Njoo, Unifuate
Machi 9–15. Yakobo 1–4: “Patanishweni na Mungu kupitia Upatanisho wa Kristo”


“Machi 9–15. Yakobo 1–4: ‘Patanishweni na Mungu kupitia Upatanisho wa Kristo,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Machi 9–15. Yakobo 1–4,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2020

Picha
Mwanamke akipiga magoti miguuni pa Yesu

Kusamehewa, na Greg K. Olsen

Machi 9–15

Yakobo 1–4

Patanishweni na Mungu kupitia Upatanisho wa Kristo

Yakobo 1–4 ina mafundisho mengi ambayo yanatumika kwenye siku yetu. Unaposoma milango hii, fikiria jinsi unavyoweza kuwasaidia wale unaowafundisha kuishi mafundisho aliyofundisha Yakobo.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kuwasaidia washiriki wa darasa kushiriki umaizi kutoka Yakobo 1–4, ungeweza kugawa vipande vya karatasi na kuwaalika washiriki wa darasa kuandika marejeleo ya maandiko kutoka kwenye milango hii ambayo wanaona yana maana. Weka vipande katika chombo, toa vichache, na waalike watu walioandika marejeleo kushiriki umaizi wao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Yakobo 1:6–8, 15–19; 2:1–11; 4:18

Viongozi wenye haki hufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya ustawi wa nafsi.

  • Ungeweza kuanza majadiliano kuhusu kazi za bidii za Yakobo miongoni mwa watu wake kwa kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki uzoefu wakati walipobarikiwa na huduma ya kiongozi wa Kanisa. Au fikiria kumuomba kiongozi wa Kanisa—wa zamani au aliyepo sasa—kuzungumza kuhusu wakati walipohisi kuvutiwa kumhudumia mtu fulani. Washiriki wa darasa kisha wangeweza kutafuta maneno na vifungu vya maneno katika Yakobo 1:6–8, 15–19; 2:1–11; na 4:18 ambavyo hutusaidia kuelewa jinsi Yakobo alivyohisi kuhusu wito wake na watu aliowahudumia. Ni kwa jinsi gani tumeona viongozi wetu wakitukuza miito yao? Mistari hii inapendekeza nini kuhusu jinsi tunavyotakiwa kuwaunga mkono viongozi wetu?

Picha
watu wawili wakishikana mikono juu ya meza

Kama Yakobo, viongozi wa Kanisa leo “wanatukuza ofisi [zao] kwa Bwana.”

Yakobo 2:12–21

Tunapaswa kuepuka kiburi na kuwafikia wale wenye mahitaji.

  • Bwana alikuwa na maonyo yenye nguvu kwa Wanefi kuhusu kiburi. Kusaidia kuanza majadiliano kwenye mada hii, ungeweza kuwasiliana na washiriki wachache wa darasa mapema na kuwaomba kutafuta jinsi adui anavyokuza kupenda utajiri katika ulimwengu wetu leo. Kisha waalike kushiriki pamoja na darasa kile walichogundua. Washiriki wa darasa wangeweza kufanya kazi katika jozi kusoma Yakobo 2:12–21 na kupata kile Bwana alichofundisha kuhusu jinsi tunavyopaswa kuwa na mtazamo wa utajiri wa vitu. Kisha wangeweza kutengeneza na kushiriki bango ambalo linatangaza kanuni hiyo. Toa muda kwa washiriki wa darasa kutafakari kibinafsi nini wanaweza kufanya kutumia kile wanachojifunza kutoka kwenye ujumbe wa Yakobo.

  • Washiriki wa darasa lako wangeweza kurejea Yakobo 2:12–21 na kuandika maswali yao wenyewe kuongezea kwenye orodha ya Mzee Perry. Ni nini maelezo ya Mzee Perry katika “Nyenzo za Ziada” kinaongeza kwenye uelewa wetu wa mafundisho ya Yakobo?

Yakobo 2:23–35

Bwana hufurahia usafi wa kimwili.

  • Mzee David A. Bednar alifundisha kwamba tunaishi “katika ulimwengu ambao umekithiri kejeli za utakatifu wa uzazi na kupunguza thamani ya maisha ya binadamu” (“Tunaamini Katika Kuwa Wasafi,” Ensign au Liahona, Mei 2013, 41–44). Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kutumia Yakobo 2:23–35 kukinza jumbe za ulimwengu kuhusu usafi wa kimwili? Njia mojawapo inaweza kuwa kuandika ubaoni Ni kwa jinsi gani Bwana anahisi kuhusu usafi wa kimwili? na waalike washiriki wa darasa kutafuta majibu kwa swali hili. Baadhi yao wangeweza kuchunguza Yakobo 2:23–35, na wengine wangeweza kuchunguza hotuba ya Mzee Bednar iliyorejelewa hapo juu. Wangeweza kuorodhesha ubaoni majibu wanayopata. Kujadili viwango na baraka zinazohusishwa na kuishi sheria ya Usafi wa Kimwili, ungeweza kurejea “Usafi wa Kijinsia” (Kwa Nguvu ya Vijana, 35–37) au onesha mojawapo ya video zilizoorodheshwa katika “Nyenzo za Ziada.” Kuna baraka gani za kuishi maisha ya usafi wa kimwili?

Yakobo 4:4–11

Wanefi waliamini katika Yesu Kristo.

  • Yakobo alitaka sisi tujue kwamba hata kama yeye na watu wake waliishi mamia ya miaka kabla ya huduma ya Mwokozi duniani, walijua kuhusu Yeye na walimtazama Yeye kwa ajili ya wokovu. Kulingana na Yakobo 4:4–5, kwa nini Wanefi walitii sheria ya Musa? Ni nini tulichonacho katika siku yetu ambacho kinaelekeza nafsi zetu kwa Mwokozi? Ni alama zipi au mifano ambayo Yakobo alitumia kufundisha kuhusu Yesu Kristo? (Ona pia Mwanzo 22:1–13).

Yakobo 4:8–18

Ninaweza kuepuka upofu wa kiroho kwa kufokasi kwa Mwokozi.

  • Je, kuna yeyote darasani kwako amefanya uchunguzi wa macho hivi karibuni? Kama ndivyo, ungeweza kumuomba mtu huyu kuelezea jinsi daktari alivyochunguza uwezo wake wa kuona. Washiriki wa darasa wangeweza kushiriki kile wanachofikiri inamaanisha kuwa kipofu kiroho. Ni kwa jinsi gani upofu wa kiroho unafanana na upofu wa kimwili? Waalike washiriki wa darasa kupendekeza njia tunazoweza kuchunguza kama sisi ni vipofu wa kiroho. Wangeweza pia kurejea Yakobo 4:8–18 na kupendekeza baadhi ya vitu tunavyoweza kufanya kuongeza uwezo wetu wa “kuona” vitu vya kiroho.

  • Mzee Quentin L. Cook alitoa muhtasari wa njia nne watu wangeweza kuangalia “zaidi ya lengo” katika siku yetu (ona “Nyenzo za Ziada”). Maneno yake yanaongeza nini kwenye uelewa wetu wa Yakobo 4:13–15? Inamaanisha nini kuangalia zaidi ya lengo? Tunawezaje kuepuka kuangalia zaidi ya lengo?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Kuwavutia washiriki wa darasa kusoma Yakobo 5–7, waambie kwamba watapata jibu kwa swali hili katika Yakobo 4:17 watakaposoma kwa sala sura tatu zinazofuata.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Mtazamo wetu juu ya utajiri wa vitu

Kuhusu Yakobo 2:13–19, Mzee L. Tom Perry alifundisha: “Tunapaswa kupeleka ushauri wa Yakobo moyoni. Tunapaswa kusoma andiko hili kama vile lilikuwa limeandikwa hasa kwa ajili yetu katika siku hizi, kwa sababu ndivyo ilivyo. Maneno yake yanapaswa kutusababisha sisi kujiuliza maswali ya kuchunguza nafsi. Je, utaratibu wa mambo ni sahihi katika maisha yetu wenyewe? Je, tunawekeza, kwanza kabisa, katika vitu ambavyo ni vya milele kiasili? Je tuna mtazamo wa milele? Au tumeangukia kwenye mtego wa kuwekeza katika vitu vya ulimwengu huu kwanza na kisha kumsahau Bwana?”(“Tumeungana katika Kuujenga Ufalme wa Mungu,” Ensign, Mei 1987, 34 ).

Video kuhusu Usafi wa Kimwili (ChurchofJesusChrist.org)

  • “Ninachagua kuwa Msafi”

  • “Usafi wa kimwili: Mipaka Yake ni Ipi?”

  • “Sheria ya Usafi wa Kimwili”

Kuangalia zaidi ya lengo

Mzee Quentin L. Cook alifundisha jinsi tunavyoweza kuangalia “zaidi ya lengo”:

“Kubadilisha falsafa za binadamu kwa kweli za injili”

“Baadhi ya watu wanaonekana kuaibishwa na urahisi wa ujumbe wa Mwokozi. Wanataka kuongeza ugumu na hata giza kwenye ukweli kuufanya uwe zaidi wa kushindana kisomi au zaidi kulingana na mitindo ya kitaaluma ya sasa. … Tunatazama zaidi ya lengo tunapokataa kukubali kweli rahisi za injili kama vile zilivyo.”

“Siasa kali ya Injili”

“Tunaangalia zaidi ya lengo tunapoinua kanuni moja yoyote, bila kujali inaweza kuwa na maana kisasi gani, kwa umaarufu ambao unapunguza msimamo wetu kwa kanuni zingine zilizo sawa kwa umuhimu au tunapochukua msimamo ambao ni kinyume na mafundisho ya Akina Kaka.”

“Ishara za kishujaa kama mbadala wa utakaso wa kila siku”

“Baadhi ya washiriki wanatangaza kwamba wangejitolea kwa shauku kama watapewa baadhi ya wito mkubwa, lakini hawaoni mafundisho ya nyumbani au mafundisho ya kutembelea [sasa huitwa kuhudumia] kustahili kuwa au utoshelevu wa kishujaa kwa jitihada zao zilizoidhinishwa.”

“Kuinua sheria juu ya mafundisho”

“Wale wenye msimamo wa kufuata sheria bila marejeleo ya mafundisho na kanuni huathirika zaidi kuangalia zaidi ya lengo” (“Kuangalia Zaidi ya Lengo,” Ensign au Liahona, Mac, 2003, 42–44).

Chapisha