Mafundisho na Maagano 2021
Mei 17–23. Mafundisho na Maagano 51–57: “Mtumishi Mwaminifu, Mwenye Haki, na Mwenye Hekima”


“Mei 17–23. Mafundisho na Maagano 51–57: ‘Mtumishi Mwaminifu, Mwenye Haki, na Mwenye Hekima,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Mei 17–23. Mafundisho na Maagano 51–57,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili

Picha
mkulima pamoja na maksai

Mfuo wa Kwanza, na James Taylor Harwood

Mei 17–23

Mafundisho na Maagano 51–57

“Mtumishi Mwaminifu, Mwenye Haki, na Mwenye Hekima”

Wakati mwingine msukumo kuhusu kitu cha kufundisha huja wakati unapojadili maandiko pamoja na mwanafamilia au rafiki.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Fikiria maneno haya kutoka kwa Mzee Quentin L. Cook: “Tumaini langu ni kwamba kila mmoja wetu atafanyia mapitio kibinafsi na kama familia utumishi ambao kwa huo tuna wajibu na tunahusika” (“Utumishi—Wajibu Mtakatifu,” Ensign au Liahona, Nov. 2009, 94). Kisha unaweza kuwauliza washiriki wa darasa kile walichojifunza kutoka sehemu za 51–57 kuhusu utumishi wao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 51:9, 15–20

Bwana anatutaka tuwe waaminifu, wenye haki, na watumishi wenye hekima.

  • Ni jinsi gani utawasaidia washiriki wa darasa kufikiria namna ambavyo maneno ya Bwana katika sehemu ya 51 yanatumika kwao? Unaweza kuandika kwenye ubao Ni nini ambacho Bwana amenikabidhi? Na uwaalike washiriki wa darasa waorodheshe majibu yao (ona “Nyenzo za Ziada” kwa ajili ya mawazo). Kisha wanaweza kutafuta kanuni katika mistari 9, 15–20 ambazo zinawafundisha jinsi ya kuwa watumishi bora wa vitu vilivyo kwenye orodha yao. Au unaweza kufokasi kwenye maneno “mwaminifu,” “haki,” na “hekima” katika mstari wa 19, kujadili jinsi ambavyo kila moja ya maneno haya yanaweza kutuongoza katika kutimiza wajibu wetu. Ikihitajika, fanyeni pamoja mapitio ya ufafanuzi wa “Mtumishi, Utumishi” katika Mwongozo wa Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org).

Picha
shamba la rangi ya kijani kibichi

Washiriki walioishi sheria ya kuweka wakfu walitoa sadaka ya kila walichokuwa nacho kwa Kanisa.

Mafundisho na Maagano 52:10; 53:3; 55:1–3

Kipawa cha Roho Mtakatifu hutolewa kwa kuwekewa mikono.

  • Mistari mingi katika ufunuo huu inataja kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu kupitia kuwekewa mikono. Kama mjadala kuhusu mada hii ungekuwa na manufaa kwa darasa lako, unaweza kuwauliza washiriki wa darasa kile wanachojifunza kutoka Mafundisho na Maagano 52:10; 53:3; 55:1–3 kuhusu kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa zaidi kuhusu mada hii, ona Matendo 8:14–17; 19:1–6. Labda washiriki wa darasa wanaweza kuzungumza kuhusu uzoefu wao wa kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu au kile ambacho wanaweza kufanya ili kuendelea kupokea ushawishi Wake katika maisha yao.

Mafundisho na Maagano 52:9–11; 22–27

Tunaweza kushiriki injili popote tulipo.

  • Wakati Bwana alipowatuma viongozi kadhaa wa Kanisa kule Missouri, aliwaambia watumie muda wao safarini na “wahubiri njiani” (mistari 25–27). Kusoma Mafundisho na Maagano 52:9–11, 22–27 kunaweza kuongoza kwenye mazungumzo kuhusu jinsi ambavyo tunaweza kushiriki injili “njiani,” au wakati wa uelekeo wa kawaida katika maisha yetu. Washiriki wa darasa wanaweza kuzungumza kuhusu namna ambavyo wanafanya kushiriki injili kuwa sehemu ya kawaida ya maisha yao.

Mafundisho na Maagano 52:14–19

Mungu alitoa mpangilio wa kuepuka udanganyifu.

  • Ili kuwasilisha mpangilio ambao Bwana alifunua katika Mafundisho na Maagano 52:14–19, unaweza kushiriki mifano ya mipangilio mingine ambayo inaweza kuwa inajulikana kwa washiriki wa darasa, kama vile mipangilio ya kujenga vitu au mipangilio ya tabia. Washiriki wa darasa wanaweza kuwa na mifano yao binafsi ya kushiriki. Ni kwa nini mipangilio ina thamani. Tunawezaje kutumia mpangilio katika mistari 14–19 kuepuka udanganyifu ambao tunaupata ulimwenguni leo?

Mafundisho na Maagano 54

Naweza kumgeukia Bwana wakati ninapoumizwa na chaguzi za wengine.

  • Wengi wetu tumesikitishwa wakati mtu ambaye tulimtegemea hakuheshimu ahadi zake. Hili liliwatokea Watakatifu kutoka Colesville, New York, ambao walitarajia kuweka makazi kwenye shamba la Leman Copley huko Ohio. Ili kujifunza kutokana na tukio hili, washiriki wa darasa wanaweza kufanya mapitio ya kichwa cha habari cha sehemu ya 54 (ona pia Watakatifu, 1:125–28; “Askofu wa Kanisa,” Ufunuo katika Muktadha, 78–79). Wanaweza kupiga taswira kwamba walikuwa na rafiki miongoni mwa Watakatifu wa Colesville na kisha watafute ushauri katika sehemu ya 54 ambao wanaweza kuushiriki na rafiki yao. Au wanaweza kuchunguza ufunuo kwa ajili ya kitu ambacho kinaweza kumsaidia mtu ambaye anateseka kwa sababu ya chaguzi za mtu mwingine. (Unaweza kuonesha ahadi iliyoko katika mstari wa 6 kwa wale ambao huheshimu maagano yao.)

  • Mafundisho na Maagano 54:10 ina virai kadhaa ambavyo washiriki wa darasa lako wanaweza kuona ni vya maana, kama vile “wavumilivu katika taabu,” “wamenitafuta mapema,” na “pumziko nafsini mwao.” Washiriki wa darasa wanaweza kuchagua kirai ili watafakari na wajifunze, kwa kutumia marejeo au nyenzo zingine ili kuchunguza maandiko husika. Kisha wanaweza kushiriki mawazo yao.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Utumishi wetu.

Rais Spencer W. Kimball alieleza: “Katika Kanisa utumishi ni wajibu mtakatifu wa kiroho au wa kimwili ambapo kuna kuwajibika. Kwa sababu vitu vyote ni vya Bwana, sisi ni watumishi wa miili yetu, akili, familia, na mali. (Ona Mafundisho na Maagano 104:11–15.) Mtumishi mwaminifu ni yule ambaye hutumia mamlaka kwa haki, hujali familia yake, na kuwajali masikini na wanaohitaji msaada” (“Welfare Services: The Gospel in Action,” Ensign, Nov. 1977, 78).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie Wanafunzi ili Wasaidiane wao kwa wao. Buni mazingira ya darasa ambapo wanafunzi wanasaidiana na kuwatia moyo wenzao. Waalike kushiriki mawazo na mbinu ambazo zinaboresha kujifunza kwao binafsi na kama familia. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 36.)

Chapisha