Njoo, Unifuate
Desemba 31–Januari 6. Tunawajibikia Elimu Yetu Wenyewe.


Desemba 31–Januari 6. Tunawajibikia Elimu Yetu Wenyewe,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2019 (2019.)

Desemba 31–Januari 6. Tunawajibikia Elimu Yetu Wenyewe. “ Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2019

Picha
familia ikitazama alibamu ya picha

Desemba 31–Januari 6

Tunawajibikia Elimu Yetu Wenyewe.

Unaposoma na kutafakari vifungu vya maandiko katika muhtasari huu, andika misukumo ya kiroho unayopokea. Hii itamwalika Roho katika maandalizi yako. Njoo Unifuate—Kwa Watu Binafsi na Familia na mawazo yafuatayo yanaweza kukusaidia kuwapa mwongozo watu katika darasa lako kujifunza Agano Jipya mwaka huu.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Himiza Kushiriki

Mojawapo ya malengo yako kama mwalimu ni kuwahimiza washiriki wa darasa kujifunza kutoka kwa maandiko wao wenyewe na pamoja na familia zao. Kusikiliza uzoefu wa wengine kunaweza kuwapa mwongozo wengine kutafuta uzoefu wao wenyewe. Kwa hiyo, mwanzoni mwa kila darasa, waombe washiriki wa darasa kushiriki maandiko kutoka kwenye kujifunza kwao ambayo yaliwapa mwongozo au yaliwavutia.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Kujifunza kikweli kutoka kwa Mwokozi, lazima tukubali mwaliko Wake, “Njoo, unifuate.”

  • Kujifunza Agano jipya ni nafasi sio tu kujifunza kuhusu Mwokozi na mafundisho Yake lakini pia kugundua jinsi ya kumfuata Yeye kikamilifu zaidi. Matukio katika Matayo 19:16–22 ni njia nzuri ya kutambulisha dhamira hii (ona pia video “Kristo na Kijana Tajiri Mtawala” kwenye LDS.org), Unaweza kuwaomba washiriki wa darasa kupekua matukio haya wakitafuta kitu wanachojifunza kuhusu kuwa mfuasi wa Yesu Kristo na kushiriki kile wanachokipata. Kwa wazo la shughuli ingine linalohusisha kanuni hii, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Watu Binafsi na Familia.

Kujifunza kunahitaji kutenda kwa imani.

  • Ni kwa jinsi gani unaweza kuwapa mwongozo washiriki wa darasa kuchukua majukumu zaidi ya utendaji katika kujifunza kwao, badala ya kuweka wajibu pekee kwa mwalimu? Hapa kuna wazo. Mwalike mshiriki wa darasa akutupie kitu laini, wakati hufanyi jitihada yoyote ya kukidaka. Tumia shughuli hii kuanzisha majadiliano kuhusu wajibu wa wanafunzi na walimu katika kujifunza injili. Kauli ya Mzee David A. Bednar kuhusu kujifunza kwa imani, inayopatikana katika “Nyenzo za Ziada,” inaweza kusaidia katika majadiliano haya.

  • Kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa kwamba kujifunza injili kunahitaji imani kufanya kazi, unaweza kuwagawa katika makundi na kualika kila kikundi kisome mojawapo ya matukio yafuatayo: Marko 5:25–34; Luka 5:17–26; na Yohana 9:1–7. Watu walifanya nini katika kila tukio kuonyesha imani yao katika Mwokozi? Ni vitendo gani tunaweza kuchukua ili kujifunza injili na kuonyesha imani yetu kwamba Bwana atatusaidia sisi kujifunza ukweli?

  • Washiriki darasa wote wana wajibu wa kumwalika Roho katika darasa. Kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa hili, waambie wasome Alma 1:26 na Mafundisho na Maagano 50:13–22; 88:122–23 na kushiriki kile mwalimu na wanafunzi wanaweza kufanya kumwalika Roho. Inaweza kusaidia kuandika majibu yao ubaoni chini ya vichwa vya habari kama hivi: Nini mwalimu anaweza kufanya na Nini wanafunzi wanaweza kufanya. Inaweza kusaidia kutengeneza bango lenye majibu ya washiriki wa darasa ambalo lingeweza kuonyeshwa wiki chache zinazofuata?

Tunahitaji kujua ukweli kwa ajili yetu wenyewe.

  • Vifungu vingi katika Agano Jipya vinafundisha kanuni ambazo zinaweza kuongoza uchunguzi wetu wa imani. Mifano inajumuisha Luka 11:9–13; Yohana 5:39; 7:14–17; na 1 Wakorintho 2:9–11. Unaweza kuwaalika washiriki wa darasa lako wanaosoma vifungu hivi katika kujifunza kwao binafsi kushiriki kile walichojifunza. Au mnaweza kusoma vifungu hivi kama darasa na kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki jinsi walivyopata ushuhuda wao.

    Picha
    wavulana na wasichana katika darasa

    Kutafuta kujifunza kwa imani kutatusaidia kupata ushuhuda wetu wenyewe.

  • Haijalishi ni muda gani tumekuwa katika Kanisa, sisi wote tunahitaji daima kuimarisha shuhuda zetu. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kutambua ukweli ambao wanahitaji kujua wao wenyewe, unaweza kuandika kwenye vipande vya karatasi marejeo ambayo yanafundisha kweli muhimu, kama vile Yohana 3:16–17; 1 Wakorintho 15:22; Mosia 3:13; Alma7:11–13; na Mafundisho na Maagano 135:3. Waombe washiriki wa darasa wasome maandiko haya, wafanye muhtasari wa kweli za milele wanazopata, na wajadili kile wanaweza kufanya kupata ushuhuda wake. Kufanya shughuli hii kuwa yenye kushirikisha zaidi kwa vijana, fikiria kuficha vipande vya karatasi kote chumbani na waalike vijana “watafute ukweli.”

  • Matendo ya Mitume 17:10–12 inaelezea Watakatifu walipekua maandiko na kupata ushahidi wa ukweli wao wenyewe. Kuwahimiza washiriki wa darasa kufuata mfano wao, someni aya hizi pamoja na waalike washiriki wa darasa kushiriki vifungu vya maandiko ambavyo vimeimarisha ushuhuda wao wa injili.

Tunawezaje kufanya kujifunza maandiko kwetu kuwa na maana zaidi?

  • Kujenga tabia ya kujifunza maandiko inaweza kuwa changamoto kwa washiriki wa darasa wanaohisi kwamba hawana muda unaohitajika, uelewa, au ujuzi. Unaweza kufanya nini kuwasaidia waweze kufanikiwa? Unaweza kuanza kwa kujadili hadithi kuhusu wakataji miti katika “Nyenzo za Ziada.” Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kupata kujiamini kujifunza maandiko, unaweza kushiriki taarifa kutoka “Mawazo ya kuendeleza Mafunzo Yako Binafsi ya Maandiko katika Njoo, Unifuate—Kwa Watu Binafsi na Familia. Labda wewe au washiriki wengine wa darasa mngeshiriki uzoefu wa kutumia baadhi ya mawazo haya au uzoefu mwingine wa maana wa kujifunza maandiko. Mnaweza pia kuchagua sura katika Agano Jipya na kujaribu kujifunza kama darasa mkitumia baadhi ya mawazo haya.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Kuwahimiza washiriki wa darasa kujifunza Mathayo 1 na Luka 1 nyumbani katika maandalizi kwa majadiliano ya wiki inayofuata, unaweza kuuliza swali hili: “Umewahi kuombwa kufanya kitu ambacho kilionekana hakiwezekani?” Sura hizi zinaonyesha ukweli kwamba “hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu” (Luka 1:37).

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Kudai elimu ya kiroho kwa ajili yetu wenyewe.

Mzee David A. Bednar alielezea: “Nimechunguza tabia ya kawaida ya wote miongoni mwa walimu walioweza kuwa na ushawishi mkubwa katika maisha yangu. Wamenisaidia kutafuta kujifunza kwa imani. Walikataa kunipa majibu rahisi kwa maswali magumu. Kwa hivyo, hawakunipa majibu kabisa. Badala yake, walionyesha njia na walinisaidia kuchukua hatua kupata majibu yangu mwenyewe. … Jibu lililotolewa na mtu mwingine kwa kawaida halikumbukwi kwa muda mrefu, kama litakumbukwa kabisa. Lakini jibu tunalogundua au kupata kupitia matumizi ya imani, kwa kawaida, linabakizwa kwa maisha yote. … Kwa njia hii tu mtu anaweza kwenda mbele akitegemea elimu ya kiroho na uzoefu wa wengine na kudai baraka hizo kwa ajili yake mwenyewe” (“Tafuta Kujifunza kwa Imani.” Ensign, Sept. 2007, 67).

Kutenga muda kwa kujifunza maandiko.

Ndugu Tad R. Callister alifundisha:

“Wakataji miti wawili … walifanya mashindano kuamua nani angeweza kuangusha miti zaidi kwa siku moja. Wakati wa mapambazuko mashindano yalianza. Kila saa mwanaume mdogo alizurura katika msitu kwa dakika 10 au zaidi. Kila wakati alipofanya hivi, mpinzani wake alitabasamu na aliashiria kwa kichwa, akihakikisha kwamba alikuwa anaendelea mbele. Mwanaume mkubwa kamwe hakuondoka kwenye kituo chake, kamwe hakuacha kukata, kamwe hakupumzika.

“Siku ilipokwisha, mwanaume mkubwa alishituka kujua kwamba mpinzani wake, aliyeonekana alipoteza muda mwingi, alikuwa amekata miti mingi zaidi kuliko yeye. ‘Ulifanya vipi wakati ulipumzika mara nyingi?’ aliuliza.

“Mshindi alijibu, ‘Oh, nilikuwa nanoa shoka langu.’

“Kila wakati tunapojifunza maandiko, tunanoa mashoka yetu ya kiroho”(“Furaha ya Kujifunza.” Ensign, Oct 2016 14).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Zingatia mafundisho. Hakikisha kwamba majadiliano ya darasani yanabaki eneo la maandiko na mafundisho ya manabii. Unaweza kufanya hilo kwa kuuliza maswali kama haya: “Ni kweli gani za injili tunazojifunza kutoka maoni tuliyoyasikia?” au “Kuna yoyote anayeweza kushiriki maandiko ambayo yanahusisiana na kile tulichojadili?” (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 20–21.)

Chapisha