Agano Jipya 2023
Januari 2–8. Mathayo 1; Luka 1: “Na Iwe Kwangu kama Ulivyosema”


“Januari 2–8. Mathayo 1; Luka 1: ‘Na Iwe Kwangu kama Ulivyosema’” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022)

“Januari 2–8. Mathayo 1; Luka 1,” Njoo,Unifuate—Kwa ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
Mariamu na Elisabeti

Januari 2–8

Mathayo 1; Luka 1

“Na Iwe Kwangu kama Ulivyosema”

Kabla hujasoma taarifa za nyongeza za kujifunza, soma na tafakari Mathayo 1 na Luka 1, na uandike misukumo yako ya kiroho. Mwachie Roho aongoze maandalizi yako. Kisha chunguza mawazo katika muhtasari huu na katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kusudi kuu la Mathayo, Luka na wale waandishi wengine wa Injili lilikuwa ni kushuhudia kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu. Wape washiriki wa darasa dakika chache kurejelea Mathayo1 au Luka1 na washiriki aya moja inayojenga imani yao katika Yesu Kristo. Pendekeza kwa darasa kwamba wanapojifunza Agano Jipya mwaka huu, wangeweza kuweka orodha ya vifungu ambavyo vinashuhudia kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu. Mnaweza hata kuweka orodha hii kama darasa.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mathayo 1:18–25; Luka 1:5–80

Baba wa Mbinguni hufanya kazi kupitia watoto Wake waaminifu ili kukamilisha malengo yake.

  • Washiriki wa darasa yawezekana wakapata uzoefu wa maana wakati wakijifunza Agano Jipya mwaka huu kama wanaweza kupata masomo kutokana na uzoefu wa watu wanaowasoma. Ili kuwasaidia kufanya hivi, unaweza kuandika majina ya watu katika Mathayo 1 na Luka 1 ubaoni, pamoja na marejeleo ya maandiko kuhusu watu hawa, kama ifuatavyo:

    Tunaweza kujifunza nini kutoka kwenye hadithi hizi ambacho kinaweza kutusaidia sisi leo?

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kufikiria kwa kina kuhusu Mariamu na nafasi yake katika mpango wa Baba, unaweza kuonyesha video “An Angel Foretells Christ’s Birth to Mary” and “Mary and Elisabeth Rejoice Together” (ChurchofJesusChrist.org). Au mngeweza kusoma pamoja Luka 1:26–38, 46–56, mkitafuta vitu ambavyo Mariamu alivisema ambavyo vinadhihirisha kitu fulani juu ya tabia yake. Kitu gani kingine tunachojifunza kutoka kwa Mariamu?

Luka 1:5–25

Baraka za Mungu zinakuja kwa wakati Wake mwenyewe.

  • Kunaweza kuwa na watu katika darasa lako ambao, kama Elisabeti na Zakaria, wanaishi maisha ya uadilifu na bado hawajapokea baraka walizotegemea. Fikiria kualika darasa kupekua Luka 1:5–25, wakitafuta masomo wanayoweza kujifunza kutoka kwa Elisabeti na Zakaria kuhusu kumngojea Bwana. Ni mifano gani mingine ya kungojea wakati wa Bwana ambayo washiriki wa darasa wanaweza kushiriki kutoka kwenye maisha yao wenyewe au kutoka kwenye matukio ya maandiko? Je, tunajifunza nini kutokana na mifano hii? Washiriki wa darasa wangeweza pia kujadili maelezo katika “Nyenzo za Ziada.”

Luka 1:26–38

“Kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”

  • Washiriki wa darasa wanaweza wakati mwingine kushangaa—kama Mariamu alivyofanya—jinsi gani mipango ya Mungu kwa ajili yao au ahadi kwa ajili yao zinavyoweza kutimizwa. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa kwamba kupitia uwezo wa Mungu mambo yote yanawezekana, unaweza kuonyesha picha Upashaji Habari: Malaika Gabrieli Anamtokea Mariamu (Kitabu cha Sanaa ya Injili, na. 28) na waalike wasome pamoja Luka 1:26–38. Tunaweza kujifunza nini kuhusu kushinda yanayoonekana kama hayawezekani kwa kujifunza maneno na matendo ya Mariamu? Waombe washiriki wa darasa kushiriki uzoefu ambapo Mungu aliwasaidia kutimiza kitu walichofikiria kuwa hakiwezekani.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Kumngojea Bwana.

Tukitambua kwamba wengi wetu tunajiuliza kwa nini tunapaswa kungojea baraka za Mungu, Mzee Jeffrey R. Holland alisema:

“Jibu kwa swali kama hilo ni ‘Ndiyo, Mungu anaweza kutoa muujiza mara moja, lakini punde au baadae tunajifunza kwamba nyakati na majira ya safari yetu katika mwili wenye kufa ni Vyake na ni Yeye pekee ndiye atayeelekeza.’ … Imani humaanisha kumtumaini Mungu katika nyakati nzuri na mbaya, hata kama hiyo inajumuisha mateso fulani hadi tunapouona mkono Wake ukifunuliwa kwa niaba yetu. …

“… Wale ‘wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya [na] watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, na hawatachoka; … watakwenda kwa miguu, na hawatazimia’ [Isaya 40:31; msisitizo umeongezwa]. Ninaomba kwamba ‘hatua kwa hatua’—punde au baadae—baraka zile zije kwa kila mmoja wenu anayetafuta msaada kutokana na masikitiko yenu na uhuru kutokana na huzuni zenu. Ninatoa ushahidi wa upendo wa Mungu na wa Urejesho wa injili Yake tukufu, ambayo, kwa njia moja au nyingine, ndilo jibu la kila jambo tunalokabiliana nalo katika maisha” (“Kumngojea Bwana,” Liahona, Nov. 2020, 116–17).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wahimize washiriki wa darasa kujifunza maandiko nyumbani. Njia mojawapo ya kuhimiza kujifunza maandiko nyumbani ni kutoa muda kwa washiriki kuelezea mambo waliyogundua na utambuzi unaotokana na kujifunza binafsi na kifamilia (ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi29).

Chapisha