Njoo, Unifuate
Juni 15–21. Mosia 13–16: “Ingia katika Pumziko la Bwana”


“Juni 15–21. Alma 13–16 : ‘Ingia katika Pumziko la Bwana,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Juni 15–21. Alma 13–16,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2020

Picha
Alma na Amuleki wakitembea kutoka gerezani

Kielelezo cha Alma na Amuleki wakikombolewa kutoka gerezani, na Andrew Bosley

Juni 15–21.

Alma 13–16

“Ingia katika Pumziko la Bwana”

Mazungumzo ya kudumu yanahitaji zaidi ya somo la kuvutia la shule ya Jumapili mara moja kwa wiki. Watie moyo washiriki wa darasa kutafuta uzoefu binafsi wa kiroho wiki mzima.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni kushiriki

Alika Kushiriki

Nini kinaweza kushawishi washiriki wa darasa kushiriki uzoefu wao pamoja na kujifunza na kuishi injili? Labda ungewaalika kushiriki umaizi walioupata katika Alma 13–16 ambao uliwashangaza au ambao hawakuufikiria hapo mwanzo. Wanaposhiriki, waulize jinsi wanavyohisi umaizi huu mpya utaleta tofauti katika maisha yao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Alma 13:1–19.

Ibada za kikuhani zinasaidia watoto wa Mungu kupokea ukombozi kutoka kwa Yesu Kristo.

  • Baadhi ya washiriki wa darasa lako wanaweza kuwa wameona kitu fulani ambacho kiliwaletea shukrani za kina kwa ukuhani walipojifunza Alma 13. Waalike waelezee kile walichokiona. Mngeweza pia kusoma pamoja mistari 2 na 16 na kuuliza swali kama “Jinsi gani ukuhani na ibada zake zinakusaidia ‘kumtazamia Mwana wa [Mungu] kwa ajili ya ukombozi’? Kama inasaidia, orodha ya ibada inaweza kupatikana katika True to the Faith, 109–10.

    Picha
    Vijana kwenye meza ya sakramenti

    Ibada za Ukuhani zinatusaidia kumtazama Yesu Kristo kwa ajili ya ukombozi.

  • Watu wengi katika Amoniha walikuwa wafuasi wa Nehori, ambaye alifundisha mawazo ya uongo kuhusu jukumu la makuhani. Kuwasaidia washiriki wa darasa kujifunza kuhusu asili ya kweli ya ukuhani, ungeweza kuwataka kutofautisha maoni ya Nehori ya kile makuhani wanapaswa kufanya (ona Alma 1:3–6) na kile Alma alichofundisha (ona Alma 13:1–12). Katika njia gani mafundisho ya Nehori yanafanana na maoni ya ulimwengu kuhusu nguvu na uongozi? Mafundisho ya Alma ni tofauti kwa jinsi gani?

  • Kusoma Alma 13:1–9 kunaweza kuongoza kwenye majadiliano kuhusu “kujiandaa kutoka msingi wa ulimwengu” kwa ajili ya majukumu yetu katika kazi ya Bwana. Ni nini Alma 13:3 inapendekeza kuhusu njia tunayopaswa kufikiria au kukaribia majukumu haya? (ona pia M&M 138:56).

Alma 13.

Mwokozi anatualika tuingie katika pumziko Lake.

  • Alma alifundisha kwamba ukuhani unatusaidia “kuingia katika pumziko la Bwana” (Alma 13:16). Kuanza majadiliano kuhusu wazo hili, ungeweza kuwataka washiriki wa darasa kusoma Alma 13:6, 12–13, 16, na 29 na kushiriki kile mistari hii inafundisha kuhusu “Pumziko la Bwana.” Wangeweza pia kutambua sifa bainifu za watu ambao “wanaingia katika pumziko la Bwana.” Tufanye nini ili tupate uzoefu wa pumziko la Bwana wakati wa maisha yetu hapa duniani?

Alma 14.

Katika nyakati za majaribu na masikitiko, lazima tumtegemee Bwana.

  • Alma 14 ingeweza kuwa nafasi ya kujadili jinsi tunavyoweza kukubali kwa uaminifu wakati sisi au wapendwa wetu wanakabiliana na mateso au majaribu hata wakati tunajaribu kuwa waadilifu. Unaweza kuanza kwa kuwaalika washiriki wa darasa kufikiria kwamba wao ni waandishi wa habari wakiripoti tukio katika Alma 14. Ni maswali aina gani wangeweza kumwuliza Alma au Amuleki kuhusu tukio hili? Kwa mfano, “Kwa nini Mungu anakuruhusu wewe na watu wengine waadilifu kuteseka?” au “Ni ushauri gani ulionao kwa wale wanaopitia majaribu magumu?” Kutokana na kile tunachojua kutoka Alma 14, Alma au Amuleki wangejibu maswali haya vipi?

  • Wengi wetu tunaweza kuhusisha kwa kiasi fulani kwa njia Amuleki alivyohisi wakati aliposhuhudia mateso ya watu waaminifu wa Amoniha: “sisi pia tunaumia” (Alma 14:10), na tunatamani tungeweza kufanya kitu fulani kuhusu hilo. Tunajifunza nini kutokana na kile Alma alichosema katika hali hii? (ona Alma 14:8–13). Ungeweza kushiriki kauli kutoka kwa Rais Spencer W. Kimball katika “Nyenzo za Ziada.” Labda washiriki wa darasa wangeweza kufanya muhtasari wa ujumbe mkuu wa kauli ya Rais Kimball katika maneno yao wenyewe.

Alma 3:16 18

Ufuasi unahitaji dhabihu.

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapendekeza kuorodhesha nini Amuleki aliacha na mimi alipata wakati alipokumbatia injili. Labda washiriki wa darasa watakuwa tayari kushiriki orodha walizozitengeneza, au wangetengeneza orodha hizi darasani. Maandiko haya yanaweza kusaidia: Alma 10:4–5; 15:16, 18; 16:13–15; na 34:8. Kwa nini Amuleki alikuwa tayari kufanya dhabihu kama hizo? Kwa nini sisi tupo tayari kufanya hivyo? Jinsi gani tunaweza kuufuata mfano wa Alma, ambaye “alimuimarisha [Amuleki] katika Bwana”?

Alma 16:1–10.

Maneno ya manabii yatatimizwa.

  • Alma 16 inatoa mifano ya mtu fulani ambaye alimwamini nabii na wa watu ambao hawa kumwamini. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kujifunza kutoka mifano hii, ungeweza kuandika ubaoni vichwa vya habari viwili: Zoramu na Watu wa Amoniha. Washiriki wa darasa wangeweza kusoma Alma 16:1–10 na kuandika chini ya kila kichwa cha habari maneno na vishazi ambavyo vinaelezea fikra walizokuwa nazo watu hawa juu ya maneno ya nabii Alma. Je, sisi tunafanya nini kumwonyesha Baba wa Mbinguni kwamba tuna imani katika maneno ya manabii wanaoishi?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Fikiria kuwauliza washiriki wa darasa kama kwa wakati wowote wamewahi kutamani wangeweza kuwa bora katika kushiriki injili. Kusoma Alma 17–22 kunaweza kuwavutia na mawazo ya kuwasaidia kukamilisha lengo hii.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Mungu hazuii siku zote janga.

Rais Spencer W. Kimball mwanzo alitoa maoni juu ya mengi ya huzuni yanavyoonekana kwa nje yasiyoelezeka ambayo yanatokea katika ulimwengu:

“Mungu angeweza kuzuia majanga haya? Jibu ni, Ndiyo. Bwana ni Mwenyezi, na ana uwezo wote wa kuamuru kusimamia maisha yetu, kutuokoa na maumivu, kuzuia ajali zote, … hata [kutulinda] kutoka kifo, kama akipenda. Lakini hata fanya hivyo. …

“Kama wagonjwa wote ambao tunawaombea wangeponywa, kama wenye haki wote wangelindwa na waovu kuangamizwa, mpango mzima wa Baba ungepotea bure, na kanuni ya msingi ya injili, haki ya kujiamulia, ungemalizika. Hakuna mtu angelazimika kuishi kwa imani. …

“… Kama tungekuwa wa kufunga milango juu ya huzuni na shida, tunaweza kuwatenga marafiki zetu wakubwa mno na wafadhili. Kuteseka kunaweza kuwafanya watu kuwa watakatifu wanapojifunza uvumilivu, subira, na umahiri kibinafsi. …

“… Ninashukuru kwamba hata kupitia ukuhani siwezi kuwaponya wagonjwa wote. Ningeweza kuponya watu ambao wangekufa. Ningeweza kuwapunguzia watu kuteseka ambako wangeteseka. Ninaogopa ningezuia makusudi ya Mungu.

“Ningekuwa na uwezo usio na kikomo, na bado maono na uelewa wenye kikomo, ningeweza kumwokoa Abinadi kutoka miali ya moto wakati alipochomwa moto kwenye nguzo, na kwa kufanya hivyo ningemdhuru kwa njia isiyorekebishika. Alikufa shahidi na alikwenda kwenye zawadi ya ushahidi—kuinuliwa.

“Huenda ningemlinda Paulo dhidi ya maadui zake kama uwezo wangu ungekuwa hauna kikomo. Kwa hakika ningeponya ‘mwiba wake katika mwili’ [2 Wakorintho 12:7.] Na kwa kufanya hivyo ningekuwa nimezuia mpango wa Bwana. …

“Ninahofia kwamba kama ningekuwa katika gereza la Carthage mnamo Juni 27, 1844, ningeweza kupangua risasi ambazo zilitoboa mwili wa Nabii [Joseph Smith] na Baba Mkuu [Hyrum Smith]. Ningeweza kuwaokoa kutoka mateso na maumivu, bali walipotea kwenye kifo cha mashahidi. …

“Pamoja na uwezo usioweza kudhibitika, kwa hakika ningehisi kumlinda Kristo kutoka maumivu katika Gethsemane, matusi, taji la miiba, ufedhuli mahakamani, majeraha ya kimwili. Ningehudumia vidonda vyake na kuviponya, nikimpa maji ya kutuliza badala ya siki. Ningeweza kumwokoa kutoka mateso na kifo, na kupoteza ulimwenguni dhabihu yake ya upatanisho. …

“Katika sura ya huzuni dhahiri lazima tuweke imani yetu katika Mungu, tukijua kwamba licha ya maono yetu yenye kikomo azma zake hazitashindwa” (Mafundisho ya Marais wa Kanisa: Spencer W. Kimball [2006], 14–17, 20).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Alika kujifunza kwa bidii. “Wakati unapojiandaa kufundisha, badala ya kufikiria, “Ni nini nitafanya ili nifundishe?’ jiulize, “Ni nini washiriki wa darasa langu watafanya ili wajifunze?’” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 29).

Chapisha