Njoo, Unifuate
Januari 7–13. Mathayo 1; Luka 1: ‘Na Iwe Kwangu kama Ulivyosema’


Januari 7-13. Mathayo 1; Luka 1: ‘Na Iwe Kwangu kama Ulivyosema” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Shuie ya Jumapili: Agano Jipya 2019 (2019)

“Januari 7–13. Mathayo 1; Luka 1,” Njoo,Unifuate—Kwa ajili ya Shule ya Jumapili: 2019

Picha
Mariamu na Elizabeti

Januari 7–13

Mathayo 1; Luka 1

“Na Iwe Kwangu kama Ulivyosema”

Kabla hujasoma nyenzo yoyote ya kujifunza ya ziada, soma na utafakari Mathayo 1 na Luka 1, na uandike misukumo ya kiroho. Mwachie Roho aongoze maandalizi yako. Kisha chunguza mawazo katika muhtasari huu na katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Himiza Kushiriki

Wape washiriki wa darasa dakika chache kurejea Mathayo 1 au Luka 1, na waalike washiriki aya zao wazipendazo na kueleza kweli gani za kimafundisho walizojifundisha. Unaweza kuona kuwa inasaidia kurejea kwa kifupi matukio katika aya hizi kwanza kutoa muktadha fulani kwa aya walizoshiriki.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mathayo 1:16–25; Luka 1:5–80

Baba wa Mbinguni hufanya kazi kupitia watoto Wake waaminifu kukamilisha azma zake.

  • Washiriki wa darasa wataelekea zaidi kuwa na uzoefu wa maana wakati wakijifunza Agano Jipya mwaka huu kama wanaweza kupata masomo kutoka uzoefu wa watu waliosoma kuwahusu. Kuwasaidia kufanya hivi, unaweza kuandika majina ya watu katika Mathayo 1 na Luka 1 ubaoni, pamoja na marejeo ya maandiko kuhusu watu hawa, kama ifuatavyo:

    Waalike washiriki wa darasa kumchagua mtu mmoja wangependa kujifunza zaidi kumhusu, kusoma aya zilizoorodheshwa, na kushiriki na mtu mwingine katika darasa kile wanajifunza kutoka uzoefu wa mtu yule. Tunaweza kufanya nini ili kufuata mfano wa imani ya mtu yule?

    Picha
    Gabrieli anamtokea Mariamu

    Upashaji Habari, na John Scott

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kufikiria kwa kina kuhusu silika ya Mariamu na wajibu wake katika mpango wa Baba, unaweza kuonyesha video “Malaika Anatabiri Kuzaliwa kwa Kristo kwa Mariamu” na “ Mariamu na Elizabeti Wanafurahia Pamoja” (LDS.org) au kusoma pamoja Luka 1:26–38, 46–56, kutafuta mambo aliyosema Mariamu ambayo yanaonyesha kitu fulani kuhusu silika yake. Kitu gani kingine tunachojifunza kumhusu Mariamu? Nini anaweza kutufundisha kuhusu kukubali mapenzi ya Mungu kwa ajili yetu?

Luka 1:5–25

Baraka za Mungu zinakuja kwa wakati Wake mwenyewe.

  • Kunaweza kuwa na watu katika darasa lako ambao, kama Elizabeti na Zakaria, wanaishi maisha ya uadilifu na bado hawajapokea baraka walizotegemea. Ni kwa jinsi gani unaweza kuwasaidia kujifunza kutoka kwa mifano ya Elizabeti na Zakaria? Unaweza kuanza kwa kuwaomba washiriki wa darasa waandike baraka wanazotegemea. Kisha wanaweza kupekua Luka 1:5–25, wakitafuta masomo wanayoweza kujifunza kutoka kwa Elizabeti na Zakaria kuhusu kumsubiri Bwana. Wanaweza pia kusoma na kutafakari dondoo katika “Nyenzo za Ziada.” Wahimize waandike kile wanajifunza kufuatana na baraka zilizotegemewa na, kama inafaa, shiriki mawazo yao.

  • Mifano gani mingine ya kusubiri mpangilio wa Bwana washiriki wa darasa wanaweza kushiriki kutoka maisha yao wenyewe au kutoka matukio katika maandiko? Nini tunajifunza kutoka kwa mifano hii?

Luka 1:26–38

“Hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.”

  • Washiriki wa darasa wanaweza wakati mwingine kushangaa—kama Mariamu alivyofanya—jinsi mipango ya Mungu kwa ajili yao au ahadi kwa ajili yao zinaweza kutimizwa. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa kwamba kupitia uwezo wa Mungu vitu vyote vinawezekana, unaweza kuonyesha picha Upashaji Habari: Malaika Gabrieli Anamtokea Mariamu (Kitabu cha Sanaa ya Injili, no. 28) na waalike wasome pamoja Luka 1:26–38. Ni nini tunaweza kujifunza kuhusu kushinda vinavyoonekana haviwezekani kwa kujifunza maneno na vitendo vya Mariamu? Waombe washiriki wa darasa kushiriki uzoefu ambao Mungu aliwasaidia kukitimiza kitu walichofikiria kilikuwa hakiwezekani. Kwa mifano ya kisasa ya Watakatifu ambao kwa msaada wa Mungu walitimiza kitu fulani ambacho kilionekana hakiwezekani, angalia video “Kuunganishwa Pamoja: “The Manaus Temple Caravan” (LDS.org).

  • Maisha ya Mwokozi yalionyesha ukweli ambao Gabriel alitangaza: “Hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.” (Luka 1:37). Kuelezea kanuni hii, unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kufikiria nyakati ambazo Mwokozi alitimiza kilichoonekana kitu kisichowezekana wakati anapotenda mapenzi ya Baba Yake (ona, kwa mfano, Yohana 9:1–7). Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuona jinsi kanuni hii inavyofanya kazi katika maisha yao, unaweza kuwaalika watafakari maswali kama yafuatayo: Ni tofauti gani inayoleta katika maisha yako kujua kwamba hakuna kisichowezekana kwa Mungu? Inabadilisha namna gani jinsi unavyohudumu katika Kanisa? Jinsi unavyoingiliana na familia yako? Inaweza pia kusaidia kufananisha Luka 1:37 na maneno ya Mwokozi katika Marko 14:36.

Mathayo 1:18–25; Luka 1:26–55

Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.

  • Kusudi kuu la Mathayo, Luka, na wale waandishi wengine wa Injili lilikuwa kushuhudia kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu. Unaweza kuwasidia vipi washiriki wa darasa kutambua kusudi hili katika sura za mwanzo kabisa watakazosoma katika Agano Jipya? Hapa kuna wazo moja: Gawa darasa katika vikundi au majozi, na lipe kila kundi seti ya aya kutoka Mathayo 1 au Luka 1. Waalike watafute matukio au maneno ambayo yanaimarisha imani yao katika ujumbe wa Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu na kisha washiriki na darasa kile wanachokipata. Baadhi ya vifungu ambavyo unaweza kupendekeza inajumuisha Mathayo 1:18–25 na Luka 1:26–38, 39–45, 46–55. Pendekeza kwa darasa kwamba linapojifunza Agano Jipya mwaka huu, linaweza kuweka orodha ya vifungu ambavyo vinashuhudia kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu. Mnaweza hata kuweka orodha hii kama darasa.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Kuwahimiza washiriki wa darasa kusoma Mathayo 2 na Luka 2 kwa ajili ya darasa la wiki ijayo, unaweza kupendekeza kwamba kama watasoma tukio la kuzaliwa kwa Mwokozi kwa maombi, watapata umaizi mpya, hata kama wameishaisoma mara nyingi kabla.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Mathayo 1; Luka 1

Msubirie Bwana.

Mzee Neal A. Maxwell alifundisha, “Imani … inajumuisha imani katika mpangilio wa Mungu, kwani ameshasema, ‘Vitu vyote lazima vipite katika muda wake.’ (M&M 64:32.)” (“Ili Msiwe Mlio Choka na Kudhoofu Katika Akili Zenu.” Ensign 1991 90).

Rais Dieter F. Uchtdorf alifundisha:

“Kila mmoja wetu ameamriwa kungoja katika njia yake mwenyewe. Tunangojea majibu kwa maombi. Tunangojea vitu ambavyo kwa wakati ule vinaweza kuonekana ni sahihi kabisa na vizuri sana kwetu hivyo hatuwezi labda kufikiria kwa nini Baba wa Mbinguni angechelewesha jibu.

“Nakumbuka wakati nilipokuwa nikijiandaa kufunzwa kuwa rubani wa ndege ya kivita. Tulitumia wakati mwingi wa mafunzo yetu tangulizi ya kijeshi kwa mazoezi ya kimwili. Tulikimbia na tukakimbia na tukakimbia sana zaidi.

“Na nilipokuwa nikikimbia nilianza kuona kitu ambacho, kwa hakika, kilinisumbua. Tena na tena nilikuwa nikipitwa na wanaume ambao walikuwa wanavuta sigara, wanakunywa pombe, na waliokuwa wanafanya mambo yote yaliyo kinyume na injili, na, hasa, Neno la Hekima.

“Nakumbuka kufikiria , ‘Ngoja kidogo! Mimi si ninafaa kuweza kukimbia na nisichoke?’ Lakini mimi nilikuwa nikichoka, na kupitwa na watu ambao bila shaka walikuwa hawafuatii Neno la Hekima. Nakiri, ilinisumbua mimi wakati huo. Nikajiuliza, hii ahadi ilikuwa ni kweli au la?”

“Jibu halikuja mara moja. Lakini hatimaye nilijifunza kwamba ahadi za Mungu daima hazitatimizwa mara moja au katika njia tunayotarajia; zinakuja kulingana na wakati Wake na katika njia Yake. Miaka mingi baadaye, niliweza kuona wazi ushahidi wa baraka za muda ambazo uja kwa wale wanaotii Neno la Hekima—kama ziada kwa baraka za kiroho ambazo huja mara moja kutokana na utiifu wa sheria yoyote ya Mungu.” (“Endelea katika Subira.” Ensign au Liahona, Mei 2010 58).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wahimize washiriki wa darasa kujifunza maandiko nyumbani. Njia moja unaweza kuhimiza kujifunza maandiko nyumbani ni kutoa muda kwa washiriki wa darasa kushiriki uvumbuzi na umaizi kutoka kwa kujifunza kwao binafsi na familia. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi. 29.)

Chapisha