Njoo, Unifuate
Machi 2–8. 2 Nefi 31–33: “Hii Ndiyo Njia”


“Machi 2–8. 2 Nefi 31–33: ‘Hii Ndiyo Njia,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020.)

“Machi 2–8. 2 Nefi 31–33,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2020

Picha
Yesu anafundisha wafuasi Wake

Kristo anafundisha Wafuasi Wake, na Justin Kunz

Machi 2–8.

2 Nefi 31–33

“Hii Ndiyo Njia”

Unapojifunza 2 Nefi 31–33, wafikirie washiriki wa darasa lako na fikiria uzoefu gani wamewahi kuwa nao wa kweli Nefi alizofundisha. Jinsi gani unaweza kuwaomba kufundishana kile walichojifunza na kuhisi kuhusu mafundisho haya?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni kushiriki

Alika Kushiriki

Kuna yeyote katika darasa lako mwenye uzoefu wa maana wiki hii ya moja ya mapendekezo ya kujifunza katika Njoo Unifuate—Kwa ajili ya watu Binafsi na Familia? Wape washiriki wa darasa nafasi ya kushiriki uzoefu wao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

2 Nefi 31–32

Yesu Kristo na mafundisho yake ni njia pekee ya kuelekea uzima wa milele.

  • Labda inaweza kunufaisha darasa lako kuona jinsi imani, toba, ubatizo, karama za Roho Mtakatifu, na kuvumila mpaka mwisho vinahusiana na Upatanisho wa Yesu Kristo. Kwa hili, unaweza kuchora njia ubaoni na watake washiriki wa darasa kuandika kando kando ya njia baadhi ya kanuni zinazopatikana katika 2 Nefi 31. Kila mshiriki wa darasa anaweza kuchagua mojawapo ya kanuni hizi na kuchambua 2 Nefi 31–32 kupata kitu fulani ambacho Nefi alifundisha kuhusu hicho. Kisha wanaweza kushiriki wao kwa wao kile walichokipata na kujadili jinsi inavyowasaidia kuelewa kanuni vizuri zaidi. Jinsi gani kuishi kanuni hizi kunaleta baraka za upatanisho wa Yesu Kristo katika maisha yetu?

  • Unawezaje kuanza majadiliano juu ya mpango wa Nefi na maelezo ya kawaida ya “njia” hadi wokovu? (2 Nefi 31:21). Pengine ungeweza kuwauliza washiriki wa darasa nini wangesema kama wangekuwa na sekunde 60 tu kueleza nini mtu lazima afanye kupokea wokovu. Kisha washiriki wa darasa wangeweza kuchunguza 2  Nefi 31–32, wakitafuta maelezo ambayo yangeweza kusaidia. Tunajifunza nini kutoka sura hizi kuhusu jukumu hasa la Mwokozi katika wokovu wetu? Maelezo katika “Nyenzo za Ziada” yanaweza kuwa ya faida kwenye mazungumzo haya.

  • Wakati mwingine tunaona kanuni za injili kama tofauti, na zilizotengana, lakini kiukweli zinahusiana. Kusaidia washiriki wa darasa kuona jinsi kanuni katika 2 Nefi 31 zimeungana, waombe washiriki wa darasa, binafsi au katika makundi madogo, kusoma Mistari 4–21 na umba mchoro ambao unaonesha jinsi imani katika Kristo, toba, ubatizo, karama za Roho Mtakatifu, na kuvumilia mpaka mwisho hujengana wao kwa wao, kuhusiana wao kwa wao, na kuendelea. Watie moyo wawe wabunifu. Wanaposhiriki michoro yao na darasa, watake kushiriki kile walichojifunza kuhusu kanuni hizi. Tunawezaje kuzifanya ziwe sehemu ya maisha yetu ya kila siku?

2 Nefi 31:15–20.

“Yule atakayevumilia hadi mwisho, huyo ataokolewa.”

  • Je, washiriki wa darasa wanaelewa ina maana gani kuvumilia hadi mwisho? Hii hapa ni shughuli ambayo inaweza kusaidia. Andika ubaoni Jinsi gani ninajua kama ninavumilia hadi mwisho? Kisha watake washiriki wa darasa kuchambua 2  Nefi 31:15–20 kupata majibu ya kufaa kwa swali hili. Watake washiriki wa darasa kuandika ubaoni maneno yoyote yenye msaada au vishazi wanavyopata. Kwa nini kuvumilia mpaka mwisho ni sehemu muhimu ya mafunzo ya Kristo? Mnaweza pia kushiriki maelezo ya Mzee Dieter F. Uchtdorf katika “Nyenzo za Ziada” au maelezo kuhusu kuvumilia hadi mwisho kwenye ukurasa 6 wa Hubiri Injili Yangu.

  • Je, washiriki wa darasa wanamjua mtu yoyote ambaye ni mfano wa kuvumilia hadi mwisho? Ni nini kilimsaidia mtu huyu “kusonga mbele na uthabiti katika Kristo”? (mstari 20). Fikiria kushiriki hadithi za watu wengine waliotajwa katika maandiko ambao walivumilia hadi mwisho.

2 Nefi 32:1–6.

Roho Mtakatifu atatuonesha nini tunapaswa kufanya.

  • Katika 2 Nefi 32, Nefi alishughulikia shaka aliyoiona waliyokuwanayo watu wake kuhusu kutumia mafundisho ya Kristo. Unaweza kuwataka washiriki wa darasa kutafuta shaka hii katika 2 Nefi 32:1 na kisha soma jibu la Nefi katika 2 Nefi 32:2–6. Jinsi gani washiriki wa darasa watatamka tena kwa maneno yao wenyewe kile Nefi alichofundisha? Ni uzoefu gani washiriki wa darasa wamekuwa nao wakati Roho Mtakatifu au maneno Kristo yamewaonesha kile wanachohitaji kufanya?

2 Nefi 33

Kitabu cha Mormoni kinatushawishi kuamini katika Kristo.

  • Nefi alitegemea kwamba maneno yake yatatushawishi “kufanya mema [na] kuamini katika [Kristo]” (2 Nefi 33:4). Ni vifungu gani au hadithi kutoka 1 na 2 Nefi imetushawishi kufanya mema na kuamini katika Kristo? Fikiria kutafuta baadhi ya nyimbo darasa lako wataimba au kusikiliza kwa kile kinachoimarisha jumbe hizi, kama vile “I Believe In Christ” au “Have I Done Any Good?” (Nyimbo, namba. 134, 223).

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Njia moja ya kuwatia moyo washiriki wa darasa kujifunza Yakobo 1–4 wiki ijayo ni kueleza kwamba katika sura hizi watapata maonyo ya Yakobo kuhusu dhambi mbili mahususi ambazo zimeenea katika siku zetu.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Fundisho la Kristo

Mzee Jeffrey R. Holland alifundisha: “Fundisho la Kristo’ kama lilivyofundishwa na Nefi katika hotuba yake kubwa iliyofupishwa, linalenga juu ya imani katika Bwana Yesu Kristo, toba, ubatizo kwa uzamisho, kupokea karama ya Roho Mtakatifu, na kuvumilia hadi mwisho. Haijaribu, katika tamko hili kuzungumzia mpango mzima wa wokovu katika tangazo hili, fadhila zote za maisha ya Kikristo, au thawabu zinazotusubiri sisi katika hali tofauti ya utukufu wa mbinguni. Halifanyi chochote, katika tamko hili, kushughulika na afisi za ukuhani, ibada za hekalu, au mafundisho mengi mengine ya kweli. Yote haya ni muhimu, lakini kama yanavyotumika katika Kitabu cha Mormoni, ‘fundisho la Kristo’ ni rahisi na la moja kwa moja. Linalenga katika kanuni ya kwanza ya injili peke yake, ikiwa ni pamoja na onyesho la kutia moyo kuvumilia, kuendelea, na kusonga mbele. Kwa hakika, ni katika uwazi na unyenyekevu wa ‘fundisho la Kristo’ ambalo matokeo yake hupatikana” (Kristo na Agano Jipya: Ujumbe wa Kimasiya wa Kitabu cha Mormoni [1997], 49–50

Mzee D. Todd Christofferson alisema: “Ninawasihi wote … kutafuta kupitia sala na mafundisho ya maandiko ushahidi wa tabia tukufu, upatanisho, na ufufuo wa Yesu Kristo. Kubali fundisho Lake kwa kutubu, kubatizwa, kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, na kisha maisha yako yote kufuata sheria na maagano ya injili ya Yesu Kristo” (“The Doctrine of Christ,” Ensign au Liahona, Mei 2012, 89).

Kuvumila hadi mwisho.

Mzee Dieter F. Uchtdorf alifafanua:

“Nilipokuwa mvulana mdogo, ‘kuvumilia hadi mwisho’ ilimaanisha kwangu hasa kwamba nilipaswa kujaribu zaidi kuwa macho mpaka mwisho wa mikutano yetu ya Kanisa. Baadaye kama kijana… Niliunganisha hii na uwezo wa ujana wa kuhisi maono ya mwingine kwa juhudi za wapendwa wetu washiriki wazee kushikilia pale mpaka mwisho wa maisha yao. …

“… Kuvumila hadi mwisho sio tuu jambo la kuvumila bila hisia hali ngumu za maisha au ‘kuning’nia pale.’ Yetu ni dini hai, kusaidia watoto wa Mungu kwa kuambaa na njia nyembamba iliyosonga kujenga uwezekano wao kamili wakati wa maisha haya na kurudi kwake siku moja. Kuangaliwa kutoka taswira hii, kuvumilia hadi mwisho ni kuinuliwa na ni utukufu, sio kutisha na kusononesha. Hii ni dini ya shangwe, mojawapo ya matumaini, nguvu, na wokovu, …

“Kuvumilia hadi mwisho inamaanisha ‘uendelevu wenye subira katika kutenda mema’ (Warumi 2:7), kujitahidi kutii amri (ona 2 Nefi 31:10). Na kufanya kazi za wenye haki (ona M&M 59:23)” (“Have We Not Reason to Rejoice?Ensign ama Liahona, Nov. 2007, 20.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tunajifunza Pamoja. Kama mwalimu, unafanya zaidi ya kusambaza taarifa—unajifunza pamoja na darasa lako zima. Shiriki pamoja nao kile unachofanya kujifunza kutoka katika maandiko.

Chapisha