Agano Jipya 2023
Februari 6–12. Yohana 2–4: “Hamna Budi Kuzaliwa Mara ya Pili”


“Februari 6–12. Yohana 2–4: ‘Hamna Budi Kuzaliwa Mara ya Pili’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022.)

“Februari 6–12. Yohana 2–4 “ Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
Yesu anazungumza na Nikodemo

Februari 6–12

Yohana 2–4

“Hamna Budi Kuzaliwa Mara ya Pili”

Kusoma Yohana 2–4 ni njia nzuri ya kuanza kujiandaa kufundisha. Andika misukumo yoyote ya kiroho unayopokea, na tumia muhtasari huu kutafuta umaizi wa ziada na mawazo ya kufundisha.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Andika vichwa vya habari vitatu ubaoni: Yohana 2 , Yohana 3 , na Yohana 4 . Washiriki wa darasa wangeweza kuchukua dakika chache kurejelea sura hizi na kisha waandike chini ya kila kichwa cha habari aya ambayo iliwasaidia kuelewa maandiko na matukio katika sura hiyo. Jadili mistari waliyoandika.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Yohana 2:1–11

Miujiza ya Yesu Kristo “ilidhihirisha utukufu Wake.”

  • Muhtasari wa wiki hii katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia unapendekeza kusoma Yohana 2:1–11 kutoka kwenye mtazamo wa mtu aliyekuwepo wakati Yesu alipogeuza maji kuwa divai. Pengine washiriki wa darasa wangeweza kuelezea utambuzi waliopata kutokana na kufanya hivyo. Je, tunajifunza nini kuhusu Mwokozi kutoka kwenye mistari hii? Ni kwa jinsi gani muujiza huu unadhihirisha utukufu wa Mungu? (ona mstari wa 11).

Yohana 2:13–22

Tunaweza kutetea sehemu na vitu vitakatifu.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kujifunza kutokana na hadithi hii ya Yesu kuwafukuza nje wabadilisha fedha kutoka ndani ya hekalu, ungeweza kuwaomba wafikirie vitu vingine, zaidi ya hekalu, ambavyo Bwana anavichukulia kuwa ni vitakatifu. Ni kwa jinsi gani tunaweza kusaidia kulinda utakatifu wa vitu hivi?

Yohana 3:1–21

Hatuna budi kuzaliwa mara ya pili ili tuingie katika ufalme wa Mungu.

  • Jinsi gani tunaweza kuelezea kwa mtu mwingine kile inachomaanisha kuzaliwa mara ya pili? Fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kufanya mazoezi jinsi ambavyo wangemjibu swali hili na mtu aliyekaa karibu nao. Wanapofanya hivyo, wangeweza kujadiliana wao kwa wao maswali kama haya: Je tunajifunza nini kutokana na maneno ya Yesu katika Yohana 3:3–7? Ni kwa jinsi gani toba, ubatizo na kuthibitishwa kunatusaidia sisi kuzaliwa mara ya pili? Maelezo katika “Nyenzo za Ziada” yangeweza kuongezea katika majadiliano.

  • Baadhi ya watu wanaamini kwamba hakika mtu hawezi kubadilika. Nikodemo, hata hivyo, ni mfano wa mtu aliyebadilika kama matokeo ya kuifuata injili ya Yesu Kristo. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuona hili, waalike kupekua Yohana 3: 1–2; Yohana 7:45–52; Yohana 19: 38–40. Tunajifunza nini kutoka katika vifungu hivi kuhusu mtazamo na imani ya Nikodemo? Alibadilika vipi baada ya muda? Ni mifano gani tunayoweza kushiriki kuhusu watu tunaowajua ambao wamebadilika kwa sababu ya injili?

Yohana 4:5–34

Yesu Kristo anatoa kwetu “maji ya uzima” na “chakula” kwa ajili ya kufanya kazi ya Mungu.

  • Miili yetu inahitaji chakula na maji kila siku. Yesu alirejea haya mahitaji ya kiulimwengu wakati alipofundisha kwa mwanamke Msamaria na wafuasi Wake (ona Yohana 4:5–34). Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa kile Mwokozi alichokuwa anafundisha, unaweza kubandika picha za chakula na maji ubaoni na uwaalike washiriki wa darasa kuandika chini ya kila picha kweli kuhusu chakula cha kiroho na maji ambavyo Yesu alifundisha. Je, ni kwa namna gani Mwokozi anatuliza njaa ya kiroho na kiu ya kiroho?

    Picha
    Kijito cha maji

    Yesu Kristo anatupatia maji ya uzima.

  • Kutafakari juu ya maendeleo ya ushuhuda wa mwanamke Msamaria juu ya Yesu Kristo kunaweza kuwasaidia washiriki wako wa darasa kutafakari jinsi walivyoweza kuja kujua kuwa Yeye ni Masiya. Kama darasa, watafute istilahi mwanamke Msamaria aliyotumia kumrejelea Mwokozi katika Yohana 4:6–30. Je, istilahi hizi zinadokeza nini kuhusu uelewa wake wa Yesu ni nani? Ni kwa jinsi gani sisi tumekua katika shuhuda zetu kwamba Yeye ni Mwokozi wetu?

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Inamaanisha nini kuzaliwa mara ya pili.

Mzee David A. Bednar alifundisha: “Uongofu … una nguvu sana, sio hafifu—kuzaliwa tena kiroho na mabadiliko ya msingi ya kile tunachohisi na kutamani, kile tunachofikiria na kufanya na vile tulivyo. Kwa kweli, kiini hasa cha injili ya Yesu Kristo kinajumuisha mabadiliko ya msingi na ya kudumu katika asili yetu yanayowezeshwa kupitia utegemezi wetu kwenye ‘fadhili, na rehema, na neema ya Masiya Mtakatifu’ (2 Nefi 2:8). Tunapochagua kumfuata Bwana, tunachagua kubadilishwa—kuzaliwa tena kiroho” (“Ye Must Be Born Again,” Liahona, May 2007, 20).

Rais Dallin H. Oaks alifundisha “Tulizaliwa mara ya pili wakati tulipoingia katika uhusiano wa agano na Mwokozi kwa kuzaliwa kwa maji na kwa Roho na kwa kujichukulia juu yetu jina la Yesu Kristo. Tunaweza kurudia kuzaliwa huko upya kila siku ya Sabato wakati tunapokula sakramenti. Watakatifu wa Siku za Mwisho wanakiri kwamba wale waliozaliwa mara ya pili katika njia hii ni wana na mabinti wa Yesu Kristo (ona Mosia 5:7; 15:9–13; 27:25). Hata hivyo, ili tupate baraka zilizokusudiwa kwa hali hii ya kuzaliwa mara ya pili, lazima bado tushike maagano yetu na kuvumilia hadi mwisho” (“Have You Been Saved?,” Ensign, Mei 1998, 56).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Mwalimu sio bora kuliko mwanafunzi. Jukumu lako kama mwalimu ni muhimu, lakini wewe sio chanzo pekee cha mwongozo wa kiungu darasani. Wasaidie washiriki wa darasa kujifunza kutoka kwa Roho na washiriki na kila mmoja kile wanacho jifunza.

Chapisha