Agano Jipya 2023
Januari 30–Februari 5. Mathayo 4; Luka 4–5: “Roho wa Bwana Yu juu Yangu”


“Januari 30 –Februari 5 Mathayo 4; Luka 4–5: ‘Roho wa Bwana Yu juu Yangu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022)

“Januari 30–Februari 5 Mathayo 4; Luka 4–5,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
Yesu amesimama nyikani

Nyikani, na Eva Koleva Timothy

Januari 30–Februari 5

Mathayo 4; Luka 4–5

“Roho wa Bwana Yu juu Yangu”

Unapojifunza Mathayo 4 na Luka 4–5, andika misukumo yako ya kiroho. Hii itakaribisha mwongozo wa kiungu juu ya njia bora ya kukidhi mahitaji ya darasa lako. Unaweza pia kufikiria kutumia Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia vile vile muhtasari huu ili kupata mawazo ya ziada.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Kusoma kwa wiki hii kunajumuisha maelezo haya: “Wakashangaa mno kwa mafundisho yake: kwa kuwa neno lake lilikuwa na nguvu” (Luka 4:32; ona pia Marko 1:22). Waalike washiriki wa darasa kushiriki mistari hii kutoka Mathayo 4 na Luka 4–5 ambayo imewasaidia kuhisi nguvu hiyo wao wenyewe.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mathayo 4:1–11; Luka 4:1–13

Baba wa Mbinguni ametupa sisi nguvu na mbinu ya kuyashinda majaribu.

  • Tukio la Mwokozi la kumshinda Shetani linaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kutambua njia ambazo Shetani anajaribu kuwajaribu. Washiriki wa darasa wanaweza kuchagua mojawapo ya majaribu katika Mathayo 4:1–14 au Luka 4:1–13 na wafikirie kuhusu majaribu ya kisasa, yaliyo sawa na hayo (maelezo katika “Nyenzo za Ziada” yanaweza kusaidia). Kwa nini inasaidia kujua kwamba Mwokozi alikabiliana na majaribu sawa na hayo tunayokabiliana nayo leo? Kwa nini Kristo aliweza kushinda majaribu? Kwa ajili ya mifano mingine ya kimaandiko ya watu wakimshinda Shetani, ona Mwanzo 39:7–20; 2 Nefi 4:16–35; na Musa 1:10–22.

  • Ni nini kingesaidia darasa lako kuyashinda majaribu? Ungeweza kuwaomba kurejelea Mathayo 4:1–11 au Luka 4:1–13 ili kujifunza maarifa ya Mwokozi juu ya maandiko yalivyomsaidia Yeye kumjibu Shetani, kama alivyofanya wakati aliposema, “Imeandikwa.” Wape washiriki wa darasa muda wa kutafuta neno “Majaribu” katika Mwongozo wa Mada kwa ajili ya maandiko ambayo yangeweza kuwalinda na kuwaimarisha wanapohisi kujaribiwa.

Luka 4:16–32

Yesu Kristo ndiye Masiya aliyetolewa unabii.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa lako kuelewa vyema hadithi hii katika Luka 4:16–32, unaweza kuelezea kwamba majina Masiya na Kristo yote yanamaanisha “mpakwa mafuta.” Washiriki wa darasa wanaposoma Luka 4:18–21, waombe wafikirie kuhusu kile inachomaanisha kusema kwamba Yesu ndiye Kristo, Masiya au Mpakwa Mafuta. Wanaweza pia kuona inasaidia kusoma “Mpakwa Mafuta” katika Kamusi ya Biblia. Ni kwa jinsi gani Yesu anatangaza kwamba Yeye ni Masiya hivi leo? Waalike washiriki wa darasa kushiriki jinsi walivyokuja kujua kwamba Yesu Kristo ni Mwokozi wao.

  • Inawezekana yakawepo masomo mengine yanayosaidia kujifunza kwa kutafiti kwa nini watu wa Nazareti hawakumkubali Yesu kama Masiya aliyetolewa unabii. Je, ni sababu zipi, kwa mfano, zinapendekezwa katika Luka 4:22 –24? Washiriki wa darasa wangeweza kulinganisha sifa hizi na zile za mjane wa Sarepta na Naamani katika Agano la Kale, watu ambao hawakuwa Waisraeli (ona Luka 4:25–27). Unaweza kuwasiliana na baadhi ya washiriki wa darasa mapema na uwaombe waje kama wamejiandaa kufanya muhtasari wa kila mojawapo ya matukio haya (ona 1 Wafalme 17:8–24; 2 Wafalme 5:1–17; Luka 4:16–30). Je, virai hivi vinatufundisha nini kuhusu kuwa na imani katika Yesu Kristo? Je, tunaona jumbe zozote kwa ajili yetu sisi katika maneno ya Mwokozi kwa watu wa Nazarethi?

Mathayo 4:18–22; Luka 5:1–11

Kumfuata Yesu Kristo kunamaanisha kuacha mapenzi yetu na kuyakubali Yake.

  • Wakati mwingine maelekezo anayotupa Bwana hayaleti maana mwanzoni. Washiriki wa darasa wanaweza kupekua Luka 5:1–11, wakitafuta kile Mwokozi alichomwuliza Petro na ni kwa nini Petro yawezekana alitia shaka maelekezo Yake. Ni kwa jinsi gani uzoefu huu waweza kuwa uliathiri mtazamo wa Petro kuhusu Mwokozi na yeye mwenyewe? Ungeweza kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki uzoefu ambao walionyesha imani yao katika mwongozo mtakatifu licha ya kutokuwa na uelewa kamili. Matokeo yalikuwaje wakati walipoitumia imani yao?

    Picha
    Yesu akiwaita Petro na Andrea kando ya bahari

    “Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu” (Mathayo 4:19).

  • Kama vile tu wavuvi “waliacha vyote” ili kumfuata Yesu Kristo(Luke 5–11), kuna vitu ambavyo tunapaswa kuviacha ili tuwe wanafunzi Wake. Tunajifunza nini kutoka Mathayo 4:18–22 kuhusu mitazamo na imani ya Petro, Andrea, Yakobo na Yohana? Yawezekana ikawa ya msaada kuleta nyavu ya samaki darasani. Waalike washiriki wa darasa kuandika vitu walivyotayari kuviacha au tayari wameviacha ili kumfuata Kristo na uviweke kwenye wavu. Fikiria kuwaalika washiriki wachache wa darasa kushiriki jinsi maisha yao yalivyobadilika kwa vile wamechagua kuacha vyote na kumfuata Mwokozi.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Aina za majaribu.

Baada ya kuzungumzia aina za majaribu ambayo Mwokozi alipambana nayo nyikani, Rais David O. McKay alibainisha aina tatu za majaribu:

“(1) Jaribu la hamu au shauku;

“(2) Kuruhusu kiburi, mtindo au majivuno;

“(3) Tamaa ya utajiri wa kiulimwengu au mamlaka na utawala juu ya nchi au milki za kidunia za wanadamu” (Teachings of Presidents of the Church: David O. McKay [2003], 82).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Washukuru wanafunzi wako. “Usizame sana kwenye somo kiasi cha kusahau kuwashukuru wanafunzi kwa michango yao. Wanahitaji kujua ya kwamba unathamini utayari wao wa kushiriki umaizi na shuhuda zao” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 33).

Chapisha