Agano Jipya 2023
Januari 16–22. Yohana 1: Tumemwona Masiya


“Januari 16–22. Yohana 1: Tumemwona Masiya,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

“Januari 16–22. Yohana 1,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
mwanamke akishiriki injili kwenye kituo cha treni

Januari 16–22

Yohana 1

Tumemwona Masiya

Unaposoma na kutafakari Yohana 1, andika misukumo unayopokea. Ni ujumbe gani unaupata ambao utakuwa na thamani kubwa kwako wewe na kwa familia yako? Ni nini ungeweza kushiriki katika madarasa yako ya Kanisani?

Andika Misukumo Yako

Je umewahi kujiuliza kama ungemtambua Yesu wa Nazareti kama Mwana wa Mungu kama ungekuwa hai wakati wa huduma Yake duniani? Kwa miaka, Waisraeli waaminifu, akiwemo Andrea, Petro, Filipo, na Nathanaeli, walisubiri na kuomba kwa ujio wa Masiya aliyeahidiwa. Walipokutana naye, walijuaje kwamba Yeye Ndiye waliyekuwa wakimtafuta? Ni kwa njia hiyo wote tunakuja kumjua Mwokozi—kwa kukubali mwaliko wa “njoni nanyi mtaona” wenyewe (Yohana 1:39). Tunasoma kuhusu Yeye katika maandiko. Tunasikia mafundisho Yake. Tunafuata njia Zake za kuishi. Tunamsikia Roho Wake. Njiani, tunagundua, kama Nathanaeli alivyogundua, kwamba Mwokozi anatujua na anatupenda na anataka kutuandaa kupokea “mambo makubwa” (Yohana 1:50).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Yohana alikuwa nani?

Yohana alikuwa mwanafunzi wa Yohana Mbatizaji na baadaye alikuwa mmoja wa wafuasi wa mwanzo wa Yesu Kristo na mmoja wa Mitume Wake Kumi na wawili. Aliandika Injili ya Yohana, nyaraka kadhaa, na kitabu cha Ufunuo. Katika Injili yake, alijitambulisha kama mwanafunzi “ambaye Yesu alimpenda” na yule “mwanafunzi mwingine” (Yohana 13:23; 20:3). Ari ya Yohana ya kuhubiri injili ilikuwa kubwa kiasi kwamba aliomba kubaki duniani mpaka Ujio wa Pili wa Mwokozi ili azilete nafsi nyingi kwa Kristo (ona Mafundisho na Maagano 7:1–6).

Ona pia Kamusi ya Biblia, “Yohana” na “Yohana, Injili ya.”

Yohana 1:1–5

Yesu Kristo “mwanzo alikuwako kwa Mungu.”

Yohana alianza injili yake kwa kuelezea kazi ambayo Kristo alifanya kabla Yeye hajazaliwa: “Hapo mwanzo … Neno [Yesu Kristo] alikuwako kwa Mungu.” Unajifunza nini kutoka mstari wa 1–5 kuhusu Mwokozi na kazi Yake? Unaweza kupata ufafanuzi wenye msaada katika Tafsiri ya Joseph Smith, Yohana 1:1–5 (katika kiambatisho cha Biblia). Unapoanza kujifunza kwako kuhusu maisha ya Mwokozi, kwa nini ni muhimu kujua kuhusu kazi Yake kabla ya kuzaliwa?

Ona pia Mada za Injili, “Yesu Kristo Alichaguliwa kama Mwokozi,” topics.ChurchofJesusChrist.org.

Yohana 1:1–18

Yesu Kristo ni “nuru halisi,” Mwana wa Mungu.

Yohana alipata ushawishi wa kumtafuta Mwokozi kwa sababu ya ushuhuda wa Yohana Mbatizaji, ambaye alitangaza kwamba yeye “alitumwa kutoa ushuhuda wa … Nuru halisi” (Yohana 1:8–9, 15–18). Yohana mwenyewe pia alitoa ushahidi wenye nguvu wa maisha na huduma ya Mwokozi.

Inaweza kuwa ya kuvutia kuweka orodha ya kweli ambazo Yohana alizijumuisha katika ushuhuda wake wa ufunguzi juu ya Kristo (mstari wa 1–18; ona pia Tafsiri ya Joseph Smith, Yohana 1:1–19 [katika kiambatisho cha Biblia]). Kwa nini unafikiri kwamba Yohana alianza Injili yake na kweli hizi? Fikiria kuandika ushahidi wako juu ya Yesu Kristo—ungetaka kushiriki nini? Ni uzoefu gani umekusaidia kumjua na kumfuata Mwokozi? Ni nani anaweza kubarikiwa kwa kusikia ushuhuda wako?

Yohana 1:11–13

Yesu Kristo hutupatia “nguvu za kuwa” wana na mabinti wa Mungu.

Japo sisi sote ni wana na mabinti wa kiroho wa Mungu Baba, tunapotenda dhambi tunakuwa tumefarakana au kutenganishwa Naye. Yesu Kristo hutupatia njia ya kurudi kupitia dhabihu Yake ya upatanisho. Tafakari kile ambacho Yohana 1:1–13 hufundisha kuhusu kuwa mabinti na wana wa Mungu. Fikiria pia kile ambacho maandiko haya yanafundisha kuhusu jinsi gani tunapokea kipawa hiki: Warumi 8:14–18, Mosia 5:7–9; Mafundisho na Maagano 25:1. Inamaanisha nini kwako kuwa na “nguvu za kuwa” binti na mwana wa Mungu?

Yohana 1:18

Baba anatoa ushuhuda juu ya Mwana Wake.

Yohana 1:18 inasema kwamba hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu. Hata hivyo, Tafsiri ya Joseph Smith ya mstari huu inafafanua kwamba “hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote, isipokuwa yeye ameshuhudia juu ya Mwana” (ona Yohana 1:18, tanbihi c). Fikiria kupitia tena mifano ifuatayo ambayo kwayo Mungu Baba alisikika akitoa ushuhuda juu ya Mwana: Mathayo 3:17; 17:5; 3 Nefi 11:6–7; Joseph Smith—Historia 1:17.

Kwa nini ni baraka kuwa na taarifa hizi? Je, zinakufundisha nini kuhusu uhusiano wa Yesu Kristo na Baba Yake?

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Picha
msichana akisoma maandiko

Tunapojifunza maandiko, tutapokea mwongozo wa kiungu kwa ajili ya maisha yetu.

Yohana 1:4–10.Ni kwa jinsi gani unaweza kusaidia familia yako kuvuta taswira ya kile wanachosoma kuhusu nuru katika mistari hii? Ungeweza kuwaacha wanafamilia kupeana zamu kumulika nuru katika chumba chenye giza na kushiriki jinsi Mwokozi alivyo Nuru ya maisha yao. Kisha, mnaposoma Yohana 1:4–10, wanafamilia wanaweza kuwa na umaizi wa ziada kwenye ushuhuda wa Yohana juu ya Yesu Kristo, Nuru ya Ulimwengu.

Yohana 1:35–36.Kwa nini Yohana Mbatizaji amemwita Yesu “Mwanakondoo wa Mungu”? Je, Tunajifunza nini kuhusu hili jina kutoka kwenye ujumbe wa Mzee Jeffrey R. Holland “Tazama Mwanakondoo wa Mungu” au ujumbe wa Mzee Gerrit W. Gong “Mchungaji Mwema, Mwanakondoo wa Mungu”? (Liahona, Mei 2019, 44–46, 97–101.)

Yohana 1:35–46.Ni nini yalikuwa matokeo ya ushuhuda wa Yohana? Familia yako inaweza kujifunza nini kutoka kwa watu walioelezewa katika mistari hii kuhusu jinsi ya kushiriki injili? Ona pia video “Inviting Others to ‘Come and See’” (ChurchofJesusChrist.org).

Yohana 1:45–51.Ni nini Nathanaeli alifanya kilichomsaidia kupata ushuhuda juu ya Mwokozi? Waalike wanafamilia kuongea kuhusu jinsi walivyopata shuhuda zao.

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “The Lord Is My Light,” Nyimbo za Kanisa, na. 89.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Shiriki masomo ya vitendo. Waalike wanafamilia kutafuta vitu ambavyo wanaweza kutumia ili kuwasaidia kuelewa kanuni zinazopatikana katika maandiko mnayosoma kama familia. Kwa mfano, wanaweza kutumia mshumaa kuwakilisha Nuru ya Kristo (ona Yohana 1:4).

Picha
Yesu Kristo akiumba dunia.

Yehova Anaumba Dunia, na Walter Rane

Chapisha