Agano Jipya 2023
Desemba 26–Januari 1. Tunawajibika kwa Kujifunza Kwetu Wenyewe


Desemba 26–Januari 1. Tunawajibika kwa Kujifunza Kwetu Wenyewe,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano Jipya 2023 (2022)

Desemba 26–Januari 1. Tunawajibika kwa Kujifunza Kwetu Wenyewe,” Njoo Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2023

Picha
familia ikitazama picha katika albamu

Desemba 26–Januari 1

Tunawajibika kwa Kujifunza Kwetu Wenyewe

Madhumuni ya Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia ni kuwasaidia kuja kwa Kristo na kuwa waongofu zaidi katika injili Yake. Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia inaweza kuwasaidia kuelewa maandiko na kupata ndani yake nguvu ya kiroho mnayohitaji wewe na familia yako. Kisha, katika madarasa yenu Kanisani, mtakuwa na nafasi za kushiriki umaizi na kuwahimiza Watakatifu wenzenu katika juhudi zao za kumfuata Kristo.

Andika Misukumo Yako

“Mnatafuta nini?” Yesu aliwauliza wafuasi wa Yohana Mbatizaji (Yohana 1:38). Unaweza kujiuliza swali hilo hilo—kwani kile unachopata katika Agano Jipya mwaka huu kwa kiasi kikubwa kitategemea kile unachotafuta. “Tafuteni, nanyi mtaona” ni ahadi ya Mwokozi (Mathayo 7:7). Kwa hivyo uliza maswali yanayokuja akilini mwako wakati unapojifunza, na kisha tafuta majibu kwa bidii. Katika Agano Jipya utasoma kuhusu uzoefu wa kiroho wenye nguvu wa wafuasi wa Yesu Kristo. Kama mfuasi mwaminifu wa Mwokozi, unaweza kuwa na uzoefu wako wenye nguvu wa kiroho unapokubali mwaliko wa Mwokozi, unaopatikana kote kwenye chuo hiki kitakatifu, “Njoo, unifuate” (Luka 18:22).

Picha
ikoni ya kujifunza binafsi

Mawazo kwa Ajili ya Kujifunza Binafsi Maandiko

Ili kujifunza kweli kutoka kwa Mwokozi, ni lazima mimi nikubali mwaliko Wake, “Njoo, unifuate.”

Mwaliko wa Mwokozi, “Njoo, Unifuate,” ni kwa wote—iwe sisi ni wapya kwenye njia ya ufuasi au tumeitembea maisha yetu yote. Huu ulikuwa ni mwaliko Wake kwa kijana mdogo tajiri ambaye alikuwa akijitahidi kushika amri (ona Mathayo 19:16–22; Luka 18:18–23). Kitu alichojifunza kijana huyu—na ambacho sote lazima tujifunze—ni kwamba kuwa mfuasi humaanisha kutoa nafsi zetu zote kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Tunaendelea katika ufuasi wetu tunapotambua kile tunachokosa, kufanya mabadiliko, na kutafuta kwa ukamilifu zaidi kuwafuata Wao.

Kujifunza kutoka kwa Mwokozi huanza tunapojitahidi kuelewa kile Yeye alichofundisha. Kwa mfano, ni kwa jinsi gani uelewa wako kuhusu unyenyekevu unaongezeka unapochunguza yafuatayo?

Kama unataka kujifunza zaidi, jaribu shughuli hii pamoja na kanuni nyingine ya injili, kama vile upendo au msamaha.

Ninawajibika kwa kujifunza kwangu mwenyewe.

Mzee David A. Bednar alifundisha: “Hatupaswi kutegemea Kanisa kama taasisi ya kutufundisha au kutuambia kila kitu tunachohitaji kujua na kufanya ili kuwa wafuasi waaminifu na kuvumilia kwa ujasiri mpaka mwisho. Badala yake, jukumu letu binafsi ni kujifunza kile tunachopaswa kujifunza, kuishi kama tunavyojua tunapaswa kuishi, na kuwa yule ambaye Bwana angetaka tuwe. Na nyumba zetu ni mazingira ya msingi kwa ajili ya kujifunza, kuishi, na kuwa” (“Kujiandaa Kupata Kila kitu Kinachohitajika,” Liahona, Mei 2019, 102).

Inamaanisha nini kuwajibika kwa kujifunza kwako wewe mwenyewe? Tafuta yanayowezekana kuwa majibu katika maelezo ya Mzee Bednar na katika maandiko yafuatayo: Yohana 7:17; 1 Wathesalonike 5:21; Yakobo 1:5–6, 22; 2:17; 1 Nefi 10:17–19; 2 Nefi 4:15; Alma 32:27; na Mafundisho na Maagano 18:18; 58:26–28; 88:118. Je, unajisikia kuongozwa kufanya nini ili kujishughulisha zaidi katika kujifunza injili?

Nahitaji kujua ukweli mimi mwenyewe.

Pengine unawajua watu ambao kamwe hawaonekani kupoteza imani yao, bila kujali kinachotokea katika maisha yao. Wanaweza kukukumbusha kuhusu wanawali watano wenye busara katika fumbo la Mwokozi (ona Mathayo 25:1–13). Ambacho unaweza usikione ni jitihada zao za bidii katika kuimarisha shuhuda zao juu ya ukweli.

Je, ni kwa jinsi gani tunapata na kukuza shuhuda zetu wenyewe? Andika mawazo yako wakati unapotafakari maandiko yafuatayo: Luka 11:9–13; Yohana 5:39; 7:14–17; Matendo 17:10–12; 1 Wakorintho 2:9–11; na Alma 5:45–46. (Ona pia Mada za Injili, “Ushuhuda,” topics.ChurchofJesusChrist.org.)

Picha
msichana kando ya njia

Kila mmoja wetu lazima apate ushuhuda wake mwenyewe.

Je, ninapaswa kufanya nini ikiwa nina maswali?

Unapotafuta ufahamu wa kiroho, maswali yatakujia akilini mwako. Kanuni zifuatazo zinaweza kukusaidia kushughulikia maswali katika njia zinazojenga imani na ushuhuda:

  • Kutafuta uelewa kutoka kwa Mungu. Mungu ni chanzo cha ukweli wote, na Yeye anafunua ukweli kupitia Roho Mtakatifu, maandiko, na manabii na mitume Wake.

  • Tenda kwa Imani. Kama majibu hayaji mara moja, amini kwamba Bwana atakufunulia majibu kwa wakati sahihi. Kwa wakati huu, endelea kuishi kwa ukweli ambao tayari unaujua.

  • Shikilia mtazamo wa milele. Jaribu kuona mambo kama Bwana anavyoyaona, si kama ulimwengu unavyoyaona. Yatazame maswali yako katika muktadha wa mpango wa wokovu wa Baba yetu wa Mbinguni.

Picha
ikoni ya kujifunza kama familia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko kama Familia na Jioni ya Nyumbani

Mathayo 13:1–23.Ili kusaidia familia yako kujiandaa kujifunza kutoka katika Agano Jipya mwaka huu, mnaweza kusoma fumbo la mpanzi. Familia yako inaweza kufurahia kwenda nje na kutafuta aina tofauti za udongo zilizoelezewa katika fumbo. Je, ni kwa jinsi gani tunaweza kuifanya mioyo yetu kuwa kama “udongo mzuri” Yesu aliouelezea? (Mathayo 13:8).

Wagalatia 5:22–23; Wafilipi 4:8.Rais Russell M. Nelson alikualika “kuigeuza nyumba [yako] kuwa mahali patakatifu pa imani na “kuirekebisha nyumba yako kuwa kituo cha kujifunza injili.” Kwa wale ambao wanafanya vitu hivi, yeye ameahidi: “WatotoWako watahamasika kujifunza na kuishi mafundisho ya Mwokozi, na ushawishi wa adui katika maisha yako na katika nyumba yako utapungua. Mabadiliko katika familia yako yatakuwa ya kuvutia na endelevu” (“Kuwa Mtakatifu wa Siku za Mwisho wa Mfano,” Liahona, Nov. 2018, 113).

Mwanzo wa mwaka ni wakati mzuri kufanya baraza la familia kuhusu kuifanya nyumba yenu iwe “kimbilio la imani” na “kitovu cha kujifunza injili”. Je, ni mawazo gani kuhusu jinsi ya kufanya haya huja akilini unaposoma Wagalatia 5:22–23 na Wafilipi 4:8? Pengine familia yako ingeweza kuweka malengo binafsi na ya familia ya kujifunza Agano Jipya mwaka huu unaokuja. Tunaweza kufanya nini ili kujikumbusha wenyewe juu ya malengo yetu?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kuwafundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Wimbo uliopendekezwa: “Teach Me to Walk in the Light,” Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 177.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Tafuta mafundisho. Mafundisho ya injili ni ukweli usiobadilika milele. Rais Boyd K. Packer alitangaza kwamba “fundisho la kweli, lililoeleweka, hubadili mitazamo na tabia” (“Watoto Wadogo,” Ensign, Nov. 1986,17). Pale wewe na familia yako mnapojifunza maandiko, tafuta kweli ambazo zitawasaidia kuishi zaidi kama Mwokozi.

Picha
Yesu Kristo

Nuru ya Ulimwengu, na Brent Borup

Chapisha