Agano Jipya 2023
Januari 9–15. Mathayo 2; Luka 2: Tumekuja Kumsujudia


“Januari 9–15. Mathayo 2; Luka 2: Tumekuja Kumsujudia,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

“Januari 9–15. Mathayo 2; Luka 2,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023

Picha
Mamajusi wakisafiri kwa ngamia.

Acha Tumwabudu, na Dana Mario Wood

Januari 9–15

Mathayo 2; Luka 2

Tumekuja Kumsujudia

Unaposoma Mathayo 2 na Luka 2, kuwa makini na umaizi wowote wa kiroho unaopokea. Mawazo ya kujifunza katika muhtasari huu yanaweza kukusaidia kutambua kanuni muhimu na husika katika sura hizi.

Andika Misukumo Yako

Toka siku ya kuzaliwa Kwake, ilikuwa wazi kwamba Yesu hakuwa mtoto wa kawaida. Haikuwa tu nyota mpya mbinguni au tangazo la shangwe la kimalaika ambalo lilifanya utoto mchanga wa Yesu kuwa wa kipekee. Ilikuwa pia kweli kwamba makundi haya tofauti ya watu waaminifu—kutoka mataifa tofauti, taaluma, na historia—yalijisikia mara moja kuvutwa Kwake. Hata kabla Yeye hajatamka mwaliko Wake wa “njoo, unifuate,” wao walikuja (Luka 18:22). Si kila mmoja alikuja Kwake, ndiyo. Kulikuwa na wengi ambao hawakumjali Yeye, na mtawala mwenye wivu hata alitafuta uhai Wake. Lakini wanyenyekevu, wasafi, wenye kuitafuta haki kwa bidii walimwona Yeye kwa kile alichokuwa—Masiya wao aliyeahidiwa. Bidii yao hutia msukumo bidii yetu, kwani “habari njema ya furaha kuu” iliyoletwa kwa wachungaji ilikuwa kwa “watu wote,” na “Mwokozi, ambaye ni Kristo Bwana” alizaliwa siku ile kwetu sisi sote (ona Luka 2:10–11).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Luke 2:1–7

Yesu Kristo alizaliwa katika mazingira duni.

Japokuwa Yesu Kristo alikuwa na utukufu na Mungu Baba “kabla ya ulimwengu kuwako” (Yohana 17:5), Alikuwa tayari kuzaliwa katika mazingira ya chini na kuishi kati yetu duniani. Unaposoma Luka 2:1–7, tafakari kile ambacho taarifa hii kuhusu kuzaliwa Kwake inatufundisha kumhusu Yeye. Jaribu kutambua maelezo au umaizi katika hadithi hii ambao hukuutambua awali. Ni kwa jinsi gani kutambua vitu hivi huathiri hisia zako Kwake?

Ona pia “The Christ Child” (video), ChurchofJesusChrist.org.

Mathayo 2:1–12; Luka 2:8–38

Kuna mashahidi wengi wa kuzaliwa kwa Kristo.

Kuzaliwa na utoto mchanga wa Kristo vilitambulika kwa mashahidi na waabuduo kutoka matabaka mengi ya maisha. Unapochunguza kwa undani hadithi zao, unajifunza nini kuhusu njia za kuabudu na kumshuhudia Kristo?

Mashahidi wa Kristo

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kumshuhudia Kristo?

Mashahidi wa Kristo

Wachungaji (Luka 2:8–20)

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kumshuhudia Kristo?

Mashahidi wa Kristo

Simioni (Luka 2:25–35)

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kumshuhudia Kristo?

Mashahidi wa Kristo

Hana (Luka 2:36–38)

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kumshuhudia Kristo?

Mashahidi wa Kristo

Mamajusi (Mathayo 2:1–12)

Ninajifunza nini kuhusu kuabudu na kumshuhudia Kristo?

Ona pia 1 Nefi 11:13–23; 3 Nefi 1:5–21; “Shepherds Learn of the Birth of Christ” na “The Christ Child Is Presented at the Temple” (video), ChurchofJesusChrist.org.

Mathayo 2:13–23

Wazazi wanaweza kupokea ufunuo ili kuzilinda familia zao.

Yusufu kamwe asingeweza kufanya kile alichotakiwa kufanya—kumlinda Yesu katika utoto Wake—bila msaada wa mbinguni. Kama Mamajusi, alipokea ufunuo ambao ulimuonya dhidi ya hatari. Unaposoma kuhusu uzoefu wa Yusufu katika Mathayo 2:13–23, fikiria kuhusu hatari za kimwili na kiroho ambazo hutukabili leo. Tafakari uzoefu wakati ulipohisi mwongozo wa Mungu katika kukulinda wewe na wapendwa wako. Fikiria kushiriki uzoefu huu na wengine. Unaweza kufanya nini kupokea mwongozo kama huo siku za baadaye?

Kwa kuongezea, unaweza kufikiria kuangalia video “The First Christmas Spirit” (Churchof JesusChrist.org) kwa ufafanuzi wa namna gani Yusufu anaweza kuwa alihisi alipokabiliwa na changamoto ya kumtunza Mwana wa Mungu.

Luka 2:40–52

Hata alipokuwa kijana, Yesu alizingatia kwenye kutenda mapenzi ya Baba Yake.

Kama kijana mdogo, Mwokozi alifundisha injili kwa nguvu kwamba hata walimu hekaluni walishangazwa na “uelewa na majibu” Yake (Luke 2:47). Unajifunza nini kutoka kwenye mistari hii kuhusu Mwokozi akiwa kijana mdogo? Ni kwa jinsi gani vijana unaowajua wanajaribu “kuwamo katika kazi ya Baba [yao]”? (Luka 2:49). Ni kwa jinsi gani vijana na watoto wamekusaidia kupata uelewa wa kina wa injili? Nini kingine unajifunza kutoka kwenye mfano wa utoto wa Yesu katika Luka 2:40–52 na katika Tafsiri ya Joseph Smith, Mathayo 3:24–26 (katika kiambatisho cha Biblia)?

Picha
Yesu akiwa mvulana pamoja na walimu hekaluni

“Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika kazi ya Baba yangu?” (Luka 2:49).

Tafsiri ya Joseph Smith ni Nini?

Kwa sababu kweli “nyingi rahisi na za thamani” zilipotea kutoka kwenye Biblia kwa karne nyingi (1 Nefi 13:28; ona pia Musa 1:41), Bwana alimuamuru Joseph Smith kufanya masahihisho ya Biblia yenye mwongozo wa kiungu, yajulikanayo kama Tafsiri ya Joseph Smith. Masahihisho mengi yaliyofanywa na Nabii yamejumuishwa kwenye kiambatisho cha toleo la maandiko ya Watakatifu wa Siku za Mwisho. Tafsiri ya Joseph Smith Mathayo 24, ijulikanayo kama Joseph Smith—Mathayo, inaweza kupatikana katika Lulu ya Thamani Kuu. Kwa maelezo zaidi, ona “Tafsiri ya Joseph Smith (TJS)” katika Kamusi ya Biblia na makala ya Mada za Injili “Biblia, Uhakika wa” (topics.ChurchofJesusChrist.org).

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Luka 2.Waalike wanafamilia kumchagua mtu aliyeelezewa katika Luka 2, wasome mistari michache kuhusu miingiliano ya mtu huyo na Mwokozi, na washiriki kitu ambacho wamejifunza ambacho huongeza imani yao katika Yesu Kristo. Imbeni pamoja “Mary’s Lullaby”, au “The Nativity Song” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 44–45, 52–53). Unajifunza nini kutoka kwenye nyimbo hizi kuhusu kuzaliwa kwa Mwokozi?

Fikiria jinsi mchoro unavyoweza kuboresha majadiliano yenu kuhusu kuzaliwa kwa Kristo. (Kwa ajili ya mifano, ona Kitabu cha Sanaa ya Injili au history.ChurchofJesusChrist.org/exhibit/birth-of-Christ.)

Mathayo 2:1–12.Unajifunza nini kuhusu kumtafuta na kumpata Mwokozi kutoka kwenye mfano wa Mamajusi?

Luka 2:41–49.“Kazi ya Baba” ni ipi? (Luka 2:49; ona Musa 1:39; Kitabu cha Maelezo ya Jumla: Kuhudumu katika Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho1.2, ChurchofJesusChrist.org). Je, tunajifunza nini kuhusu kazi hiyo kutokana na hadithi hiyo katika Luka 2:41–49? Fikiria kuandika baadhi ya njia ambazo kwazo familia yako inaweza kushiriki katika kazi ya Baba na kuziweka katika chupa kubwa. Wiki inayofuata, familia yako inapotafuta njia za kusaidia katika kazi ya Baba wa Mbinguni, wanaweza kuchagua mawazo kutoka kwenye chupa kubwa. Panga muda ambapo mtashiriki uzoefu wenu.

Luka 2:52.Tunaweza kujifunza nini kutoka Luka 2:52 kuhusu jinsi Yesu alivyoendelea katika maisha Yake? Ni malengo gani binafsi na ya familia tunaweza kuweka ili kuongezeka “katika hekima na kimo, na kumpendeza Mungu na wanadamu”?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa “Stars Were Gleaming,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 37.

Kuboresha Kujifunza Binafsi.

Tumia visaidizi vya kujifunza maandiko. Ili kupata umaizi wa ziada unapojifunza maandiko, tumia nyenzo kama vile tanbihi, Mwongozo wa Mada, Kamusi ya Biblia, Mwongozo wa Maandiko, na visaidizi vingine vinavyopatikana katika ChurchofJesusChrist.org.

Picha
Mariamu, Yusufu, na mtoto mchanga Yesu

Mwokozi wa Ulimwengu alikuja duniani katika mazingira duni.

Chapisha