Agano Jipya 2023
Agosti 28–Septemba 3. 1 Wakorintho 8–13: “Ninyi ni Mwili wa Kristo”


“Agosti 28–Septemba 3. 1 Wakorintho 8–13: ‘Ninyi Ni Mwili wa Kristo’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022)

“Agosti 28–Septemba 3. 1 Wakorintho 8–13,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
mkutano wa sakramenti

Agosti 28–Septemba 3

1 Wakorintho 8–13

“Ninyi ni Mwili wa Kristo”

Mzee Richard G. Scott alifundisha kwamba tunaweza “kuacha mwongozo binafsi wa thamani sana, wa Roho kwa kutosikika” kama tutashindwa kuandika na kuitikia “mwongozo wa kwanza unaokuja [kwetu]” (“Kupata Mwongozo wa Kiroho,” Liahona, Nov. 2009, 8).

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Katika 1 Wakorintho 8–13, Paulo alifundisha ukweli wa injili akitumia sitiari kama vile mkimbiaji katika mashindano ya mbio, mwili wa binadamu, na “shaba iliayo” (ona 1 Wakorintho 9:24–25; 12:13–26; 13:1). Ungeweza kuwaomba washiriki wa darasa kushiriki walichojifunza kutokana na milinganisho hii. Je, ni kwa jinsi gani milinganisho inatusaidia sisi kuelewa kweli za injili?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

1 Wakorintho 10:1–13

Mungu hutoa njia ya kuepuka majaribu.

  • Unawezaje kuwasaidia washiriki wa darasa kugundua kweli zenye nguvu katika 1 Wakorintho 10:13? Wazo moja ni kuugawa mstari katika virai vifupi, toa kila kimoja kwa mshiriki tofauti wa darasa, na waombe washiriki wa darasa kusema tena virai kwa maneno yao wenyewe. Kwa mfano, ni njia ipi nyingine ya kusema “Mungu ni mwaminifu” au “kujaribiwa zaidi ya vile mnavyoweza kustahimili”? Unaweza kisha kusoma upya mstari huo, ukitumia baadhi ya maelezo ya washiriki wa darasa. Washiriki wa darasa wanaweza kushiriki uzoefu ambapo waligundua ahadi katika kifungu hiki kuwa za kweli. Ni umaizi gani wa ziada tunaoweza kuupata kutoka kwenye mistari hii kutoka katika Alma 13:27–28?

  • Badala ya kukaa katika majaribu mahususi ya mtu fulani, ungeweza kuzingatia mjadala wako wa 1 Wakorintho 10:13 juu ya majaribu ambayo, kwa maneno ya Paulo “ni kawaida ya mwanadamu.” Washiriki wa darasa wangeweza kuanza kwa kutambua majaribu ambayo Paulo alionya juu yake katika mstari wa 1–12. Wanaweza pia kupendekeza mifano ya majaribu ya siku hizi ambayo ni ya kawaida, kama majaribu ya kutokuwa mwaminifu, kusengenya au kuhukumu wengine. Ni kwa namna gani mtu, kwa msaada wa Mungu, anaweza “kuyaepuka” majaribu haya?

1 Wakorintho 10:16–17; 11:23–30

Sakramenti hutuunganisha sisi kama waumini wa Kanisa la Kristo.

  • Mistari hii ingeweza kuchochea mjadala kuhusu namna gani sakramenti inaweza kuunganisha kata yenu katika juhudi zenu za kuwa kama Mwokozi. Ungeweza kuanza kwa kusoma 1 Wakorintho 10:16–17 na kuchunguza neno ushirika lingeweza kumaanisha nini katika muktadha huu (mwingine angeweza kuangalia maana katika kamusi). Ni kwa namna gani kula sakramenti pamoja kunatusaidia kujiona kuwa na umoja zaidi? Je, ni kwa namna gani ushauri wa Paulo “lakini mtu ajihoji mwenyewe” unahusiana na lengo hili? (1 Wakorintho 11:28).

1 Wakorintho 12

Karama za kiroho hutolewa ili kuwanufaisha watoto wote wa Baba wa Mbinguni.

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuona mifano ya jinsi gani kukuza vipawa vyao vya kiroho husaidia kuliinua Kanisa, fikiria kuwaalika kutafakari kuhusu vipawa vya kiroho watu katika maandiko walivyokuwa navyo. Kwa mawazo juu ya hilo, ungeweza kuwapa majukumu ya kutafuta moja kati ya marejeleo ya maandiko katika “Nyenzo za Ziada” na kutaja vipawa vya kiroho wanavyodhani mtu huyo alikuwa navyo. Wanaweza pia kuzungumzia karama za kiroho wanazoziona katika kila mmoja wao. Je, ni kwa jinsi gani vipawa vya kiroho vya watu hawa ni baraka kwetu sote? Je, tunawezaje kutumia karama zetu za kiroho kuwabariki wengine na kujenga mwili wa Kristo, au Kanisa? (ona 1 Wakorintho 12:12–31; ona pia 1 Wakorintho 14:12).

  • Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa jinsi ya kukuza karama za kiroho, waalike kusoma 1Wakorintho 12:27–31; Moroni 7:48; 10:23,30; Mafundisho na Maagano 46:8. Maandiko haya yanatufundisha nini sisi juu ya kupata karama za kiroho? Ni kwa jinsi gani kukuza karama zetu za kiroho hutufanya kuwa zaidi kama Kristo? Alika washiriki wa darasa kuchagua karama ambayo wangetaka kupata na kutafuta msaada wa Bwana katika kuipata.

1 Wakorintho 13

Hisani ni karama ya kiroho iliyo kuu zaidi.

  • Ungeweza kuwaomba washiriki wa darasa kutafakari kimya kimya 1 Wakorintho 13 na kumfikiria mtu wanayemjua ambaye ni mfano mzuri wa jambo moja au zaidi juu ya hisani aliyoisema Paulo. Baadhi ya washiriki wa darasa wangeweza kumwelezea mtu waliyemfikiria na tukio ambapo mtu huyu alionyesha mfano mzuri wa hisani. Ungeweza pia kuorodhesha sehemu ya maelezo ya Paulo kwenye ubao na kuwaalika washiriki wa darasa kutoa mawazo yao kuhusu kinachomaanishwa kwa mtu mwenye hisani “huvumilia” au “haesabu mabaya” (1 Wakorintho 13:4–5). Je, ni kwa namna gani Mwokozi alionyesha mfano wa tabia hizi za hisani? Ni kweli zipi za ziada Moroni 7: 46–48 inatufundisha kuhusu hisani?

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Mifano ya kimaandiko ya karama za kiroho.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Ishi kanuni unazofundisha. Kuishi kanuni unazofundisha kutakusaidia wewe kuzitolea ushuhuda wenye nguvu zaidi. Paulo alifundisha, “Na hivyo Bwana ameamuru kwamba wale waihubirio injili waishi kwa hiyo injili” (1 Wakorintho 9:14).

Chapisha