Agano Jipya 2023
Septemba 11–17. 2 Wakorintho 1–7: “Na Mpatanishwe na Mungu”


“Septemba 11–17. 2 Wakorintho 1–7: ‘Na Mpatanishwe na Mungu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022)

“Septemba 11–17. 2 Wakorintho 1–7 Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
Yesu Kristo

Septemba 11–17

2 Wakorintho 1–7

“Na Mpatanishwe na Mungu”

Unaposoma 2 Wakorintho 1–7 wiki hii, fikiria kuhusu washiriki maalum wa darasa lako—wale ambao wanakuja darasani na wale ambao hawaji. Ni kwa namna gani kanuni za sura hizi zitawabariki?

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Washiriki wa darasa wanaweza kunufaika kutokana na kusikia mawazo kutoka kwa wengine kuhusu jinsi ya kufanya ili kujifunza kwao maandiko kuwe na tija zaidi. Toa dakika chache kwa ajili ya hili mara kwa mara.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

2 Wakorintho 1:3–7; 4:6–10, 17–18; 7:4–7

Majaribu yetu yanaweza kuwa baraka.

  • Matukio ambayo Paulo ameyaeleza na ushauri aliotoa katika 2 Wakorintho unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kufikiria kuhusu baraka ambazo zinaweza kuja kutokana na majaribu yao. Kwa kuanza mjadala, unaweza kumuomba mshiriki wa darasa kuja akiwa amejiandaa kuzungumza kuhusu ni kwa namna gani jaribu lilibariki maisha yake au nini alijifunza kutoka kwa mtu aliyestahimili jaribu. Kisha unaweza kuwapa washiriki wa darasa dakika chache kurejelea 2 Wakorintho 1:3–7; 4:6–10, 17–18; na 7:4–7, wakitafuta Paulo alifundisha nini kuhusu madhumuni na baraka za majaribu. Waombe washiriki wa darasa kuelezea kile wanachokipata. Ungeweza kupendekeza kwamba wasome kwa sauti mistari ambayo kwayo wanapata fundisho maalum na kisha waelezee tukio au ushuhuda unaohusiana na fundisho hilo.

  • Kwa kuongezea katika mjadala wenu, fikiria kuimba kwa pamoja wimbo unaopendwa wa washiriki wa darasa ambao unashuhudia kuhusu faraja na baraka Baba yetu wa Mbinguni na Mwokozi wanatupatia katika nyakati za majaribu—kama vile “Msingi Imara” (Wimbo wa Kanisa, na. 85). Baada ya kuimba kwa pamoja, unaweza kuwakaribisha washiriki wa darasa kutafuta kirai katika 2 Wakorintho 1 na 4 ambacho wanahisi kinaendana na ujumbe wa wimbo huo.

2 Wakorintho 2:5–11

Toba ni baraka ambayo sote tunaitoa na kupokea.

  • Wote tumewahi kuwa na uzoefu ambapo mtu fulani “alisababisha huzuni” kwetu au katika familia yetu (mstari wa 5). Labda washiriki wa darasa wangeweza kutafuta kutoka katika 2 Wakorintho 2:5–11, wakiangalia ushauri kutoka kwa Paulo kuhusu namna ya kumchukulia mtu ambaye ametukwaza. Fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kurejea Mathayo 5:43–48 na Luka 8: 1–32 ili kujifunza zaidi kuhusu jinsi tunavyopaswa kuwatendea wale waliotukwaza. Je, ni kwa nama gani tunajidhuru sisi wenyewe pamoja na wengine pale tunapokuwa hatuko tayari kusamehe?

2 Wakorintho 5:14–21

Kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo, tunaweza kupatanishwa na Mungu.

  • Watu wengi huja Kanisani wakiwa na hamu ya kuhisi wako karibu na Mungu, na mjadala wa 2 Wakorintho 5:14–21 unaweza kuwasaidia. Ili kuanza, washiriki wa darasa wangeweza kuchunguza maana ya neno kupatanisha, labda anza kwa kuangalia neno hilo katika kamusi. Je, hii inaleta umaizi gani kuhusu kupatanishwa na Mungu? Je, ni umaizi gani wa ziada tunapata kutokana na ingizo la neno “Upatanisho, katika Kamusi ya Biblia? Ni kwa jinsi gani umaizi huu hutusaidia kuelewa 2 Wakorintho 5:14–21? Yawezekana ukataka kuwaalika washiriki wa darasa kuelezea hisia zao kuhusu Mwokozi , ambaye Upatanisho wake unafanya iwezekane kwetu sisi kuungana na Mungu tena.

2 Wakorintho 7:8–11

Huzuni ya kimungu hutuongoza kwenye toba.

  • 2 Wakorintho 7:8–11 hutoa maelezo ya msaada kuhusu huzuni ya kimungu na nafasi yake katika toba. Je, tunajifunza nini kuhusu huzuni ya kimungu kutoka 2 Wakorintho 7: 8–11 na maneno ya Rais Dieter F. Uchtdorf katika “Nyenzo za Ziada”? Kwa nini huzuni ya kimungu ni muhimu katika toba?

  • Unaweza kuhisi msukumo wa kuhimiza majadiliano kwa kina kuhusu toba. Kama ndivyo, unaweza kujaribu kitu kama hiki: Andika ubaoni Toba ni . Waombe washiriki wa darasa kutafuta jinsi ya kumalizia kirai hiki wakitumia mambo wanayojifunza kutoka 2 Wakorintho 7:8–11, pia kutoka kwenye maandiko na nyenzo zingine zinazopatikana katika Mada za Injili “Toba” (topics.ChurchofJesusChrist.org). Ni kwa namna gani tunaweza kutumia mafundisho haya ili kumsaidia mtu fulani kuelewa namna ya kutubu kwa dhati?

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Huzuni ya kimungu hushawishi kuwa na mabadiliko na matumaini.

Rais Dieter F. Uchtdorf alifafanua:

Huzuni ya kimungu hushawishi tuwe na mabadiliko na matumaini kwa njia ya Upatanisho wa Yesu Kristo. Huzuni ya kiulimwengu hutuvuta chini, huzima matumaini, na hutushawishi kushindwa na kuingia katika majaribu zaidi.

Huzuni ya kimungu hutuongoza kwenye uongofu na badiliko la moyo. Hutufanya sisi kuchukia dhambi na kupenda wema. Hutuhimiza kusimama na kutembea katika nuru ya upendo wa Kristo. Toba ya kweli ni kuhusu badiliko, si mateso na maumivu” (“Unaweza Kufanya Hivyo Sasa!,” Liahona, Nov. 2013, 56).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wajumuishe wale wote wanaosumbuka. Wakati mwingine washiriki wa darasa wanaosumbuka wanahitaji kujumuishwa ili wahisi wanapendwa. Fikiria kuwapangia jukumu ili washiriki katika somo lijalo. Usikate tamaa kama watashindwa kuitikia jitihada zako kwa mara ya kwanza. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 8–9.)

Chapisha