Njoo, Unifuate
Januari 27–Februari 2. 1 Nefi 16–22: “Nitawatayarishia Njia”


“Januari 27–Februari 2. 1 Nefi 16–22: ‘Nitawatayarishia Njia,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020.)

“Januari 27–Februari 2. 1 Nefi 16–22” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2020

Picha
Lehi akiangalia Liahona

Lehi na Liahona , na Joseph Brickey

Januari 27–Februari 2

1 Nefi 16–22

“Nitawatayarishia Njia”

Unaposoma 1 Nefi 16–22, fikiria kuhusu jinsi mfano wa Nefi wa kukabiliana na changamoto unaweza kuwa wenye msaada kwa watu wa darasa lako.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni kushiriki

Alika Kushiriki

Nefi aliona thamani ya kufananisha maandiko na yeye mwenyewe na watu wake (ona 1 Nefi 19–23). Fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki kanuni walizojifunza kutoka maelezo ya safari ya Nefi kwenda nchi ya ahadi ambayo inasimulia maisha yao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

1 Nefi 16:10–16, 23–31; 18:10–13, 20–22

Mungu anatumia njia ndogo kukamilisha vitu vikubwa.

  • Unaweza, au mtu fulani katika darasa lako, kufikiria kitu kidogo ambacho kinaweza kutumika kusababisha kitu fulani kikubwa? (ona 1 Nefi 16:29). Unaweza kuwataka washiriki wa darasa kujadili nini wanachojifunza kuhusu kanuni hii baada ya kusoma maandiko haya kibinafsi au katika vikundi: 1 Nefi 16:25–31; Alma 37:3–8; na Mafundisho na Maagano 64:33; 123:12–17. Jinsi gani Mungu ametumia njia ndogo kukamilisha vitu vikubwa katika maisha yetu?

  • Darasa lako linaweza kunufaika kutokana na kujadiliana jinsi Baba wa Mbinguni anavyoelekeza njia zetu. Kwa kuanza, unaweza kulitaka darasa kujadili kanuni ambazo zilifanya Liahona kufanya kazi (ona 1 Nefi 16:10–16, 23–31; 18:10–13, 20–22; ona pia Alma 37:38–47). Jinsi gani kanuni hizi zinaweza kufikiriwa “njia ndogo”? Washiriki wa darasa wanaweza kuorodhesha ubaoni vitu ambavyo Mungu amevitoa kutuongoza (ona “Nyenzo za Ziada” kwa mawazo). Ni vitendo gani vidogo tunavyoweza kufanya kupata mwongozo wa Mungu?

Picha
Lehi akitumia Liahona

Kama Mmejitayarisha Hamtaogopa, na Clark Kelley Price

1 Nefi 4:18–32; 17:7–16; 18:1–4

Tunapotii sheria, Mungu atatusaidia kukabiliana na changamoto.

  • Washiriki wa darasa lako wanaweza kuwa wanakabiliana na kazi na changamoto ambazo zinaonekana haziwezekani. Unawezaje kutumia uzoefu wa Nefi pamoja na kazi zake zinazoonekana haziwezikani—kuilisha familia yake nyikani na kujenga meli—kuwasaidia? Labda washiriki wa darasa wanaweza kusoma 1 Nefi 16:18–32; 17:7–16; na 18:1–4, kutafuta kanuni ambazo zinaweza kuwasaidia wakati wanapokabiliana na changamoto ya shida (kwa mfano, 1 Nefi 16:24–26 inafundisha kwamba sala na unyenyekevu vinaturuhusu kupokea msukumo na mwelekeo kutoka kwa Mungu). Unaweza kuanza kwa kuwapa mfano wa kanuni uliyoipata katika mistari hii. Wanaposhiriki kile walichopata, wanaweza pia kushiriki uzoefu binafsi unaofanana.

1 Nefi 16:18–32,; 17:7–22

Imani inaongoza kwenye matendo.

  • Uzoefu wa Lehi na familia yake nyikani unaonesha nguvu ya imani na matokeo ya kutoamini. Kuwasaidia washiriki wa darasa kugundua kweli hizi, unaweza kuandika maswali haya ubaoni: Nefi aliifanyia nini imani yake? Alibarikiwa vipi kama matokeo yake? Nini yalikuwa matokeo ya kutoamini kwa Lamani na Lemueli? Waalike washiriki wa darasa kama vikundi kutafuta majibu kwa maswali haya katika 1 Nefi 16:18–32 au 17:7–22 na shiriki kile wanachopata.

1 Nephi 19:22–24

Tunaweza kulinganisha maandiko nasi.

  • Kuwasaidia washiriki wa darasa kujifunza jinsi ya kulinganisha maandiko nao wenyewe, wanaweza kusoma mifano ya jinsi Nefi alivyofanya. Kwa mfano, katika 1 Nefi 4:1–3 na 17:23–32, 41–45, ni kanuni gani Nefi alizofundisha kwa kulinganisha maandiko na hali ya familia yake? Kauli ya Mzee Robert D. Hales katika “Nyenzo za Ziada” inaonesha jinsi gani kulinganisha maandiko nasi kunaweza kutubariki. Fikiria kuwataka washiriki wa darasa kutambua changamoto zinazowakabili au familia zao na kisha kupata kauli za kimaandiko ambazo zinaweza kuwapa utambuzi na msaada kwa hali hizo. Kulingana na 1 Nefi 19:22–24, jinsi gani kulinganisha maandiko nasi kunaweza kutubariki?

  • Kujadiliana 1 Nefi 19:22–24 kunaweza kuwa nafasi kubwa kwa washiriki wa darasa kushiriki jinsi “wanavyolinganisha maandiko” kwa wao wenyewe na famila zao, vilevile baraka walizopokea kwa kufanya hivyo. Fikiria kuorodhesha ubaoni mawazo ya washiriki wa darasa kuhusu jinsi ya kulinganisha maandiko na wao wenyewe (kwa baadhi ya mapendekezo, ona orodha katika “Nyenzo za Ziada”). Katika darasa linalofuata, unaweza kutaka washiriki wa darasa kushiriki uzoefu wakati walipotumia mawazo kwenye orodha.

1 Nefi 20–21

Bwana ataikusanya nyumba ya Israeli katika siku za mwisho.

  • Kuwatia moyo washiriki wa darasa kushiriki mafundisho ya maana waliyoyapata katika 1 Nefi 20–21, fikiria kuandika vichwa vya habari kama hivi ubaoni: Watoto wa Israeli, Familia ya Lehi, na Watu katika siku zetu. Wape muda warejee 1 Nefi 20–21 na orodhesha chini ya kila kichwa cha habari jinsi unabii wa Isaya unavyohusika na vikundi hivi.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Kuwatia moyo washiriki wa darasa kusoma 2 Nefi 1–5, watake wafikiri kuhusu nini watakachosema kwa famila zao kama muda wao duniani ni mfupi. Onesha kwamba sura chache za kwanza za 2 Nefi zina ujumbe wa mwisho Lehi alioutoa kwa familia yake.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Video za Kitabu cha Mormoni

Tafuta video ambazo zinaonesha matokeo kutoka 1 Nefi 16–22 katika lundo la video za Kitabu cha Mormoni kwenye ChurchofJesusChrist.org au Gospel Library app.

“Liahona” Zetu.

Mzee David A. Bednar alifundisha: “Roho Mtakatifu hufanya kazi katika maisha yetu kwa njia sawa na jinsi Liahona ilivyofanya kwa Lehi na familia yake, kulingana na imani yetu na bidii na kufuata” (“That We May Always Have His Spirit to Be with Us,” Ensign au Liahona, Mei 2006, 31).

Katika mkutano mkuu wa Oktoba 2005, Mzee Lowell M. Snow wa Sabini alisema: “Mkutano huu mkuu bila shaka ni Liahona ya kisasa, muda na sehemu ya kupokea mwongozo wa kutia moyo na mwelekeo ambao unatustawisha” (“Compass of the Lord,” Ensign au Liahona, Nov. 2005, 97).

Rais Thomas S. Monson alifundisha: “Bwana yule yule aliyetoa Liahona kwa ajili ya Lehi anatoa kwa ajili yako na kwa ajili yangu leo zawadi adimu na ya thamani kutoa mwelekeo kwa maisha yetu. … Zawadi ambayo ninaitaja inajulikana kama baraka yako ya baba mkuu”( Thomas S. Monson,” (“Your Patriarchal Blessing: A Liahona of Light,” Ensign, Nov. 1986, 65).

Kuyalinganisha maandiko na sisi wenyewe.

Mzee Robert  D. Hales alifundisha:

“Miaka michache iliyopita nilikuwa ninamfundisha kijana wetu mdogo kuhusu maisha na uzoefu wa kaka yake Yaredi. Ingawa hadithi ilikuwa ya kuvutia sana, hakuwa amevutiwa. Kisha nilimuuliza hadithi ilikuwa na maana gani kwake binafsi. Ina maana kwa kiasi fulani wakati tunapowauliza watoto wetu, ‘Ina maana gani kwako?’ Alisema, ‘Unajua, sio tofauti kiasi hicho kutoka kile Joseph Smith alifanya katika kijisitu aliposali na kupata jibu,’

“Nilisema, ‘Upo karibu na umri wa Joseph. Je, unafikiria sala kama hii inaweza kuwa yenye msaada kwako?’ Ghafla, hatukuwa tunazungumza kuhusu hadithi ya muda mrefu uliopita katika nchi ya mbali. Tulikuwa tunazungumza kuhusu kijana wetu—kuhusu maisha yake, mahitaji yake, na njia sala inaweza kumsaidia.

“Kama wazazi, tuna jukumu la kuwasaidia watoto wetu ‘kulinganisha maandiko [hasa, kila sehemu ya injili ya Yesu Kristo] nasi [na kwa watoto wetu], …kwa ajili [ya] faida na kujifunza [kwa familia zetu]’” (With All the Feeling of a Tender Parent: A Message of Hope to families.” Ensign or Liahona, Mei 2004, 90).

Mapendekezo kwa ajili ya kulinganisha maandiko.

  • Fikiria kuhusu matukio au hali katika siku zetu ambazo zinafanana na hizo katika maandiko unayosoma.

  • Tafuta kile watu wanachokijua, jifunze, au fanya katika maandiko kile kinachoweza kukusaidia na tatizo lako binafsi la sasa au swali.

  • Tambua kanuni kutoka hadithi ile ambazo zinaweza kukusaidia katika hali yako mwenyewe.

Chapisha