya washiriki wa darasa na kuwaalika kutafuta mistari ambayo inafundisha kuhusu vitu hivi na andika mistari hii chini ya kichwa cha habari kinachofaa ubaoni. Sura hizi zina jumbe gani kwetu? Ingeweza kuwa yenye msaada kuwaambia washiriki wa darasa kwamba Mafundisho na Maagano 113:1–6 inaweza kuwasaidia kuelewa 2 Nefi 21:1–5, 10.)

  • Nyimbo za Kanisa kama vile “High on the Mountain Top” (Nyimbo za Kanisa, na. 5) au “The Lord is My Light” (Nyimbo za Kanisa, na. 89), ambazo zina msingi juu ya sehemu ya unabii katika 2 Nefi 12:2–5 na 2 Nefi 22, zinaweza kuimarisha jumbe na roho ya maneno ya Isaya.

2 Nefi 14:4–6

Nyumba zetu na “mikusanyiko” ya Sayuni vinaweza kuwa sehemu za usalama na kimbilio.

  • Katika 2 Nefi 14:4–6 Isaya alitoa unabii kuhusu usalama na amani ambayo wenye haki watafurahia baada ya Bwana “kuosha kabisa” na “kutakasa” dhambi zao. Ingawa mistari hii inaelezea hali ambazo zitakuwepo katika Milenia, ingeweza kuwasaidia washiriki wa darasa pale wanapotafuta usalama wa kiroho katikati ya uovu wa siku za mwisho. Waalike kutafakari na kujadili kile inachomaanisha kuwa na “wingu na moshi” na “miale ya moto” kwenye “makao yao” na “mikusanyiko” (mstari wa 5; ona pia kutoka 13:21–22). Nini baadhi ya vitu ambavyo vinaweza kufananishwa na joto, tufani, na mvua vilivyotajwa katika mstari wa 6? Ni kwa jinsi gani tunaweza kupata usalama? (Ona pia M&M 115:6). Pengine washiriki wa darasa wangeweza kupendekeza njia za kuhakikisha mikusanyiko ya nyumbani mwetu na Kanisani ni sehemu za ulinzi wa kiroho.

2 Nefi 25:19–29

“Njia sahihi ni kuamini katika Kristo”

  • Washiriki wako wa darasa wanaweza pia kuwa na hamu kama ya Nefi ya “kushawishi watoto wetu, na pia ndugu zetu, kuamini katika Kristo.” Ni kwa jinsi gani Nefi “alifanya kazi kwa bidii” kufanikisha lengo hili? (2 Nefi 25:23). pengine washiriki wa darasa wangeweza kutafuta 2 Nefi 25:19–29 kupata kweli kuhusu Mwokozi na injili Yake ambazo Nefi alitaka watu wake wazijue. Kisha wangeshiriki kile walichokifanya kufundisha kweli hizi kwa familia zao au marafiki. Kwa mfano, ni kwa jinsi gani wamefundisha ukweli kwamba “ni kwa neema kwamba tunaokolewa, baada ya kutenda yote tunayoweza”? (Maelezo kutoka kwa Rais Dieter F. Uchtdorf katika “Nyenzo za Ziada” yanaweza kutoa baadhi ya utambuzi kwenye ukweli huu.) Ni kwa jinsi gani wamewasaidia wengine “kufurahi katika Kristo”?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Washiriki wa darasa wangeweza kuvutiwa kujua kwamba 2 Nefi 26–30 inaweza kuwasaidia kutoa jibu kwa watu wanaosema, “Hatuhitaji Kitabu cha Mormoni.”

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

“Kwa ajili yetu mtoto amezaliwa.”

Kuongozea kwenye majadiliano yako ya 2 Nefi 19:6, tazama au sikiliza kwaya ya Tabernacle wakiwa Temple Square wakiimba “For unto Us a Child Is Born” (ChurchofJesusChrist.org).

“Ni kwa neema kwamba tunaokolewa, baada ya kutenda yote tunayoweza.”

Akitoa maoni kwenye maneno ya Nefi katika 2 Nefi 25:23, Rais Dieter F. Uchtdorf alisema:

“Ninashangazwa kama wakati mwingine tunatoa tafsiri isiyo sahihi ya neno ‘baada ya yote tunayoweza kufanya.’ Ni lazima tuelewe kwamba ‘baada’ sio sawa na ‘kwa sababu.’

“Hatuokolewi ‘kwa sababu’ ya yote yale ambayo tunaweza kufanya. Kuna yeyote kati yetu amefanya yote ambayo tunaweza kufanya? Je, Mungu anasubiri mpaka tuwe tumetumia juhudi zote kabla hajaingilia katika maisha yetu kwa neema yake ya kuokoa? …

“Nina hakika Nefi alijua kwamba neema ya Mwokozi inaruhusu na inatuwezesha kushinda dhambi [ona 2 Nefi 4:19–35; Alma 34:31]. Hii ndiyo sababu Nefi alifanya kazi kwa bidii sana kuwashawishi watoto wake na ndugu zake ‘kuamini katika Kristo, na kupatanishwa na Mungu.’ [2 Nefi 25:23].

“Hata hivyo, hicho ndicho kile tunachoweza kufanya! Na hiyo ndiyo kazi yetu katika maisha ya duniani!” (“Kipawa cha Neema,” Ensign au Liahona, Mei 2015, 110 ).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Uliza maswali ambayo yanaalika ushuhuda. “Kuuliza maswali ambayo yanahimiza wanafunzi kushiriki ushuhuda kuhusu kanuni ambazo zinafundishwa inaweza kuwa njia yenye nguvu ya kumwalika Roho. … Shuhuda zao—na shuhuda za wengine darasani—zitakua wakati Roho anapotoa ushahidi wa ukweli” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 32).

Chapisha