Njoo, Unifuate
Septemba 9–15. 2 Wakorintho 1-7: ‘Mpatanishwe kwa Mungu’


“Septemba 9–15. 2Wokorintho 1–7:”Mpatanishwe kwa Mungu’”. Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2019 (2019)

“Septemba 9–15. 2 Wakorintho 1-7” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2019

Picha
Yesu Kristo

Septemba 9–15

2 Wakorintho 1–7

“ Mpatanishwe kwa Mungu” .

Anza maandalizi yako kwa kusoma 2 Wakorintho 1–7. Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia inaweza kukusaidia kuelewa sura hizi, na huu muhtasari unaweza kukupa mawazo ya kufundisha.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Baadhi ya watoto katika darasa lako wanaweza kuwa wameandika barua wiki hii kuhusu jinsi mwana familia alivyo mfano mzuri wa mfuasi wa Yesu Kristo. Kama walifanya hivyo, waombe kabla ya muda washiriki barua darasani. Au waombe watoto washiriki jambo lingine walilojifunza.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wadogo

2 Wakorintho 1:3–4

Baba wa Mbinguni hunifariji, na mimi naweza kuwafariji wengine.

Je, ni kwa namna gani unaweza kuwapa watoto matumaini kwamba Baba wa Mbinguni atawafariji? Je, ni kwa namna gani unaweza kuwatia moyo wa kuwafariji wengine?

Shughuli Yamkini

  • Lete vitu darasani ambavyo vinatoa faraja, kama vile blanketi au bendeji. Waulize watoto nini kinawafariji wakati wana huzuni au hofu au wana matatizo mengine. Soma 2 Wakorintho 1:3–4 pamoja na watoto, na eleza kwamba “dhiki” ni neno lingine kwa ajili ya matatizo magumu. Elezea baadhi ya njia ambazo Baba wa Mbinguni amekufariji, na shuhudia kwamba atawafariji watoto vile vile.

  • Onyesha picha za watu wakiwa wanabatizwa (ona Kitabu Cha Sanaa za Injili, na. 103 na 104) unaposoma 2 Wakorintho 1:4 na Mosia 18:8–9 kwa watoto. Eleza kwamba wakati wa ubatizo sisi tunaahidi kuwa tutawafariji wengine. Je, ni kwa namna gani sisi tunaweza kufuata ushauri wa Paulo wa “kuwafariji katika dhiki zao zote”?

  • Waalike wanafunzi kuchora picha yao wenyewe wakimsaidia mtu fulani mwenye shida. Waache waeleze jinsi kufanya vitu hivi kunaweza kuleta faraja kwa wengine.

2 Wakorintho 2:7–8 10

Mimi Naweza Kuwasamehe Wengine.

Chagua kutoka shughuli zifuatazo—au lete yako mwenyewe—kusaidia kuimarisha matamanio ya watoto kuwasamehe wengine.

Shughuli za Yakini

  • Waelezee watoto kwamba Paulo alitaka Watakatifu wa Korintho kumsamehe mtu aliyefanya dhambi. Soma 2 Wakorintho 2:7–8 10, na waalike watoto kuweka mikono yao juu ya mioyo yao kila wakati wanaposikia maneno samehe na alisamehe.

  • Waalike watoto waigize jinsi watakavyoitika katika hali ya mtu fulani akifanya jambo la kikatili. Acha watoto wachukue zamu kusema “Samahani” na “ninakusamehe.” Tunawasaidiaje watu kujua kwamba tunawasamehe? Eleza kwamba njia moja inaweza kuwa “kuthibitisha upendo wako,” au kuonyesha upendo kwao (2 Wakorintho 2:8).

2 Wakorintho 4:1–2

Ninaamini katika kuwa mwaminifu.

Paulo alifundisha kwamba watumishi wa Kristo hawasemi uongo kwa wengine—“wamekataa vitu vilivyojificha vya kutokuwa waaminifu.” Tafakari jinsi unavyoweza kuimarisha hamu za watoto za kutaka kuwa waaminifu katika mambo vyote.

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kukariri kirai “Tunaamini katika kuwa waaminifu” (Makala ya Imani 1:13). Andika kirai hiki kwenye bangili ya karatasi watoto waweze kupamba na kuvaa nyumbani. Elezea kwamba kuwa mwaminifu humaanisha kusema ukweli.

  • Waombe watoto wainue mikono yao unaposema kitu ambacho ni cha kweli na waishushe unaposema kitu ambacho sio cha kweli. Toa kauli rahisi lakini ya dhahiri, kama vile “Leo ni Jumapili” au “Nina pua tatu.” Rudia shughuli hii mara kadhaa, ukiwaacha watoto wachukue zamu kuwa yule anayefanya kauli za kweli na za uongo. Kwa nini ni vizuri kuwa mwaminifu?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Watoto Wakubwa

2 Wakorintho 1:3–4

Baba wa Mbinguni hunifariji, na mimi naweza kuwafariji wengine.

Kukumbuka jinsi Mungu alivyowafariji kunaweza kuwavutia watoto kutoa faraja kwa wengine.

Shughuli Yamkini

  • Unaposoma 2 Wakorintho 1;3–4, waombe watoto kusikiliza jibu kwa swali “Mungu anafanya nini kwa ajili yetu?” Wasaidie watoto kuorodhesha njia ambazo Mungu anatufariji. Waalike watoto washiriki uzoefu wakati walipokuwa wamehuzunika au kuwa na wasiwasi au na hofu na Mungu akawafariji.

  • Waalike watoto kushiriki njia ambazo tunaweza kuwafariji wengine. Wape muda wa kumfikiria mtu fulani wanayemjua anayehitaji faraja na fanya mpango wa kumfikia mtu huyo.

2 Wakorintho 2:5–11

Mimi Naweza Kuwasamehe Wengine.

Inaweza kuwa vigumu kuwasamehe wengine wakati wao ni wakatili kwetu. Lakini watoto unaowafundisha watapata uzoefu wa upendo, amani, na furaha wanapojifunza kusamehe.

Shughuli Yamkini

  • Waambie watoto kwamba mtu fulani Korintho alikuwa amefanya dhambi na “alisababisha huzuni” kwa Watakatifu (ona 2 Wakorintho 2:5). Waombe watoto kupekua 2 Wakoritho 2:7–8 na watafute kile ambacho Paulo aliwataka Watakatifu wafanye.

  • Elezea juu ya tukio ambalo wewe ulimsamehe mtu fulani—au mtu fulani alipokusamehe wewe—na jinsi ulivyojisikia baadaye.

2 Wakorintho 5:6–7

“Ninatembea kwa imani, sio kwa kuona.”

Fikiria jinsi unavyoweza kuwatia moyo watoto kutii amri za Mungu hata wakati hawaoni baraka wanazotamani mara moja.

Shughuli Yamkini

  • Soma 2 Wakorimtho 5:6–7 na Alma 32:21 pamoja na watoto, na uwaombe watafute maneno na virai ambavyo vinasaidia kufafanua imani. Waombe waandike ufafanuzi wao, usome kwa sauti, na uweke ubaoni.

  • Mfumbe macho mmoja wa watoto, na waombe watoto wengine kutoa maelekezo ya kumsaidia kukamilisha kazi kama vile kujenga mnara kwa matofali, kuweka pamoja fumbo, au kutembea kuvuka chumba. Ni kwa jinsi gani shughuli hii inatusaidia kuelewa nini inamaanisha “kutembea kwa imani” katika Mungu?

  • Onyesha video “Imani Safi na Rahisi” (LDS.org), na wauliza watoto jinsi gani msichana alitembea kwa imani. Shiriki uzoefu wako wakati ulipotakiwa uwe na imani katika Mungu. Waalike watoto kushiriki uzoefu wo wote waliowahi kuwa nao wa kutembea kwa imani.

2 Wakorintho 7:8–11

Huzuni ya kimungu inaniongoza kutubu.

Ni kawaida kwa watoto kuona haya au aibu wakati wanaposhikwa wakifanya kitu kisicho sahihi. Wasaidie kutofautisha hisia hizi na huzuni ya kimungu, inayoongoza kwenye toba ya kweli.

Shughuli Yamkini

  • Eleza kwamba katika 2 Wakorintho 7:8–11, Paulo alirejea barua aliyoiandika punde kwa Watakatifu, kwa ujasiri akiwaonya kuhusu dhambi zao. Someni aya hizi pamoja. Kwa nini Paulo alifurahi kwamba Watakatifu walikuwa na huzuni? Toa angalizo kwamba aina hii ya huzuni inaitwa huzuni ya kimungu.

  • Waombe watoto kufumba macho yao na kufikiria kuhusu muda walipofanya kitu kisicho sahihi na wakajisikia vibaya kuhusu kitu hicho. Waalike kujiuliza wenyewe, “Kwa nini nilijisikia vibaya?” Andika ubaoni baadhi ya sababu ambazo watu hujisikia vibaya baada ya kufanya kitu ambacho sio sahihi, kama vile “Niliogopa ningeadhibiwa” au “niliona aibu ya kile watu wangenifikiria” au nilijua Baba wa Mbinguni alikuwa amesikitishwa nami.” Lipi kati ya majibu ubaoni linaonekana kama ni “huzuni ya kimungu”? Kwa nini huzuni ya kimungu ni bora kuliko aina zingine za huzuni tunazoweza kuhisi baada ya kufanya kitu kisicho sahihi?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waambie watoto kwamba wanaweza kushiriki mojawapo ya shughuli kutoka darasa la leo pamoja na familia zao nyumbani, labda wakati wa jioni ya familia nyumbani.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Onyesha maandiko. Chagua aya ya maandiko ambayo unayaona yakiwa na maana na uitundike katika darasa lako ambapo watoto wataiona mara kwa mara. Pengine watoto wanaweza kuchukua zamu kuchagua andiko la kutundikwa.

Chapisha