Njoo, Unifuate
Septemba 9–15. 2 Wakorintho 1–7: ‘Mpatanishwe kwa Mungu’


Septemba 9–15. 2 Wakorintho 1–7: ‘Mpatanishwe kwa Mungu’’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2019)

“Septemba 9–15. 2 Wakorintho 1–7,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Yesu Kristo

Septemba 9–15

2 Wakorintho 1–7

“Mpatanishwe kwa Mungu”

Unapojifunza barua ya Paulo kwa Wakorintho, andika baadhi ya kanuni za injili unazogundua na tafakari jinsi utakavyozitumia katika maisha yako.

Andika Misukumo Yako

Wakati mwingine, kuwa kiongozi wa Kanisa humaanisha kuweza kusema mambo mengine yaliyo magumu. Hii ilikuwa kweli katika siku ya Paulo kama ilivyo leo. Inavyoonekana barua iliyopita kutoka kwa Paulo kwenda kwa Watakatifu wa Korintho ilijumuisha maonyo na kusababisha hisia za kuumiza. Katika barua iliyokuja kuwa 2 Wakorintho, yeye alijaribu kuelezea kile kilichokuwa kimechochea maneno yake kuwa makali: “Maana katika dhiki nyingi na taabu ya moyo niliwaandikia na machozi mengi; si kwamba mhuzunishwe, bali mpate kujua upendo wangu nilionao kwenu jinsi ulivyo mwingi” (2 Wakorintho 2:4). Wakati unapokuwa katika upande wa kupokea baadhi ya masahihisho kutoka kwa kiongozi, kwa hakika inasaidia kujua kwamba ni mwongozo wa kiungu kwa upendo wa Kristo. Na hata katika hali hizo ambapo sivyo, kama tuko tayari kuwaona wengine kwa aina ya upendo Paulo aliouona, ni rahisi kuitikia kwa njia ifaayo kwa maudhi yoyote. Kama Mzee Jeffrey R. Holland alivyoshauri, “Kuwa mkarimu kuheshimu udhaifu wa binadamu—wa kwako na vilevile wa wale wanaotumikia pamoja nawe katika Kanisa linaloongozwa na wanaume na wanawake, wenye kujitolea. Isipokuwa katika suala la Mwanawe wa Pekee aliye mkamilifu, watu wasio wakamilifu ndio ambao Mungu amekuwa akishughulika nao”“Bwana Naamini,” Ensign au Liahona, Mei 2013, 94).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

2 Wakorintho 1:3–7; 4:6–10, 17–18; 7:4–7

Majaribu yangu yanaweza kuwa baraka.

Ukichukulia dhiki ambayo Paulo alipata kwenye huduma yake, siyo kitu cha kushangaza kwamba aliandika mengi kuhusu lengo na baraka za mateso. Fikiria kuhusu njia ambazo majaribu yako yanaweza kuwa baraka unaposoma 2 Wakorintho 1:3–7; 4:6–10, 17–18; na 7:4–7. Kwa mfano, unaweza kutafakari jinsi gani Mungu “amekufariji [wewe] katika dhiki [zako] zote” na jinsi gani unaweza, kwa zamu, “kuwafariji wale walio katika dhiki za namna zote”2 Wakorintho 1:4). Au unaweza kuzingatia katika nuru ya Yesu Kristo ambayo “iling’ara mioyoni mwetu,” hata wakati “tumedhikika” na “kuona shaka” (2 Wakorintho 4:6–10).

Ona pia Mosia 24:13–17; Mada za Injili, “Majaribu,” topics.lds.org.

2 Wakorintho 2:5–11

Ninapokea baraka na kuwabariki wengine ninaposamehe.

Hatujui mengi kuhusu mtu ambaye Paulo alimzungumzia katika 2 Wakorintho 2:5–11—ni kwamba tu alivunja sheria (ona mistari 5–6) na kwamba Paulo aliwataka Watakatifu wamsamehe (ona mistari 7–8). Je, ni kwa nini wakati mwingine tunashindwa “kuthibitisha upendo [wetu] kwa” mtu aliyetuudhi? (mstari 8). Ni kwa jinsi gani kuzuia msamaha kunawadhuru wengine na sisi wenyewe? (ona mistari 7:10–11). Inamaanisha nini kwako kwamba kutokuwasamehe wengine humpa nguvu “Shetani … ya kutushinda”? (mstari 11).

Ona pia Mafundisho na Maagano 64:9–11.

2  Wakorintho 5:14–21

Kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo, Ninaweza kupatanishwa na Mungu.

Kama ilivyo kwa mtu yeyote, Paulo alijua jinsi inavyokuwa kwa mtu kuwa “kiumbe kipya.” Alitoka kwenye kuwa mtesaji wa Wakristo mpaka kuwa mtetezi jasiri wa Kristo. Alijua mwenyewe jinsi gani Yesu, ambaye “hakuijua dhambi,” anaweza kuondoa dhambi zetu na kutupatia “haki,” Yake akiturejesha katika umoja na Mungu. Unaposoma mistari hii, fikiria kuhusu inamaanisha nini kupatanishwa na mtu mwingine. Ni kwa jinsi gani hii hukusaidia kuelewa inamaanisha nini kupatanishwa na Mungu? Tafakari nini kinaweza kuwa kinakutenganisha wewe na Mungu? Je, unahitaji kufanya nini ili kupatanishwa Naye kikamilifu?

Ona pia 2 Nefi 10:23–25.

2 Wakorintho 7:8–11

Kuhuzunika kwa jinsi ya Mungu hutupeleka kwenye toba.

Kwa kawaida hatufikirii huzuni kama kitu kizuri, lakini Paulo aliongelea juu ya “kuhuzunishwa kwa jinsi ya Mungu” kama sehemu muhimu ya toba. Je, unajifunza nini kuhusu kuhuzunishwa kwa jinsi ya mungu kutoka katika yafuatayo? 2 Wakorintho 7:8–11; Alma 36:16–21; Mormoni 2:11–15; na Mada za Injili, “Toba,” topics.lds.org. Ni lini ulijisikia kuhuzunika kwa jinsi ya Mungu, na ilileta athari gani katika maisha yako?

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Hapa kuna baadhi ya mapendekezo:

2  Wakorintho 3:1–3

Je, watu wa familia yako wamewahi kumuomba mtu kuwaandikia barua ya mapendekezo, kama vile kwa ajili ya maombi ya kazi au shule? Waombe wazungumzie tukio hilo na kile ambacho barua ilisema juu yao. Paulo alifundisha kwamba maisha ya Watakatifu yalikuwa kama barua za mapendekezo kwa ajili ya injili kutoka kwa Kristo Mwenyewe, “zilizoandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai.” Mnaposoma 2 Wakorintho 3:1–3 pamoja, jadilini ni kwa jinsi gani mifano yetu ni kama barua za mapendekezo kwa ajili ya injili ambazo zinaweza “kujulikana na kusomwa na watu wote.” Pengine kila mwanafamilia anaweza kuandika barua au “waraka” akielezea ni kwa jinsi gani mwanafamilia mwingine amekuwa mfano mzuri wa mfuasi wa Yesu Kristo. Wanaweza kusoma barua zao kwa familia na kumpa mwanafamilia waliyeandika juu yake. Kwa nini ni muhimu kuelewa kwamba maisha yetu ni “waraka wa Kristo”?

2 Wakorintho 5:6–7

Inamaanisha nini “twaenenda kwa imani, si kwa kuona”? Je, sisi tunafanya ili kuonyesha kwamba tunaamini katika vitu tusivyoviona?

2 Wakorintho 5:17

Je, familia yako inaweza kufikiria juu ya—au kutafuta—mifano katika uhalisia wa vitu ambavyo hupitia mabadiliko yasiyo kifani na kuwa kiumbe kipya? (ona picha inayoambatana na muhtasari huu). Je, mifano hii hutufundisha nini kuhusu jinsi gani injili ya Yesu Kristo inavyoweza kutubadilisha?

2 Wakorintho 6:1–10

Kulingana na mistari hii, inamaanishas nini kuwa “mtumishi wa Mungu”?

2 Wakorintho 6:14–18

Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kufuata ushauri wa Paulo, “Tokeni kati ya [wasioamini], na mkatengwe nao,” huku pia tukiwa mifano mizuri kwa wale wanaotuzunguka?

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fundisha masomo ya vitendo. Baadhi ya dhana za injili, kama vile Upatanisho, zinaweza kuwa ngumu kuelewa. Fikiria kutumia picha au vitu ambavyo vitaisaidia familia yako kuelewa kanuni unazogundua katika maandiko.

Picha
Kiwavi, kifukofuko, na kipepeo

Tunapoongoka kwenye injili ya Yesu Kristo, badiliko letu ni kubwa sana kwamba Paulo alilielezea kama kuwa “kiumbe kipya” (2 Wakorintho 5:17).

Chapisha