Njoo, Unifuate
Septemba 23–29 Wagalatia: ‘Tembea katika Roho’


Septemba 23–29 Wagalatia: ‘Tembea katika Roho’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2019 (2019)

Septemba 23–29 Wagalatia,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2019

Picha
Kristo anamtokea Paulo gerezani

Septemba 23–29

Wagalatia

“Tembea katika Roho”

Kwa maombi unaposoma na kutafakari Wagalatia, Bwana atakufundisha kile unachohitaji kushiriki na darasa lako. Kuandika misukumo yako kunaonyesha shukrani kwa Mungu kwa msaada Wake (ona Paul B. Pieper, “To Hold Sacred,” Ensign au Liahona, Mei 2012, 109).

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kujifunza maandiko mara nyingi hutupeleka kwenye mjadala wa injili wenye kuleta maana na wana familia au marafiki. Je, hii ilitokea kwa washiriki wa darasa lako wiki hii? Waalike kuelezea uzoefu wao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Wagalatia 1:6–7; 3:1–5; 4:8–21; 5:1, 13–14

Injili ya Yesu Kristo hutoa uhuru.

  • Kujifunza kitabu cho chote cha maandiko ni rahisi zaidi pale tunapojua kwa nini kiliandikwa. Kwa sababu hii, ingeweza kuwa vizuri kuanza mjadala kuhusu Wagalatia kwa swali kama “Je, unadhani dhumuni la Paulo lilikuwa nini katika kuandika waraka huu?” au “Ni tatizo gani Paulo alikuwa akijaribu kutatua” Alika washiriki wa darasa kutafuta viashiria vya jibu katika Wagalatia 1:6–7; 3:1–5; 4:8–21. Je, ni kwa namna gani ujumbe wa Paulo unatuhusu sisi leo?

  • Baadhi ya Watakatifu wa Galatia walidhani bado walihitajika kuishi sheria ya Musa. Kwa Paulo, hii ilikuwa kama kuishi na “nira ya utumwa” ikilinganisha na uhuru uliotolewa katika sheria ya Kristo (Wagalatia 5:1). Wakati kwa kawaida hatukabiliwi na tatizo kama hili leo, sote tunakabiliwa na uchaguzi sawa na huo kati ya kifungo cha kiroho na uhuru kupitia Yesu Kristo. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa lako kuchunguza mafundisho ya Paulo kuhusu uhuru na kifungo, ungeweza kuwaomba kuorodhesha mitazamo na matendo ambayo yanaweza kutupeleka kwenye kifungo cha kiroho (kama vile desturi za kitamaduni, tabia mbaya, imani potofu, au kuzingatia kwenye matendo ya nje kuliko uongofu wa ndani). Kulingana na Wagalatia 5:1, 13–14, tunapataje uhuru kutoka kifungo cha kiroho? Je, ni kwa namna gani washiriki wa darasa wameonja uhuru ulioahidiwa katika injili ya Kristo? Ungeweza pia kuwaalika washiriki wa darasa kuelezea ni kwa namna gani wangeweza kumjibu mtu ambaye anahisi kwamba kuishi injili kunazuia uhuru binafsi

Wagalatia 5:16–26

Kama “tutatembea katika Roho,” tutapokea “tunda la Roho.”

  • Watu wengi wana changamoto ya kutambua ushawishi wa Roho. Wagalatia 5 inaweza kuwasaidia washiriki wa darasa lako kutambua tunda la Roho. Labda ungeweza kuanza kwa kuwataka kutafuta kutoka Wagalatia 5:22–25 ili kupata maneno aliyoyatumia Paulo kuelezea tunda la Roho. Ni kwa nini tunda ni mfano mzuri kuelezea jinsi Roho anavyotushawishi sisi? Labda washiriki wa darasa wangeweza kuelezea ni kwa namna gani tunda hili limekuwa la dhahiri katika maisha yao au maisha ya watu wanaowajua. Baadhi ya nyenzo nyingine za kuchunguza hujumuisha Mathayo 7:16–18; Yohana 14:26–27; Moroni 7:13–17; Mafundisho na Maagano 11:12–13; na kauli kutoka kwa Rais Gordon B. Hinckley katika “Nyenzo za Ziada.”

    Picha
    Tufaha katika mti

    Tunaweza kupokea “tunda la Roho” tunapolitafuta.

  • Wakati mwingine tunaweza kujifunza kuhusu kanuni kwa kujifunza kile ambacho ni kinyume chake. Kwa mfano, katika Wagalatia 5:16–26, Paulo alitofautisha “kazi za mwili” na “tunda la Roho.” Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kutafakari ni kwa kiasi gani wanatembea katika roho, ungeweza kupendekeza kwamba wasome Wagalatia 5:16–26 na kisha watengeneze tathmini binafsi sawa na Shughuli ya Sifa katika ukurasa namba 126 wa Hubiri Injili Yangu. Kwa mfano, kwa kila kitu kilichoorodheshwa katika mstari wa 19–23, wangeweza kuandika swali kama vile “Je, ninawaonea husuda rafiki zangu?” Au “Je nina hisi upendo kila siku?” Majibu ya washiriki wa darasa katika kujitathmini kwao binafsi yasitolewe hadharani, lakini unaweza kuwaalika kushiriki dhana au mawazo ili kumsaidia kila mmoja wao “kutembea katika Roho.” Kama huna muda kumaliza shughuli hii darasani, unaweza kupendekeza kwamba washiriki wa darasa wakaimalizie nyumbani.

Wagalatia 6:7–10

Tunapopanda “katika roho,” tutavuna baraka kwa wakati wake.

  • Kujifunza Wagalatia 6:7–10 kunaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kufikiri zaidi kiundani kuhusu matokeo ya muda mrefu ya chaguzi zao. Ili kuwasaidia, ungeweza kuleta mbegu za aina tofauti tofauti, pamoja na mimea, matunda au mboga za majani zinazokua kutoka kwenye kila mbegu hizi (au ungeweza kuleta picha za vitu hivi). Washiriki wa darasa wangeweza kufanya kazi kwa pamoja kuhusisha kila mbegu na kile inachozalisha. Kisha wangeweza kusoma mstari wa 7–10 na kuzungumza kuhusu maana ya “kupanda katika mwili” na “kupanda katika Roho” (Ujumbe kutoka kwa Mzee Ulisses Soares katika “Nyenzo za Ziada” ungeweza kusaidia.) Je, tunavuna nini tunapopanda katika mwili? Je, tunavuna nini tunapopanda katika Roho? (ona Wagalatia 5:22–23). Fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kutafakari baraka za kiroho wanazotumaini kupokea. Je, ni “kupanda kupi” wanakoweza kufanya sasa ili kujiandaa kupokea baraka hizo? Ungeweza hata kuwaalika waandike mawazo yao na, kama wanaona ni vyema, wayashiriki.

  • Baadhi ya washiriki wa darasa wanaweza kuhisi “kuchoka katika kutenda mema” (Wagalatia 6:9)—labda kwa sababu hawana uhakika kwamba jitihada zao zinazaa matunda. Mjadala wa Wagalatia 6:7–10 ungeweza kusaidia. Ili kutambulisha mistari hii, ungeweza kumwalika mtu fulani katika darasa kuzungumza kwa ufupi kuhusu wakati ambapo alihitaji uvumilivu wakati alipokuwa akijaribu kupanda kitu. Je, uzoefu wa mtu huyu, pamoja na Wagalatia 6:7–10, ungeweza kutufundisha nini kuhusu jitihada zetu za “kutembea katika Roho”? (WagalatiaWagalatia 5:25).

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Ili kuwahimiza washiriki wa darasa lako kusoma waraka wa Paulo kwa Waefeso, ungeweza kuwaambia kwamba katika waraka huu watajifunza namna wanavyoweza “kuzipinga hila za shetani” (Waefeso 6:11).

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Wagalatia

Matunda ya kuishi injili.

Rais Gordon B. Hinckley alifundisha; “Tunawezaje kujua mambo ya Roho? Tutajuaje kama yanatoka kwa Mungu? Kwa matunda yake. Kama yanaelekeza kwenye ukuaji, na maendeleo kama yanaelekeza kwenye imani na ushuhuda, kama yanaelekeza kwenye njia bora ya kufanya mambo, kama yanaelekeza kwenye uchamungu, basi yanatoka kwa Mungu. Kama yanatuvuta chini, kama yanatuleta kwenye giza, kama yanatukanganya, na kututia wasiwasi, kama yanaelekeza kwenye kutokuwa na imani, basi hayo ni ya shetani.

Katika tukio jingine, Rais Hinckley alisema: Unatambua ushawishi wa Roho kupitia matunda ya Roho—kile ambacho huangaza, kile ambacho hujenga, kile ambacho ni chanya na cha uhakika na cha kuinua na kutuongoza katika maneno na mawazo mazuri zaidi na matendo mazuri zaidi ni kutoka kwa Roho wa Mungu. Kile ambacho hubomoa, ambacho hutuongoza katika njia zilizokatazwa—ni cha adui. Nafikiri ni dhahiri kiasi hicho, rahisi kiasi hicho (Teachings of Presidents of the Church: Gordon B. Hinckley [2016], 121).

Kupanda katika Roho.

Mzee Ulisses Soares alifafafanua: “Kupanda katika Roho humaanisha kwamba mawazo yetu yote, maneno na matendo lazima yaituinue katika hali ya utakatifu wa wazazi wetu wa mbinguni. Hata hivyo, maandiko yanauzungumzia mwili kama wenye asili ya kufa au wenye uovu wa mwanadamu wa asili, ambao huwaruhusu watu kuathiriwa na matamanio, hamu na mihemko ya mwili badala ya kuangalia ushawishi kutoka kwa Roho Mtakatifu. Kama hatuko makini, vishawishi hivyo pamoja na shinikizo la uovu katika ulimwengu vinaweza kutusababishia kukubali tabia ovu na zisizokuwa na mpangilio ambazo zinaweza kuwa sehemu ya sifa yetu” (“Kaeni katika Himaya ya Bwana!” Ensign au Liahona, Mei 2012, 39).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie wanafunzi ili wainuane “Kila mtu katika darasa lako ni chanzo kikubwa cha ushuhuda, utambuzi, na uzoefu kutokana na kuishi injili. Waalike kushiriki wao kwa wao na kuinuana” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 5).

Chapisha