Njoo, Unifuate
Septemba 9–15 2 Wakorintho 1–7: ‘Na Mpatanishwe na Mungu’


“Septemba 9–15. 2 Wakorintho 1–7: ‘Na Mpatanishwe na Mungu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2019 (2019)

“Septemba 9–15 . 2 Wakorintho 1–7 Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2019

Picha
Yesu Kristo

Septemba 9–15

2 Wakorintho 1–7

“Na Mpatanishwe na Mungu”

Unaposoma 2 Wakorintho 1–7 wiki hii, fikiria kuhusu washiriki maalum wa darasa lako—wale ambao wanakuja darasani na wale ambao hawaji. Ni kwa namna gani kanuni za sura hizi zitawabariki?

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Toa muda kwa washiriki wa darasa kutoa mawazo ambayo hufanya usomaji wao wa maandiko kuwa wa maana zaidi.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

2 Wakorintho 1:3–7; 4:6–10, 17–18; 7:4–7

Majaribu yetu yanaweza kuwa baraka.

  • Labda kuna mtu kwenye darasa lako anapitia jaribu gumu. Matukio ambayo Paulo ameyaeleza na ushauri aliotoa katika 2 Wakorintho unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kufikiria kuhusu baraka ambazo zinaweza kuja kutokana na majaribu yao. Kwa kuanza mjadala, unaweza kumuomba mshiriki wa darasa kuja akiwa amejiandaa kuzungumza kuhusu ni kwa namna gani jaribu lilibariki maisha yake au nini alijifunza kutoka kwa mtu fulani aliyestahimili jaribu. Kisha unaweza kuwapa washiriki wa darasa dakika chache kurejea 2 Wakorintho 1:3–7; 4:6–10, 17–18; na 7:4–7, wakiangalia Paulo alifundisha nini kuhusu madhumuni na baraka za majaribu. (Kwa mifano ya mafundisho yake, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya watu Binafsi na Familia.) Waombe washiriki wa darasa kuelezea kile wanachojifunza. Ungeweza kupendekeza kwamba wasome kwa sauti mistari ambayo kwayo wanapata fundisho maalum na kisha waelezee tukio au ushuhuda unaohusiana na fundisho hilo.

  • Fikiria kuwapa washiriki wa darasa muda wa kutafakari ni kwa namna gani majaribu yanaweza kubariki maisha yetu, ikijumuisha kurejea kwenye mafundisho ya Paulo yanayopatikana katika 2 Wakorintho 1:3–7; 4:6–10, 17–18; na 7:4–7. Kwa muda huu wangeweza kuandika ni kwa namna gani mafundisho ya Paulo yangeweza kutumika katika majaribu wanayokabiliana nayo

  • Kwa kuongezea katika mjadala wenu, fikiria kuimba kwa pamoja wimbo unaopendwa wa washiriki wa darasa ambao unashuhudia kuhusu faraja na baraka Baba yetu wa Mbinguni na Mwokozi wanatupatia katika nyakati za majaribu—kama vile “Msingi Imara” (Wimbo, namba. 85). Baada ya kuimba kwa pamoja, unaweza kuwakaribisha washiriki wa darasa kuangalia kirai katika 2 Wakorintho 1 na 4 ambacho wanahisi kinaendana na wimbo huo.

2 Wakorintho 2:5–11

Tunapokea baraka na kuwabariki wengine pale tunaposamehe.

  • Wote tuna uzoefu ambapo mtu fulani “alisababisha huzuni” kwetu au katika familia yetu (mstari wa 5). Labda washiriki wa darasa wangeweza kutafuta kutoka katika 2 Wakorintho 2:5–11, wakiangalia ushauri kutoka kwa Paulo kuhusu namna ya kumchukulia mtu ambaye ametukwaza. Fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kurejea Luka 15:11–32; Yohana 8: 1–11; na nukuu kutoka kwa Mzee Kelvin R. Duncan (ona “Nyenzo za Ziada”) kujifunza zaidi kuhusu namna gani tunatakiwa kuwachukulia wale ambao wametenda dhambi. Je, ni kwa nama gani tunajidhuru sisi wenyewe pamoja na wengine pale tunapokuwa hatuko tayari kusamehe?

2 Wakorintho 5:14–21

Kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo, tunaweza kupatanishwa na Mungu.

  • Watu wengi huja Kanisani wakiwa na hamu ya kuhisi wako karibu na Mungu, na mjadala wa 2 Wakorintho 5:14–21 unaweza kuwasaidia. Kwa kuanza, washiriki wa darasa wangeweza kuchunguza maana ya neno kupatanisha labda kwa kuanza kuangalia neno hilo kwenye kamusi. Je, hii inaleta umaizi gani kuhusu kupatanishwa na Mungu? Je, ni umaizi gani wa ziada tunapata kutoka kwenye neno “Upatanisho” katika Kamusi ya Biblia? Ni kwa jinsi gani umaizi huu hutusaidia kuelewa 2 Wakorintho 5:14–21? Unaweza kuwaalika washiriki wa darasa kuelezea hisia zao kuhusu Mwokozi , ambaye Upatanisho wake unafanya iwezekane kwetu sisi kuungana na Mungu tena.

2 Wakorintho 7:8–11

Huzuni kwa jinsi ya mungu hutuongoza kwenye toba.

  • 2 Wakorintho 7:8–11 hutoa maelezo ya msaada kuhusu huzuni kwa jinsi ya mungu na kazi yake katika toba. Je, tunajifunza nini kuhusu huzuni kwa jinsi ya mungu kutoka 2 Wakorintho 7:8–11 na maneno ya Rais Dieter F. Uchtdorf katika “Nyenzo za Ziada”? Kwa nini huzuni kwa jinsi ya mungu ni muhimu katika toba?

  • Unaweza kuhisi msukumo wa kuhimiza majadiliano kwa kina kuhusu toba. Kama ndivyo, unaweza kujaribu kitu kama hiki: Andika ubaoni Toba ni . Waombe washiriki wa darasa kutafuta jinsi ya kumalizia kirai hiki wakitumia mambo wanayojifunza kutoka 2 Wakorintho 7:8–11, pia kutoka kwenye maandiko na nyenzo zingine zinazopatikana katika “Nyenzo za Ziada.” Ni kwa namna gani wangeweza kutumia mafundisho haya ili kumsaidia mtu fulani kuelewa namna ya kutubu kwa dhati?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waulize washiriki wa darasa kama wamewahi kusali ili mateso au jaribu liondoshwe? Katika 2 Wakorintho 8–13, watapata kujua jinsi gani Paulo alijibu baada ya kusali juu ya hili lakini sala yake haikujibiwa kama alivyotarajia.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

2 Wakorintho 1–7

Kuwaona wenzetu kama vile Mungu anavyowaona hutusaidia sisi kusamehe.

Mzee Kevin R. Duncan alifundisha: “Kitu muhimu katika kuwasamehe wengine ni kuwaona wengine kama vile Mungu anavyowaona. Kuna wakati, Mungu anaweza kufungua pazia na kutubariki kwa kipawa cha kuona katika moyo, nafsi, na roho ya mtu mwingine ambaye ametukwaza. Umaizi huu unaweza hata kutuongoza kwenye upendo usio kifani kwa mtu huyo” (“Mafuta ya Uponyaji ya Msamaha,” Ensign au Liahona, Mei 2016, 34).

Huzuni kwa jinsi ya mungu hutoa mwongozo wa kiungu wa badiliko na tumaini.

Rais Dieter F. Uchtdorf alifafanua:

Huzuni kwa jinsi ya mungu hutoa mwongozo wa kiungu wa badiliko na tumaini kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo. Huzuni kwa jinsi ya dunia hutuvuta chini, huzima tumaini, na hutushawishi kushindwa na kuingia katika majaribu zaidi.

Huzuni kwa jinsi ya mungu hutuongoza kwenye uongofu na badiliko la moyo. Hutufanya sisi kuchukia dhambi na kupenda wema. Hutuhimiza kusimama na kutembea katika nuru ya upendo wa Kristo. Toba ya kweli ni kuhusu badiliko, si mateso na maumivu” (“Unaweza Kufanya Hivyo Sasa!” Ensign au Liahona, Nov. 2013, 56).

Toba ni nini?

Mzee Neil L. Andersen alifundisha:

“Tunapotenda dhambi, tunampa Mungu kisogo. Tunapotubu, tunamgeukia Mungu.

“Mwaliko wa kutubu mara chache ni sauti ya kukanya bali ni ombi la kupendeza la kugeuka na ‘ku-rudi’ tena kwa Mungu [ona Helamani 7:17]. Ni wito wa Baba mpendwa na Mwanaye wa Pekee wa kuwa zaidi ya tulivyo, kufikia katika njia ya juu ya maisha, kubadilika, na kuisikia furaha ya kuzishika amri. Kwa kuwa wafuasi wa Kristo, tunafurahia katika baraka ya kutubu na shangwe ya kuweza kusamehewa. Wao wanakuwa sehemu yetu, wakitengeneza jinsi tunavyofikiri na kuhisi. …

“Kwa wengi, toba ni safari na si tukio la mara moja. Si rahisi. Kubadilika ni jambo gumu Inahitaji kukimbia katika upepo, kuogelea kinyume na mkondo wa maji. Mwokozi alisema, “Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate” [Mathayo 16:24]. Kutubu ni kugeuka kutoka baadhi ya mambo, kama vile kutokuwa na uaminifu, kiburi, hasira, na mawazo yasiyo safi, na kugeukia vitu vingine, kama vile, huruma, kutokuwa na ubinafsi, kuwa na uvumilivu na utakatifu. Ni ‘ku-rudi tena kwa Mungu” (“Tubu … Ili Kwamba Niweze Kukuponya,” Ensign au Liahona, Nov. 2009, 40–41).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wajumuishe wale wote wanaosumbuka. Wakati mwingine washiriki wa darasa wanaosumbuka wanahitaji kujumuishwa ili wajisikie wanapendwa. Fikiria kuwapangia jukumu ili washiriki katika somo lijalo. Usikate tamaa kama watashindwa kuitikia jitihada zako kwa mara ya kwanza. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 8-9.)

Chapisha