Agano Jipya 2023
Julai 24–30. Matendo ya Mitume 16–21: “Bwana Alituita kwa ajili ya Kuhubiri Injili”


“Julai 24–30. Matendo ya Mitume 16–21: ‘Bwana Alituita kwa ajili ya Kuhubiri Injili’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022)

“Julai 24–30. Matendo ya Mitume 16–21,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
Paulo akifundisha juu ya kilima

Julai 24–30

Matendo ya Mitume 16–21

“Bwana Alituita kwa ajili ya Kuhubiri Injili”

Kabla ya kuangalia muhtasari huu, kwa maombi soma Matendo ya Mitume 16–21 ukiwa na washiriki wa darasa lako akilini mwako. Mawazo yafuatayo yanaweza kuchangia katika mwongozo wa kiungu uliopokea kutoka kwa Roho.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kuelezea kifungu kutoka Matendo ya Mitume 16–21 ambacho kiliwakumbusha uzoefu ambao walikuwa nao wa kushiriki injili.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Matendo ya Mitume 16–21

Kama waumini wa Kanisa la Mwokozi, tunashuhudia juu Yake Yesu na kushiriki na wengine injili Yake.

  • Ujumbe mmoja maarufu kutoka katika Matendo ya Mitume 16–21 ni umuhimu wa Roho Mtakatifu katika kushiriki injili na wengine. Kwa mfano mmoja, washiriki wa darasa wangeweza kusoma kuhusu jinsi gani Roho Mtakatifu aliwasaidia Paulo na Sila katika Matendo ya Mitume 16:6–15. Kwa nini tunamhitaji Roho Mtakatifu wakati tunapofundisha injili? (ona 2 Nefi 33:1; Mafundisho na Maagano 33:8–10; 42:14; 100:5–8). Labda washiriki wa darasa wangeweza kushiriki uzoefu wao wakati Roho Mtakatifu alipoongoza jitihada zao za kushiriki injili.

  • Ni kwa namna gani uzoefu wa Paulo unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa lako kuwa na ujasiri wanapopata ushawishi wa kutoa shuhuda zao? Fikiria kumwomba kila mshiriki wa darasa kurejelea moja ya hadithi zifuatazo: Matendo ya Mitume 16:16–34; 17:16–34; 18:1–11. Waombe kuelezea ushahidi wanaopata juu ya uimara na ujasiri wa Paulo? Ni kweli gani Paulo alifundisha (na kuelewa) ambazo zilimpa kujiamini katika ujumbe wake? Je, ni kwa nini wakati mwingine sisi tunasita kushiriki injili na wengine, na ni kwa namna gani Mwokozi anatusaidia? Wahamasishe washiriki wa darasa kufikiria njia mojawapo wanayoweza kufuata mfano wa Paulo na kushiriki ushuhuda wao juu ya Kristo mara nyigi zaidi (video ya “I’ll Go Where You Want Me to Go” [ChurchofJesusChrist.org] inaweza kusaidia).

Matendo ya Mitume 17:16–34

Sisi ni wazao wa Mungu.

  • Katika kilima cha Maazi, Paulo alifundisha kuhusu Baba wa Mbinguni kwa kundi la watu ambao walikuwa na ufahamu mdogo kuhusu asili ya kweli ya Mungu. Ili kuchunguza zaidi mafundisho haya, washiriki wa darasa wangeweza kusoma Matendo ya Mitume 17:24–31 na kuandika ubaoni kweli ambazo wanapata kuhusu Baba wa Mbinguni, uhusiano wetu sisi na Yeye, na uhusiano baina yetu sisi kwa sisi. Wangeweza kisha kushiriki uzoefu ambapo walihisi ukweli wa maelezo ya Paulo kwamba Mungu “hayuko mbali na kila mmoja wetu” (aya 27).

  • Wakati mnapoangalia mistari hii kwa pamoja, fikiria kujadili ukweli uliofundishwa katika mstari wa 29, “Sisi tu wazao wa Mungu.” Ungeweza kuandika kwenye ubao Kwa kuwa sisi tu watoto wa Mungu, … na Kama tusingejua kuwa tu watoto wa Mungu, … Waalike washiriki wa darasa kukamilisha sentensi hizi. Kwa mfano, ukweli kuwa sisi tu watoto wa Mungu unatufundisha nini kuhusu sisi wenyewe na kuhusu jinsi gani tunavyotakiwa kuchukuliana sisi kwa sisi? Je, ni kwa jinsi gani maisha yetu yangekuwa tofauti kama tusingejua kuhusu uhusiano wetu wa kweli na Mungu? Je, maelezo ya Rais Dallin H. Oaks katika “Nyenzo za Ziada” yanaongezea nini katika mjadala huu?

    Picha
    Mtoto mchanga akiwa ameshikwa

    Kila mmoja wetu ni mtoto wa Mungu.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Sisi sote tu watoto wa Mungu.

Familia: Tangazo kwa Ulimwengu” inaelezea ukweli wa milele kuhusu uhusiano wetu na Mungu: “Binadamu wote—wa kiume na wa kike—wameumbwa kwa mfano wa Mungu. Kila mmoja ni mwana au binti mpendwa wa kiroho wa wazazi wa mbinguni, na, kama hivyo, kila moja ana asili takatifu na hatima ya kiungu”(ChurchofJesusChrist.org).

Rais Dallin H. Oaks wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alizungumzia kuhusu umuhimu wa sisi wenyewe kujiona kwanza na zaidi ya yote kama watoto wa kiroho wa Mungu:

“Kuwa makini na jinsi gani unavyojichukulia wewe mwenyewe. Usijichukulie au kujipambanua mwenyewe kwa sifa za kupita. Sifa moja pekee ambayo inapaswa kututambulisha sisi ni kwamba sisi tu wana au mabinti wa Mungu. Ukweli huu unazidi sifa zingine zote, ikijumuisha asili yetu, kazi, sifa za kimaumbile, heshima au hata ushirikishwaji wa kidini. …

“Tunayo haki yetu ya kujiamulia, na tunaweza kuchagua sifa yoyote ile kutuelezea. Lakini tunahitaji kujua kwamba tunapochagua kujielezea au kujipambanua kwa baadhi ya sifa ambazo ni za muda au zisizo halisi katika muktadha wa umilele, tunaacha kusisitiza kile ambacho ni muhimu juu yetu, na tunasisitiza zaidi kile ambacho si cha muhimu. Hii inaweza kutupeleka chini kwenye njia isiyo sahihi na kuzuia ukuaji wetu wa milele” (“Be Wise” [Brigham Young University–Idaho devotional, Nov.7, 2006], byui.edu).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Alika vijana kuwa sehemu ya somo lako. Kama unafundisha vijana, kumbuka kwamba mara nyingi wanaweza kuelewa vitu ambavyo marafiki zao wanapitia. Wakati kijana anapotoa ushuhuda au kufundisha mafundisho ya injili, vijana wengine wanaweza kuguswa katika njia ambayo huwezi kurudufu. Wape vijana fursa za kufundishana (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi28.)

Chapisha