Mafundisho na Maagano 2021
Oktoba 4–10. Mafundisho na Maagano 111–114: “ Nitapanga Mambo Yote Kwa Faida Yenu”


“Oktoba 4–10. Mafundisho na Maagano 111–114: ‘Nitapanga Mambo Yote kwa Faida Yenu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Oktoba 4–10. Mafundisho na Maagano 111–114,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2021

Picha
Joseph Smith akihubiri

Oktoba 4–10

Mafundisho na Maagano 111–114

“Nitapanga Mambo Yote kwa Faida Yenu”

Unaposoma Mafundisho na Maagano 111–14, zingatia ukweli wa kiroho ambao Bwana anataka washiriki wa darasa kuelewa. Roho Mtakatifu atasaidia kukuongoza kujua kanuni zipi za kutilia mkazo.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki na wengine

Alika Kushiriki

Fikiria kuchora sanduku la hazina ubaoni. Washiriki wa darasa wangeweza kuandika ubaoni mistari kutoka sehemu ya 111–14 pale ambapo wamepata kitu ambacho wamekiona kuwa “cha thamani zaidi” (Mafundisho na Maagano 111:2). Waombe baadhi ya washiriki kushiriki kile walichopata ambacho ni cha thamani kwenye mistari hiyo.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 111

Bwana anaweza “kuyapanga mambo yote kwa faida [yetu].”

  • Ushauri wa Bwana katika Mafundisho na Maagano 111 unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa lako pale wanapohofia kuhusu wasiwasi wa kimwili au wa kiroho, kama ulivyomsaidia Joseph Smith na wasiwasi wake kuhusu Sayuni. Ungeweza kuanza mjadala wa sehemu hii kwa kuwakaribisha washiriki wa darasa kuorodhesha kwenye ubao vitu ambavyo wao au watu wanaowajua wanahofia. Kisha, kwa dhana hilo akilini, wangetafuta sehemu ya 111 kwa ushauri na faraja ambayo Bwana hutoa kutusaidia. Washiriki wa darasa wangeshiriki jinsi ambavyo Mwokozi amewasaidia walipoweka imani yao Kwake.

  • Washiriki wa darasa lako yaweza kuwa wamekuwa na uzoefu kama wa Joseph—walipohisi kuwa Mungu aliwakubali licha ya “upumbavu” wao (Mafundisho na Maagano 111:1). Je, ni kwa namna gani uzoefu wao ni mfano wa kweli zinazofundishwa katika Mafundisho na Maagano 111? Kwa mfano, ni wakati gani walihisi kuwa Bwana [“alipanga] mambo yote kwa faida [yao]”? (mstari wa 11). Je, uzoefu huu unawafundisha nini kuhusu Mwokozi na kuhusu wao wenyewe?

Mafundisho na Maagano 112:3–15, 22

Bwana atawaongoza wale wanaotafuta mapenzi Yake kwa unyenyekevu.

  • Kuwasaidia washiriki wa darasa kujadili kile sehemu ya 112 inachofundisha kuhusu unyenyekevu, fikiria kuligawa darasa katika vikundi vitatu. Kipe kila kikundi mojawapo ya maswali yafuatayo kutafakari wanapotathmini mistari 3–15 na 22: Unyenyekevu ni nini? Tunawezaje kuwa wanyenyekevu zaidi? Je, ni baraka gani zimeahidiwa kwa wanyenyekevu? Vipe vikundi muda wa kujadili majibu yao. Makundi hayo yangeweza kupata utambuzi wa nyongeza kwa kusoma maelezo ya Mzee Elder Quentin L. Cook’s katika “Nyenzo za Ziada” au sehemu yenye kichwa cha habari “Humility” katika Preach My Gospel (ukurasa wa 126–27). Kwa nini unyenyekevu ni muhimu kwa ajili ya kufanya kazi ya Bwana?

    Picha
    watu wawili wakisali

    Ikiwa tu wanyenyekevu, Bwana atatuongoza na kujibu maombi yetu.

Mafundisho na Maagano 112:12–26

Wale ambao kwa kweli wameongoka humjua Yesu Kristo.

  • Ukweli kwamba baadhi ya mitume katika mwaka 1837 waligeuka dhidi ya Nabii ni ukumbusho mzuri kwamba licha ya mwito ambao tunao au ni kwa kiasi gani tunaijua injili, lazima kibinafsi tuhakikishe kuwa tumeongoka kweli kweli. Kusoma ushauri ambao Bwana alimpa Thomas B. Marsh kumsaidia kuunganisha Akidi ya wale Kumi na Wawili kunaweza kulipa darasa lako utambuzi kwenye nini maana ya kuongoka. Labda washiriki wa darasa wangesoma Mafundisho na Maagano 112:12–26 wakiwa na mwanafamilia au rafiki akilini—mtu ambaye labda anahangaika na imani yake. Ni ukweli upi katika vifungu hivi washiriki wa darasa wangetilia mkazo kumsaidia mtu huyo kuwa mwongofu kikamilifu zaidi? Wape washiriki wa darasa muda kutafakari kile wanachoweza kufanya kuupa nguvu uongofu wao wenyewe kwa Bwana.

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Mfano wa Sifa ya Yesu Kristo ya Unyenyekevu.

Mzee Quentin L. Cook alifundisha:

“Kwa bahati mbaya, katika siku yetu katika karibu kila sehemu ya jamii, tunaona umaarufu-binafsi na kiburi vikiinuliwa wakati unyenyekevu na uwajibikaji kwa Mungu vinashushwa. Sehemu kubwa ya jamii imepoteza maadili yake na haielewi kwa nini tuko kwenye dunia hii. Unyenyekevu wa kweli, ambao ni muhimu kwa kufikia kusudi la Mungu kwetu, unaonekana kwa uchache.

“Ni muhimu kuelewa ukubwa wa unyenyekevu, haki, tabia na akili ya Kristo, kama vinavyotolewa mfano katika maandiko. Ni upumbavu kupuuza umuhimu wa kuendelea kujitahidi kwa ajili ya tabia hizi za mfano wa Kristo na sifa kila siku, hasa sana unyenyekevu. …

“Mnamo Julai 23, 1837, Nabii Joseph alikutana na Mzee Thomas B. Marsh, Rais wa Akidi ya wale Kumi na Wawili. Mzee Marsh alionekana kuvunjika moyo kwamba Nabii alikuwa amewaita washiriki wawili wa akidi yake ili kwenda Uingereza bila kumshirikisha yeye. Wakati Joseph alipokutana na Mzee Marsh, hisia zote za uchungu ziliwekwa kando, na Nabii akapokea ufunuo wa ajabu. Sasa ni sehemu ya 112 ya Mafundisho na Maagano. Inatoa mwongozo wa ajabu kutoka mbinguni na heshima kwa unyenyekevu na kazi ya umisionari. Mstari wa 10 unasomeka, ‘Jinyenyekeze; na Bwana Mungu wako atakuongoza kwa mkono, na kukupa jibu la sala zako’ [Mafundisho na Maagano 112:10; mkazo umeongezwa]” (“Milele Kila Siku,” Ensign au Liahona, Nov. 2017, 51–52).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fokasi kwenye watu. “Jinsi unavyowatendea watu ni muhimu kama vile yale unayowafundisha. Mara nyingine kushughulika kwetu zaidi kwenye kuwasilisha somo kunaweza kutuzuia kuonesha upendo wetu kwa wale tunaowafundisha. … Fikiria jinsi ambavyo unaweza kufokasi katika kile kilicho muhimu zaidi” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,6)

Chapisha