Njoo, Unifuate
Septemba 16–22. 2 Wakorintho 8–13: ‘Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu’


“Septemba 16–22. 2 Wakorintho 8-13: ‘Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2019 (2019)

Mathayo 16-22; Marko 2; Luka 8; -13 Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2019

Picha
Yesu akiongea na mtoto mdogo

Septemba 16–22

2 Wakorintho 8–13

“Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu”

Wakati unasoma 2 Wakorintho 8-13, fikiria kuhusu watu unaowafundisha na panga shughuli ambazo zingewasaidia kugundua kanuni katika sura hizi. Kisha rejea muhtasari huu kwa ziada ya mawazo.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Hapa kuna njia mojawapo ya kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki na wengine walichojifunza kutoka 2 Wakorintho 88–13. Waombe wachache kati yao kuandika ubaoni kirai wakipendacho kutoka katika usomaji wao, na waombe waliobaki kukitafuta katika maandiko. Waalike washiriki wa darasa kuelezea ni kwa nini virai hivi ni vya muhimu kwao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

2 Wakorintho 8:1–15; 9:6–15

Watakatifu kwa ukarimu hushiriki na wengine vile walivyonavyo ili kuwabariki masikini na wenye shida.

  • Mungu amewaamuru Watakatifu Wake kusaidia kuwatunza wale wenye shida, na mistari katika 2 Wakorintho 8–9 inaweza kuwahamasisha washiriki wa darasa lako katika juhudi zao. Ili kuwasaidia kupata mistari hii ungeweza kuandika kwenye ubao maswali kama Kwa nini tunatoa? na Kwa namna ipi tunatakiwa kutoa? Nusu moja ya darasa wangeweza kutafuta majibu kutoka 2 Wakorintho 8:1–15, na nusu nyingine wangeweza kutafuta kutoka 2 Wakorintho 9:6–15. (Ungeweza kuelezea kwamba katika sura ya 8, mstari wa 1–5, Paulo aliongea kuhusu Watakatifu wa Makedonia kama mfano wa watoaji kwa ukarimu.) Je, ni kwa namna gani kanuni zilizofundishwa na Paulo hutusaidia kuwatunza vyema zaidi walio masikini na wenye shida?

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa vyema njia ya Bwana ya kutimiza mahitaji ya kimwili ya Watakatifu wake, kuna nyenzo nyingi zimeorodheshwa katika “Nyenzo za Ziada.” Labda ungewapa kazi washiriki wachache wa darasa kurejea moja kati ya nyenzo hizi na kuelezea kile ambacho kinawavutia. Je, washiriki wa darasa wanaweza kupata mawazo kutoka 2 Wakorintho 8:1–15; 9:6–15 kuonyesha kwamba Watakatifu wa nyakati za Paulo waliwatunza walio masikini katika njia sawa na tufanyavyo leo?

2 Wakorintho 11:13–33

Manabii wa uongo hutafuta kudanganya.

  • Kwa sababu sisi kama Watakatifu wa Korintho, tunaathiriwa kiurahisi na mafundisho ya uongo, tunaweza kunufaika kwa kurejea maonyo ya Paulo kwa Wakorintho kuhusu “manabii wa uongo.” Washiriki wa darasa wanaweza kupata mifano ya mafundisho ya uongo ambayo yanatuathiri hivi leo katika ujumbe wa Mzee Quentin L. Cook “Imara katika ushuhuda wa Yesu” (Ensign au Liahona, Nov. 2016, 40–43). Labda ungempa kazi mmoja wao kusoma ujumbe huu kabla na kushiriki na darasa kile ambacho ujumbe huu unafundisha kuhusu jinsi gani tunaweza kuepuka “vizuizi” ambavyo hutupeleka mbali na injili. Ni mafundisho gani ambayo ni ya kawaida ulimwenguni leo yanayoweza kutupeleka mbali na injili? Unaweza kuwauliza washiriki wa darasa kurejea 2 Wakorintho 11: 21–33 na kushiriki walichojifunza kutoka mistari hii kuhusu “watumishi wa kweli wa Kristo.”

2 Wakorintho 11:3; 13:5–8

Tunapaswa “kuhoji” uaminifu wetu katika injili ya Yesu Kristo.

  • Wakati mwingine waumini wa Kanisa wanahisi kuzidiwa na mahitaji ya kimaisha—ikijumuisha kile ambacho wangeweza kukiona kama mahitaji ya kuwa Mtakatifu wa Siku za Mwisho. Ushauri wa Paulo wa “kujihoji sisi wenyewe, kama tuko kwenye imani” unaweza kukusaidia wewe pamoja na darasa lako kuzingatia katika “urahisi ulioko katika Kristo” (2 Wakorintho 13: 5; 11:3). Labda mngeweza kusoma pamoja 2 Wakorintho 11:3 na kujadili nini kirai “urahisi ulioko katika Kristo” kinaweza kumaanisha. Ungeweza pia kuwauliza washiriki wa darasa kupiga taswira kuwa wameitwa kuandika maelezo ya injili ya Yesu Kristo katika gazeti, kwa kikomo cha maneno 100. Wape muda kuandika maelezo yao, na waache washiriki walichokiandika. Kama wanahitaji msaada, wanaweza kurejea Yohana 3:16–17; 3 Nefi 27:13–21; na Kweli kwa Injili, 76. Waalike washiriki wa darasa kutafakari kama wanaishi kikweli kanuni muhimu za injili.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa “kuhoji” jinsi gani wanaweza kurahisisha maisha yao kuwa wafuasi wazuri zaidi, ungeweza kushiriki pamoja nao kauli ya Rais Dieter F. Uchtdorf katika “Nyenzo za Ziada.” Washiriki wa darasa wangeweza kujadili jinsi gani wanaweza kuufanyia kazi mwaliko wa Rais Uchtdorf wa “kuzingatia kwenye mafundisho ya msingi, kanuni na matumizi ya injili.” Je, ni mawazo gani mengine washiriki wa darasa wanayo kuhusu jinsi gani tunaweza kujihoji wenyewe ili kuhakikisha kuwa tunabaki wakweli katika imani?

2 Wakorintho 12:5–10

Neema ya Kristo inatosha kutusaidia kupata nguvu katika udhaifu wetu.

  • Ungeweza kusema nini kwa rafiki yako ambaye amesali kwa ajili ya kupata nafuu kutokana na udhaifu wa kimwili lakini anahisi sala hii haijibiwi? Fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kutafakari swali hili wanaposoma kimoyo moyo 2 Wakorintho 12:5–10. Kisha wangeweza kuelezea umaizi wao kutoka kwenye mistari hii ambao ungeweza kusaidia katika hali kama hii. Wangeweza pia kushiriki na wengine uzoefu ambapo, kwa njia ya neema ya Yesu Kristo, walipata nguvu katika udhaifu wao. Je, ni kwa namna gani jambo hilo linaathiri maisha yao?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Ili kuwahimiza washiriki wa darasa kuendelea kusoma Wagalatia, ungeweza kuwauliza kama wanamjua mtu yoyote ambaye amejitenga mbali na injili. Kama ndivyo, wangetaka kusoma jinsi Paulo alivyowaalika Wagalatia ambao walikuwa wamejitenga mbali na injili kurudi tena.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

2 Wakorintho 8–13

Njia ya Bwana ya kutoa mahitaji kwa maskini na wenye shida.

Tunaweza kurahisisha njia yetu ya kuishi injili.

Rais Dieter F. Uchtdorf alifundisha:

“Akina kaka na akina dada, kuishi injili hakuhitaji kuwe changamani.

Ni dhahiri hasa. Ingeweza kuelezeka hivi:

  • “Kulisikia neno la Mungu kwa umakini kunatuongoza sisi katika kumwamini Mungu na kuamini ahadi Zake.

  • “Kadiri tunavyomwamini Mungu, ndivyo mioyo yetu inavyojawa na upendo Kwake na kwa kila mmoja wetu.

  • “Kwa sababu ya upendo wetu kwa Mungu, tunatamani kumfuata Yeye na kutenda mambo yanayoendana na neno Lake.

  • “Kwa sababu tunampenda Mungu, tunataka kumtumikia Yeye na kufikia kubariki maisha ya wengine na kuwasaidia maskini na wenye mahitaji.

  • “Kadiri tunavyotembea katika njia hii ya ufuasi, ndivyo tunavyojifunza neno la Mungu.

“Na ndivyo iendavyo, kila hatua inatuongoza kwenye hatua nyingine na kutujaza ongezeko la milele la imani, tumaini na hisani.

“Ni rahisi sana, na inafanya kazi vizuri sana.

“Kaka zangu na dada zangu, kama uliwahi kufikiria kwamba injili haifanyi kazi vizuri kwako, ninakuomba rudi nyuma, yaangalie maisha yako, na rahisisha mwenendo wako wa ufuasi. Zingatia katika mafundisho ya msingi, kanuni, na matumizi ya injili. Ninawaahidi kwamba Mungu atawaongoza na kuwabariki katika njia zenu za maisha ya kuridhisha, na injili itafanya kazi vizuri kwenu” (Inafanya kazi vizuri sana ,” Ensign au Liahona, Nov. 2015, 22).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fanya kazi pamoja na wana familia. “Watu ambao wana ushawishi mkubwa kwa mtu binafsi—kwa wema au ubaya—kawaida ni wale walio wa nyumbani mwake. Kwa sababu nyumbani ni mahali muhimu pa kujifunza na kuishi injili, juhudi zako za kumuimarisha mshiriki wa darasa zitakuwa za ufanisi zaidi wakati unaposhirikiana na … wanafamilia” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 8).

Chapisha