Njoo, Unifuate
Septemba 16–22. 2 Wakorintho 8–13: ‘Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu’


Septemba 16–22. 2 Wakorintho 8–13: ‘Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya (2019)

Septemba 16–22. 2 Wakorintho 8–13,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2019

Picha
Yesu akiongea na mtoto mdogo

Septemba 16–22

2 Wakorintho 8–13

“Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu”

Kuandika misukumo yako ya kiroho kutakuwezesha kukumbuka kile unachojifunza wakati wa kujifunza maandiko. Unaweza kuandika katika shajara ya kujifunza, andika kwa ufupi pembeni mwa maandiko yako, ongeza kwa kuandika kifupi kwenye Gospel Library app, au jitengenezee rekodi ya kusikiliza ya mawazo yako.

Andika Misukumo Yako

Je, ungefanya nini kama ungesikia kwamba mkusanyiko wa Watakatifu katika eneo jingine ulikuwa unasumbuka katika ufukara? Hii ndiyo hali ambayo Paulo aliielezea kwa Watakatifu wa Korintho katika 2 Wakorintho 8–9. Alitumaini kuwashawishi Watakatifu wa Korintho kujitolea sehemu ya ziada yao kwa Watakatifu wenye uhitaji. Lakini zaidi ya ombi la kujitolea, maneno ya Paulo pia yalikuwa na kweli za kina kuhusu kutoa: “Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima: maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu” (2 Wakorintho 9:7). Katika siku yetu, bado kuna Watakatifu ulimwenguni kote ambao wanahitaji msaada. Wakati mwingine kikubwa tunachoweza kufanya kwa ajili yao ni kufunga na kutoa matoleo ya mfungo. Katika mambo mengine, kutoa kwetu kunaweza kuwa kwa moja kwa moja na kibinafsi. Katika mfumo wowote dhabihu zetu zilivyo, inastahili kujiuliza sababu ya kutoa kwetu. Je, dhabihu zetu ni kielelezo cha upendo” Hata hivyo, ni upendo ambao humfanya mtoaji kutoa kwa moyo mkunjufu.

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo ya Kujifunza Maandiko Binafsi

2 Wakorintho 8:1–15; 9:5–15

Ninaweza kwa moyo mkunjufu kushiriki na wengine kile nilichonacho ili kuwabariki masikini na wenye shida.

Kuna watu wengi sana wenye shida kote ulimwenguni. Ni kwa jinsi gani tunaweza kuleta tofauti” Mzee Jeffrey R. Holland alitoa ushauri huu: “Tajiri au maskini, sote tunapaswa ‘kutenda tunavyoweza’ wakati wengine wakiwa katika shida [ona Marko 14:6, 8]. … [Mungu] atakusaidia na kukuongoza katika matendo ya upendo ya kiufuasi kama kwa uangalifu unataka na kuomba na kutafuta njia za kutii amri alizotupa tena na tena” (“Je Sisi Sote Si Waombaji?” Ensign au Liahona, Nov. 2014, 41).

Soma 2 Wakorintho 8:1–15; 9:6–15, andika kwa kifupi kanuni alizofundisha Paulo kuhusu kuwajali masikini na wenye shida. Je, ni kitu gani kinakuvutia kuhusu ushauri wa Paulo? Unaweza kuomba kwa ajili ya mwongozo kuhusu kile unachoweza kufanya ili kumbariki mtu mwenye shida. Hakikisha unaandika misukumo yoyote unayopokea na uifanyie kazi.

Ona pia Mosia 4:16–27; Alma 34:27–29; Henry B. Eyring, “Je Saumu Niliyoichagua Siyo ya Namna Hii?” Ensign au Liahona, Mei 2015, 22–25; Linda K. Burton, “Nalikuwa Mgeni,” Ensign au Liahona, Mei 2016, 13–15.

2 Wakorintho 11

Manabii wa uongo hutafuta kudanganya.

Inaweza kukusaidia kuelewa sura hii kujua kwamba “mitume wa uongo” waliinuka miongoni mwa Watakatifu wa Korintho (2 Wakorintho 11:13). Je, unajifunza nini kutoka mstari 13–15 kuhusu wale wanaofundisha mafundisho ya uongo? Je, unajifunza nini kuhusu manabii wa kweli unaposoma kuhusu uzoefu wa Paulo kama mtumishi wa Kristo? (Ona mstari 23–33).

2 Wakorintho 11:3; 13:5–8

Ninapaswa “kuukagua” uaminifu wangu katika injili ya Yesu Kristo.

Kwa sababu leo kuna wengi wanaotafuta kutupeleka mbali “tukauacha unyofu na usafi kwa Kristo” (2 Wakorintho 11:3), unaweza kukubali mwaliko wa Paulo wa “kujijaribu [mwenyewe], kama umekua katika imani” (2 Wakorintho 13:5). Kwa mfano, unaweza kutafakari nini unaweza kuondoa kutoka katika maisha yako ambacho kitakuwezesha kuzingatia kwa Kristo, au unaweza kutekeleza “shughuli ya sifa” katika Hubiri Injili Yangu, ukurasa 126.

2 Wakorintho 12:2–4

Je, mbingu ya tatu” ni nini, na nani alikuwa mtu “aliyenyakuliwa” kwenda huko?

Katika mistari hii, Paulo alikuwa akijiongelea, bila kujitaja moja kwa moja—pengine kuepuka kujivuna kuhusu ono lake la ajabu. Kirai “mbingu ya tatu” humaanisha ufalme wa selestia (ona M&M 76:96–98).

2 Wakorintho 12:5–10

Neema ya Mwokozi yatosha kunisaidia mimi kupata nguvu katika udhaifu wangu.

Hatujui “mwiba katika mwili” wa Paulo ulikuwa nini, lakini ni rahisi kuhusisha na tamaa yake ya kutaka uondolewe. Sote tuna changamoto na matatizo ambayo Bwana ameona haifai kuyaondoa katika maisha yetu. Fikiria kuhusu changamoto zako mwenyewe unaposoma 2 Wakorintho 12:5–10. Je, Paulo alifundisha nini kuhusu udhaifu? Inamaanisha nini kwako kwamba neema ya Mungu inatosha kwa ajili yako? Je, ni kwa jinsi gani umepata uzoefu wa nguvu ya uimarisho ya Mungu?

Ona pia Mosia 23:21–24; 24:10–15; Etheri 12:27; Moroni 10:32–33.

2 Wakorintho 13:1.

Je, Paulo alimaanisha nini alipoongea juu ya “mashahidi wawili au watatu”?

Katika nyakati za Agano la Kale, mashahidi wawili au watatu walihitajika kutoa mashitaka dhidi ya mtu (ona Kumbukumbu la Torati 19:15). Paulo alidondoa utaratibu huu alipoongelea ujio wake wa tatu huko Korintho. Mifano ya siku za leo ya kanuni hii ya mashahidi wengi hujumuisha Mashahidi Watatu wa Kitabu cha Mormoni, shuhuda za Yesu Kristo zilizotolewa na Biblia na Kitabu cha Mormoni, na utaratibu wa wamisionari, waalimu wa nyumbani, na waalimu watembeleaji wakishuhudia wakiwa wawili.

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia.

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani.

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Hapa kuna baadhi ya mapendekezo:

2 Wakorintho 8–9

Je, unagundua nini katika sura hizi ambacho kinaishawishi familia yako kuwafikia maskini na wenye shida? Huu unaweza kuwa ni wakati mzuri wa kuandaa tendo la huduma kama familia kwa mtu mwenye shida.

2 Wakorintho 9:6–7

Je, familia yako inamjua mtu ambaye anaweza kuelezewa kama “atoaye kwa moyo wa ukunjufu”? Ni kwa jinsi gani tunaweza kufanya huduma yetu kwa wengine kuwa ya moyo wa ukunjufu zaidi?

2 Wakorintho 10:3–7

Ni kwa jinsi gani unaweza kuifundisha familia yako kuhusu “vita” vyetu dhidi ya uovu? Je, familia yako itafurahia kujenga ukuta au ngome kwa kutumia viti na mablanketi? Hii inaweza kutupeleka kwenye mjadala kuhusu jinsi ya kuangusha mambo yanayotuongoza mbali na Mungu na “[kuteka] nyara kila fikira ipate kumtii Kristo.” Ni “silaha” zipi za kiroho tunatumia kuthibiti mawazo yetu? (ona Waeffeso 6:11–18).

2 Wakorintho 11:3.

Je, familia yako inaweza kufanya nini ili kuzingatia zaidi kwenye “unyofu kwa Kristo”?

Kwa mawazo zaidi juu ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii ndani ya Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Andika Misukumo. Mzee Richard G. Scott alisema: “Maarifa yanayoandikiwa kwa uangalifu ni maarifa unayoweza kuyatumia katika wakati wa shida. … [Kuandika mwongozo wa kiroho] huongeza uwezekano wako wa kupokea nuru zaidi” (“Kupata Maarifa ya Kiroho,” Ensign, Nov. 1993, 88; ona pia Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 1230).

Picha
Vijana wadogo wakisaidia kwenye kazi ya kujitolea

“Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima: maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu” (2 Wakorintho 9:7).

Chapisha