Mafundisho na Maagano 2021
Oktoba 25–31. Mafundisho na Maagano 124: “Nyumba kwa Jina Langu”


“Oktoba 25–31. Mafundisho na Maagano 124: ‘Nyumba kwa Jina Langu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Mafundisho na Maagano 2021 (2020)

“Oktoba 25–31. Mafundisho na Maagano 124,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2021

Picha
Nauvoo

Nauvoo, Mji Mzuri, na Larry Winborg

Oktoba 25–31

Mafundisho na Maagano 124

“Nyumba kwa Jina Langu”

Ili Roho aweze kuleta kanuni katika kumbukumbu zetu tunapofundisha (ona Yohana 14:26), kwanza ni lazima tusome na kutafakari kanuni hizo kwa bidii.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Zingatia kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki kile walichokipata katika Mafundisho na Maagano 124 ambacho kiliwafanya wazingatie kanuni ya injili katika njia mpya. Je walisoma nini—binafsi ama kama familia—ambacho kimebadilisha jinsi wanavyohisi, kufikiri au kuishi?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mafundisho na Maagano 124:15, 20

Bwana hufurahia uadilifu.

  • Katika sehemu ya 124, Bwana alimsifu Hyrum Smith na George Miller kwa uadilifu wao. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kusoma sifa hii kwa undani zaidi, ungeweza kuwaalika kusoma Mafundisho na Maagano 124:15, 20 na kufikiria wanachojifunza kuhusu uadilifu kutoka kwenye mistari hii. Ni nini kingine tunajifunza kutokana na maandiko yaliyoorodheshwa chini ya “Uadilifu” katika Mwongozo kwenye Maandiko (scriptures.ChurchofJesusChrist.org) au kutoka kwenye ujumbe wa Mzee Richard J. Maynes “Kupata Kuaminiwa na Bwana na Familia Yako”? (Ensign au Liahona, Nov. 2017, 75–77). Labda washiriki wa darasa wangeweza kushiriki mifano ya watu wanaowajua kuwa wana uadilifu. Kwa nini uadilifu ni sifa inayothaminiwa hivyo?

Mafundisho na Maagano 124:22–24, 60–61

Bwana anatutaka tuwakaribishe na kuwakubali wengine.

  • Washiriki wa darasa lako wanaweza kujifunza kitu kutokana na maelezo ya Bwana kuhusu Nyumba ya Nauvoo kinachoweza kuwasaidia katika kuchangamana kwao na watu ambao si Watakatifu wa Siku za Mwisho ama ambao wamejitenga na Kanisa. Ungeweza kuchora nyumba ubaoni na kuwaalika washiriki wa darasa kutafuta toka Mafundisho na Maagano 124:22–24, 60–61 maneno ambayo Bwana alitumia kufafanua madhumuni ya Nyumba ya Nauvoo. Kisha wangeweza kuandika maneno hayo kuzunguka nyumba hiyo. Maneno haya yangewezaje kutumika katika Kanisa la Yesu Kristo? Je, tunaweza kufanya nini ili kuunda utamaduni huu wa makaribisho katika kata yetu na nyumba zetu?

Mafundisho na Maagano 124:25–45, 55

Bwana anatuamuru tujenge mahekalu ili tuweze kupokea ibada takatifu.

  • Labda washiriki wa darasa wangeweza kufikiria kana kwamba wanaishi Nauvoo mwaka 1841 na kufanyia kazi Hekalu la Nauvoo wakati rafiki anapouliza, “Je, kwa nini tunaendelea kujenga mahekalu haya?” Je, tungesema nini kwa rafiki huyu? Washiriki wa darasa wangeweza kutafuta mawazo katika Mafundisho na Maagano 124:28–30, 37–42, 55. Ikiwa baadhi ya washiriki wa darasa hawana ufahamu wa ibada zilizotajwa katika mistari hii, zingatia kufafanua madhumuni na baraka za ibada hizi. Ona temples.ChurchofJesusChrist.org kwa ajili ya mwongozo kuhusu kile ambacho kinaweza kujadiliwa nje ya hekalu na kwa picha za mahekalu ambazo unaweza kuonesha darasani.

    Picha
    Joseph Smith na wanaume wengine wakijenga Hekalu la Nauvoo

    Joseph Smith katika Hekalu la Nauvoo, na Gary E. Smith

Mafundisho na Maagano 124:45–55

Bwana atawabariki wale ambao wanajitahidi kutii amri zake.

  • Watakatifu walikuwa wamepewa amri ya kujenga hekalu katika Wilaya ya Jackson lakini “walizuiliwa na maadui zao” (Mafundisho na Maagano 124:51). Katika mistari 49–55, ambapo Bwana alizungumzia hali hii, kunaweza kuwa na ujumbe wa hakikisho kwa watu ambao wanataka kutii amri za Mungu lakini wanazuiliwa kufanya hivyo kwa sababu ya familia au sababu zingine. Ungeweza kusoma mistari hii pamoja na washiriki wa darasa na uwaombe wafikirie hali ambazo watu wanaweza kushindwa kutimiza matamanio yao ya haki kwa sababu ya hali ambazo ziko nje ya uwezo wao. Je, ni ushauri upi tunaupata katika mistari hii ambao ungeweza kumsaidia mtu katika hali kama hiyo? Je, mistari hii inatufundisha nini kuhusu utii?

Mafundisho na Maagano 124:91–92

Bwana anaweza kutuongoza kupitia baraka zetu za patriaki.

  • Je, washiriki wa darasa lako wangenufaika kutokana na majadiliano kuhusu mapatriaki na baraka za patriaki? Ungeweza kuanza kwa kuwaalika washiriki wa darasa kusoma Mafundisho na Maagano 124:91–92, wakiangalia kile ambacho Hyrum Smith aliitwa kukifanya. Kisha ungeweza kuandika ubaoni Nini na Kwa nini na kuwaalika washiriki wa darasa kusoma “Patriarchal Blessings” (True to the Faith, 111–13) ili kujua baraka za patriaki ni nini na kwa nini zina thamani. Je, mtu anawezaje kujiandaa kupokea baraka ya patriaki? Zingatia kuwaalika watu wachache ambao wamekwishapokea baraka zao za patriaki ili kushiriki ni kwa nini wao wanashukuru kuwa na hizo baraka. (Wakumbushe kutoshiriki chochote ambacho ni cha binafsi sana au kitakatifu sana kutoka kwenye baraka zao.) Je, tunawezaje kuonyesha kwamba tunathamini baraka zetu za patriaki?

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Omba kwa ajili ya washiriki wa darasa lako. Omba kwa kuwataja majina wale unaowafundisha. Unaweza kuomba ili kufahamu mahitaji yao na kujua kitu cha kufundisha ili kukidhi mahitaji hayo. Pia ungeweza kumuomba Baba wa Mbinguni “kuandaa mioyo yao” (Alma 16:16) ili kupokea kweli ambazo utazifundisha. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 6.)

Chapisha