Agano Jipya 2023
Januari 16–22. Yohana 1: Tumemwona Masiya


“Januari 16–22. Yohana 1: Tumemwona Masiya,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022.)

“Januari 16–22. Yohana 1,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
mwanamke akishiriki injili kwenye kituo cha treni.

Januari 16–22

Yohana 1

Tumemwona Masiya

Unaposoma na kutafakari Yohana 1, sali upate mwongozo wa kiroho katika kazi yako ya kufundisha kuhusu ushuhuda wa Yohana. Andika misukumo unayopokea. Njoo Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia na mawazo katika muhtasari huu yanaweza kuwashawishi watu katika darasa lako kuelewa na kutumia mafundisho katika sura hii.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kushiriki kitu wanachojifunza, unaweza kuwaomba waandike maswali, maoni au utambuzi kutoka kwenye usomaji wao katika vipande vya karatasi na uviweke kwenye chombo. Chukua vipande kutoka kwenye chombo hicho ili kujadili kama darasa.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Yohana 1:1–5

Yesu Kristo “mwanzo alikuwako kwa Mungu.”

  • Yohana alifundisha nini kuhusu Yesu kabla ya hajazaliwa duniani? Kwa nini ni muhimu kujua kuhusu nafasi za Kristo kabla ya kuzaliwa duniani? Inaweza kusaidia kuandika maswali haya ubaoni na kuwaomba washiriki wa darasa kutafuta majibu katika Yohana 1:1–5 (ona pia Tafsiri ya Joseph Smith, Yohana 1:1–5 [katika kiambatisho cha Biblia]; Musa 1:32–33; Mwongozo wa Mada, “Jesus Christ, Antemortal Existence of”). Washiriki wa darasa wangeweza pia kushiriki kitu wanachojifunza kuhusu nafasi za Mwokozi kabla ya kuzaliwa duniani kutoka katika “Kristo Aliye Hai: Ushuhuda wa Mitume” (ChurchofJesusChrist.org).

  • Kama ungependa kutumia aya hizi kuzungumza kuhusu uumbaji wa Bwana, unaweza kusoma Yohana 1:3 na uonyeshe picha ambazo zinaonyesha uzuri wa dunia. Ungeweza kuonyesha video ya “Our Home” (ChurchofJesusChrist.org). Waalike washiriki wa darasa kushiriki jinsi uumbaji wa Mwokozi unavyowasaidia kuhisi upendo Wake.

Yohana 1:1–14

Yesu Kristo ndiye Nuru.

  • Fikiria kuwauliza washiriki wa darasa kupata kila mfano wa neno nuru katika Yohana 1:1–14. Kwa nini nuru ni neno zuri kumwelezea Yesu Kristo? Washiriki wa darasa wanaweza kushiriki ni kwa jinsi gani Mwokozi na injili Yake huleta nuru ya kiroho katika maisha yao. Kama sehemu ya majadiliano haya, unaweza kuwaalika washiriki wa darasa wasome zaidi kuhusu Nuru ya Kristo katika Mafundisho na Maagano 84:45–46; 88:11–13, au unaweza kuwarejesha kwenye “Nuru ya Kristo” katika Kamusi ya Biblia. Ni kwa jinsi gani tunaweza kushiriki nuru ya Mwokozi na wengine?

    Picha
    mwanga wa jua kupitia uumbaji wa mwamba ufukoni

    Mwokozi na injili Yake hutoa nuru ya kiroho.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuvuta taswira ya kitu kinachofundishwa kuhusu Mwokozi katika Yohana 1, ungeweza kuonyesha picha kadhaa (ikijumuisha moja kutoka katika muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia) ambazo zinaonyesha vipengele vya maisha ya Yesu Kristo na huduma yake ya kiungu. Washiriki wa darasa wangeweza kupekua Yohana 1:1–14, wakitafuta maneno au virai ambavyo vingeweza kutumika kama majina ya hizo picha.

Yohana 1:35–51

Tunaweza kupata ushahidi wetu wenyewe juu ya Mwokozi na kisha kuwaalika wengine “waje na waone.”

  • Katika Yohana 1, mwaliko wa “njoo uone” unajitokeza mara mbili (ona mistari ya 39, 46). Tunaweza tusiwe na bahati ya kumwona Mwokozi kimwili kwa njia ambayo Andrea na Nathanaeli walivyofanya, lakini tunaweza kujibu mwaliko huo huo. Yawezekana ikamaanisha “njoo uone” katika siku yetu?

  • Washiriki wa darasa wangeweza kusoma Yohana 1:35–51 na kushiriki kitu wanachojifunza kutoka kwenye mistari hii kuhusu kuwaalika wengine kujifunza kuhusu Kristo (ona pia “Nyenzo za Ziada” au video ya “Inviting Others to ‘Come and See’” kwenye ChurchofJesusChrist.org). Wangeweza pia kushiriki jinsi wao walivyopata njia rahisi na halisi za kuwaalika wengine “kuja na waone.”

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Tunaweza kuwaalika wengine “waje na waone.”

Mzee Neil L. Andersen alifundisha:

“Mwokozi alitufundisha jinsi ya kushiriki injili. Ninapenda hadithi ya Andrea, ambaye aliuliza, ‘Bwana, unakaa wapi?’ [Yohana 1:38.] Yesu angeweza kujibu kwa kutoa sehemu ambako Yeye aliishi. Lakini badala yake alimwambia Andrea, ‘Njoo uone’ [Yohana 1:39]. Ninapenda kufikiri kwamba Mwokozi alikuwa anasema, ‘Njoo uone sio tu wapi ninapokaa bali jinsi ninavyoishi. Njoo na uone mimi ni nani. Njoo na umsikie Roho.’ Hatujui kila kitu kuhusu siku ile, lakini tunajua kwamba wakati Andrea alipomwona kaka yake Simoni, alitangaza, “Tumemwona … Kristo’ [Yohana 1:41].

“Kwa wale wanaoonyesha kuvutiwa na mazungumzo yetu, tunaweza kufuata mfano wa Mwokozi kwa kuwaalika “njooni muone.’ Baadhi watakubali mwaliko wetu, na wengine hawatakubali. Sisi sote tunamjua mtu ambaye amealikwa mara kadhaa kabla hajaukubali mwaliko wa ‘njoo uone’” (“Ni Muujiza,” Liahona, Mei 2013, 79).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie wanafunzi walinganishe maandiko na wao wenyewe. Mwaliko ule ule Kristo aliowapa wafuasi Wake—wa njoo uone—unaweza kuwasaidia wale unaowafundisha kutamani kumfuata Mwokozi. Wahimize wanafunzi kutumia kanuni zinazopatikana katika maandiko katika maisha yao wenyewe na kuwaalika wengine kufanya vivyo hivyo. (Ona 1 Nefi 19:23; Kufundisha katika Njia ya Mwokozi21.)

Chapisha