Agano Jipya 2023
Juni 26–Julai 2. Mathayo 28; Marko 16; Luka 24; Yohana 20–21: “Amefufuka”


“Juni 26–Julai 2. Mathayo 28; Marko 16, Luka 24; Yohana 20–21: ‘Amefufuka’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022)

“Juni 26–Julai 2. Mathayo 28; Marko 16; Luka 24; Yohana 20–21,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili; 2023

Picha
Yesu Akiongea na Petro kwenye ufukwe wa bahari

Walishe Kondoo Wangu, na Kamille Corry

Juni 26–Julai 2

Mathayo 28; Marko 16; Luka 24; Yohana 20–21

“Amefufuka”

Kabla ya kuchunguza mawazo ya kufundisha katika muhtasari huu, soma Mathayo 28; Marko 16; Luka 24; Yohana 20–21, na utafakari jinsi sura hizi zinavyoweza kutumika kuimarisha imani ya wale unaowafundisha.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kushiriki kile walichojifunzaa katika kujifunza kwao binafsi na kama familia, waombe waandike ukweli kutoka katika somo lililopangwa wiki hii ambao wanahisi unapaswa kushirikishwa kwa “ulimwengu wote” (ona Marko 16:15). Mwisho wa darasa, waulize kama walipata kweli zo zote za nyongeza ambazo wangependa kushiriki.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Mathayo 28; Marko 16; Luka 24; Yohana 20

Kwa sababu Yesu alifufuka, sisi pia tutafufuliwa.

  • Unaweza kuwapa washiriki wa darasa dakika chache kurejea kazi ya kusoma waliyopangiwa wiki hii na “Ufufuko” katika Kamusi ya Biblia na kuandika kweli walizojifunza kuhusu Ufufuko. Waache wachache washiriki kile walichoandika, na wahimize washiriki wa darasa kuinua mikono yao wakati wanaposikia mtu fulani akishiriki ukweli ambao unafanana na ule walioandika. Kwa nini kweli hizi ni muhimu kwetu? Ni kwa jinsi gani unashawishi uhusiano wetu? Ni kwa jinsi gani unashawishi chaguzi zetu?

Luka 24:13–35

Tunaweza kumwalika Mwokozi “kukaa pamoja nasi.”

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuona uhusiano kati ya uzoefu wao na uzoefu wa wafuasi waliokuwa njiani kwenda Emau, chora njia ubaoni, na waombe washiriki wa darasa waandike maelezo kutoka kwenye hadithi katika Luka 24:13–35 upande mmoja wa barabara. Kisha, upande mwingine wa barabara, wanaweza kuandika milingano wanayoona kwenye uzoefu wao wenyewe kama wafuasi wa Yesu Kristo. Kwa mfano, wanaweza kuandika “Macho yao yalifumbwa” (Luka 24:16) upande mmoja wa barabara na Wakati mwingine hatutambui ushawishi wa Bwana katika maisha yetu upande mwingine. Tunawezaje kumwalika Mwokozi “kukaa pamoja nasi?

Picha
Kristo aliyefufuka akiwatokea Mitume

Yesu alimfundisha Tomaso, “Wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye” (Yohana 20:27).

Yohana 20:19–29

“Wa heri wale wasioona, wakasadiki.”

  • Darasa lako la Shule ya Jumapili linaweza kuwa mahali pa washiriki wa darasa kuimarishana imani zao katika vitu ambavyo hawavioni. Pengine unaweza kuanza kwa kumuomba mtu mmoja kufanya muhtasari wa tukio la Tomaso katika Yohana 20:19–29. Unaweza pia kuonyesha video “Blessed Are They That Have Not Seen, and Yet Have Believed” (ChurchofJesusChrist.org). Washiriki wa darasa wanaweza kuorodhesha ubaoni baadhi ya mambo ambayo Mungu anatutaka sisi tuamini bila kuyaona. Kisha unaweza kuwaomba washiriki uzoefu ambao umeimarisha shuhuda zao juu ya mambo haya na baraka ambazo zimewajia kwa kuwa wameifanyia kazi imani.

Yohana 21:1–17

Mwokozi anatualika tuwalishe Kondoo Wake.

  • Nini kinaweza kuwasaidia washiriki wa darasa lako kukubali mwaliko wa Mwokozi “kuwalisha kondoo [Wake]”? Unaweza kuanza kwa kuwaalika wasome Yohana 21:15–17 kimya kimya, wakibadilisha jina la Simioni na kuweka majina yao na “kondoo wangu” na majina ya watu wanaohisi Bwana anawataka wawahudumie—kwa mfano, watu wanaowatumikia, majirani au watu wanaowafahamu kazini au shuleni. Baada ya dakika chache, washiriki wa darasa wanaweza kushiriki misukumo waliyopata. Tunajifunza nini kuhusu Mwokozi kutokana na matendo Yake katika Yohana 21:4–13? Tunaweza kufanya nini ili kuwalisha wanakondoo na kondoo wa Mwokozi? Maelezo ya Mzee Gary E. Stevenson katika “Nyenzo za Ziada” yangeweza kusaidia kujibu swali hili.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Tunawezaje “kulisha kondoo [Wake]”?

Mzee Gary E. Stevenson alielezea jinsi tunavyoweza kutimiza amri ya Bwana ya kulisha kondoo Wake:

“Mchungaji ni nani? Kila mwanamume, mwanamke na mtoto katika ufalme wa Mungu ni mchungaji. Hakuna wito unaohitajika. Tangu wakati tunapotoka nje ya maji ya ubatizo, tunapewa wajibu kwenye kazi hii. Tunawafikia wengine kwa upendo kwa sababu hicho ndicho kile Mwokozi wetu ametuamuru kufanya. Wakati wowote majirani zetu wanapokuwa katika dhiki kimwili au kiroho, kwa haraka tutoe msaada. Tunabebeana mizigo ili iwe miepesi. Tunaomboleza na wale wanaoomboleza. Tunawafariji wale ambao wanahitaji faraja (ona Mosia 18: 8– 9). Bwana kwa upendo anategemea hili kutoka kwetu. Na siku itafika ambapo Atatuwajibisha kwa matunzo tunayotoa katika kulitumikia kundi Lake [ona Mathayo 25:31–46]” (“Kuchunga Nafsi,” Liahona, Nov. 2018, 111)25

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Tenga muda kwa ajili ya wanafunzi kushiriki. “Wakati wanafunzi wanapoelezea kile wanachojifunza, hawahisi tu Roho na kuimarisha shuhuda zao pekee, bali pia wanawahimiza washiriki wengine wa darasa kugundua ukweli wao wenyewe. … Tenga muda kwa ajili ya wanafunzi kushiriki katika kila somo—katika masuala mengine, unaweza kugundua kwamba majadiliano haya ndiyo somo” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 30).

Chapisha