Agano Jipya 2023
Julai 17–23. Matendo ya Mitume 10–15: “Neno la Mungu Likazidi na Kuenea”


“Julai 17–23. Matendo ya Mitume 10–15: ‘Neno la Mungu Likazidi na Kuenea’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022)

“Julai 17–23. Matendo ya Mitume 10–15,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
Petro akiongea na Kornelio

Julai 17–23

Matendo ya Mitume 10–15

“Neno la Mungu Likazidi na Kuenea”

Kujifunza kwa maombi Matendo ya Mitume 10–15 kabla ya kusoma muhtasari huu kutakusaidia kupokea misukumo kutoka kwa Bwana. Mawazo hapa chini ni mapendekezo tu.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike washiriki wa darasa kushirikiana na yule waliyekaa karibu naye kitu ambacho Roho amewafundisha walipokuwa wakisoma Matendo ya Mitume 10–15. Alika wachache kuelezea umaizi wao kwa darasa zima.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Matendo ya Mitume 10; 11:1–18; 15:1–25

Baba Yetu wa Mbinguni hutufundisha mstari juu ya mstari kupitia ufunuo.

  • Baadhi ya washiriki wa darasa wanaweza kuwa na mawazo yasiyo sahihi kuhusu mchakato wa kupokea ufunuo. Inaweza kuwasaidia wao kujadili jinsi gani ufunuo ulikuja kwa Petro na jinsi gani wanaweza kusonga mbele, “bila shaka yoyote” (Matendo ya Mitume 10:20), wakati ufunuo unapoonekana kutokamilika au kutoeleweka. Fikiria kuchora mstari kwenye ubao na andika kwenye mwisho wa mstari Injili ifundishwe kwa Wayunani. Kama darasa, pitieni Matendo ya Mitume 10 na 11:1–18, na kisha muongeze vipengele kwenye mstari ambavyo vinaonyesha ni kwa namna gani Bwana alimfunulia Petro hatua kwa hatua kwamba muda ulikuwa umefika wa kuhubiri injili kwa Wayunani. Kwa mfano, ungeweza kuanza na kipengele kiitwacho “Kornelio aliona ono” (Matendo ya Mitume 10:1–6) au hata kuanza na amri ya Mwokozi kwa wanafunzi Wake “mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi” katika Mathayo 28:19. Tunaweza kujifunza nini kuhusu ufunuo kutokana na tukio la Petro? Je, mafundisho ya Nefi kuhusu ufunuo katika 2 Nefi 28:30 na mafundisho kutoka kwa Mzee David A. Bednar katika “Nyenzo za Ziada” yanaongeza nini katika uelewa wetu?

    Picha
    msichana akisoma maandiko

    Ufunuo binafsi mara nyingi huja baada ya muda na kupitia jitihada endelevu.

  • Unaweza kujifunza mifano kutoka kwenye maandiko ambamo ndani yake Bwana aliwafundisha watu mstari juu ya mstari. Kama nyongeza kwa uzoefu wa Petro katika Matendo ya Mitume 10, washiriki wa darasa wangeweza kurejea uzoefu wa Nefi (1 Nefi 18:1–3); Alma (Alma 7:8; 16:20); na Mormoni (3 Nefi 28:17, 36–40). Ni mifano gani mingine washiriki wa darasa wanafikiria ambapo watu walipokea mwongozo wa kiroho “hapa kidogo na pale kidogo”? (2 Nefi 28:30). Ni kwa nini wakati mwingine Bwana anachagua kufunua mambo katika njia hii kuliko kutupatia majibu yote kwa wakati mmoja? (ona Mafundisho na Maagano 50:40; 98:12).

  • Wakati mwingine waumini wanakuwa na tatizo kuhusu mabadiliko katika sera au programu katika Kanisa. Ingeweza kuwasaidia wao kujadili jinsi gani ufunuo wa kuanza kufundisha injili kwa Wayunani (ona Matendo ya Mitume 10) ulichukua nafasi ya maelekezo ya awali ya Bwana kwa wanafunzi Wake (ona Mathayo 10:1, 5–6). Ungeweza kuonyesha video ya “The Jerusalem Conference” (ChurchofJesusChrist.org). Ni kwa namna gani washiriki wa darasa wangeweza kumjibu mmoja wa watu waliokuwepo wakati wa Petro ambaye hakukubaliana na maelekezo ya Petro kwa sababu yalipingana na tamaduni za awali? Ni kwa namna gani ufunuo katika Matendo ya Mitume 10 unatusaidia kufuata ufunuo endelevu wa Bwana kupitia Nabii Wake?

Matendo ya Mitume 10:9–48

“Mungu hana upendeleo.”

  • Je, washiriki wa darasa lako wangenufaika kutokana na majadiliano kuhusu kile kinachomaanishwa na “hana upendeleo”? Unaweza kuanza kwa kualika darasa kusoma maandiko ambayo yanafundisha kwamba Mungu hana upendeleo, kama vile Warumi 2:1–11; 1 Nefi 17:34–40; 2 Nefi 26:32–33; Alma 5:33; Moroni 8:12; na Mafundisho na Maagano 1:34–35. Waombe washiriki wa darasa kuandika maana yamkini za “hana upendeleo,” kulingana na kile wanachosoma, halafu waelezee kile walichoandika. Ni kwa namna gani matukio na kanuni katika Matendo ya Mitume 10:34–48 huonyesha kwamba Mungu hana upendeleo? Ni kwa namna gani mwenye haki “anakubaliwa” na “kupendelewa” na Mungu licha ya kwamba Yeye hana upendeleo? (ona Matendo ya Mitume 10:34–35; 1 Nefi 17:35).

    Unaweza kuhitajika kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa kwamba “hana upendeleo” haimaanishi kwamba Mungu humbariki kila mtu sawa sawa bila kujali matendo yetu. Yeye anataka watoto Wake wote waikubali injili, lakini utimilifu wa baraka za injili umetunzwa kwa ajili ya wale wanaofanya Naye maagano na kuyashika.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Kupokea ufunuo mstari juu ya mstari

Mzee David A. Bednar alifanya uchunguzi wa yafuatayo kuhusu njia ya Bwana ya ufunuo: “Wengi wetu hasa hudhani tutapokea jibu au mwongozo kutokana na sala zetu za dhati na maombi. Na pia mara nyingi tunategemea kwamba jibu au mwongozo vitakuja bila kuchelewa na kwa mara moja. Hivyo, tunakuwa wenye kuamini kwamba Bwana atatupatia jibu kubwa kwa haraka na yote kwa mara moja. Hata hivyo, mpangilio ambao umeelezewa mara kwa mara kwenye maandiko unapendekeza kwamba tupokee ‘amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni,’ au kwa maneno mengine majibu mengi madogo madogo kwa kipindi cha muda fulani. Kutambua na kuelewa mpangilio huu ni ufunguo muhimu katika kupata mwongozo wa kiungu na usaidizi kutoka kwa Roho Mtakatifu (“Mstari juu ya Mstari, Kanuni juu ya Kanuni,” New Era, Sept. 2010, 3–4).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Anza na maandiko. Kabla ya kugeukia nyenzo saidizi, kwa bidii jifunze maandiko ya kale na ya sasa. Kujifunza kwa maombi neno la Mungu kutamruhusu Roho akusaidie kukumbuka kile ambacho ulijifunza wakati unapofundisha. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi12.)

Chapisha