Agano Jipya 2023
Septemba 18–24. 2 Wakorintho 8–13: “Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu”


“Septemba 18–24. 2 Wakorintho 8–13: ‘Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022)

“Septemba 18–24 . 2 Wakorintho 8–13 Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
Yesu akiongea na mtoto mdogo

Septemba 18–24

2 Wakorintho 8–13

“Mungu Humpenda Yeye Atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu”

Wakati unasoma 2 Wakorintho 8–13, fikiria kuhusu watu unaowafundisha na panga shughuli ambazo zingewasaidia kugundua kanuni katika sura hizi. Kisha rejea muhtasari huu kwa ziada ya mawazo.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Hapa kuna njia moja ya kuwaalika washiriki wa darasa kushiriki walichojifunza kutoka 2 Wakorintho 8–13: waombe wachache wao kuandika juu ya ubao kifungu cha maneno wakipendacho kutokana na kusoma kwao na washiriki kwa nini vifungu hivi ni vya maana kwao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

2 Wakorintho 8:1–15; 9:6–15

Watakatifu kwa ukarimu hushiriki na wengine vile walivyonavyo ili kuwabariki masikini na wenye shida.

  • Mungu amewaamuru Watakatifu Wake kusaidia kuwatunza wale wenye shida, na vipengele katika 2 Wakorintho 8–9 vinaweza kuwashawishi washiriki wa darasa lako katika juhudi zao. Ili kuwasaidia kupata vifungu hivi ungeweza kuandika kwenye ubao maswali kama Kwa nini tunatoa? na Tunapaswa kutoaje? Nusu ya darasa wangeweza kutafuta majibu katika 2 Wakorintho 8:1–15, na nusu nyingine wangeweza kutafuta katika 2 Wakorintho 9:6–15. (Ungeweza kuelezea kwamba katika sura ya 8, mstari wa 1–5, Paulo aliongea kuhusu Watakatifu wa Makedonia kama mfano wa watoaji kwa ukarimu.) Je, ni kwa namna gani kanuni zilizofundishwa na Paulo hutusaidia kuwatunza vyema zaidi walio masikini na wenye shida?

2 Wakorintho 11:1–4

Tunapaswa kuzingatia kwenye “unyofu ambao u katika Kristo.”

  • Wakati mwingine waumini wa Kanisa wanahisi kuzidiwa na mahitaji ya kimaisha—ikijumuisha kile ambacho wangeweza kukiona kama mahitaji ya kuwa Mtakatifu wa Siku za Mwisho. Ushauri wa Paulo kuhusu “unyofu ulio katika Kristo” (2 Corinthians 11:3) unaweza kusaidia. Labda mngeweza kusoma pamoja 2 Wakorintho 11:3 na kujadili kirai “unyofu na usafi kwa Kristo” kinaweza kumaanisha nini. Ungeweza pia kuwauliza washiriki wa darasa kupiga taswira kuwa wamealikwa kuandika maelezo ya injili ya Yesu Kristo katika gazeti, kwa kikomo cha maneno100. Wape muda kuandika maelezo yao na waache washiriki walichokiandika. Kama wanahitaji msaada, wanaweza kurejelea kwa Yohana 3:16–17; 3Nefi 27:13–21; maelezo ya Rais Dieter F. Uchtdorf’ katika “Nyenzo za Ziada.” Washiriki wa darasa wanaweza kushiriki mawazo kuhusu jinsi ya “kunyoosha njia [zetu] kuendea ufuasi.”

2 Wakorintho 12:5–10

Neema ya Kristo inatosha kutusaidia kupata nguvu katika udhaifu wetu.

  • Ungeweza kusema nini kwa rafiki yako ambaye amesali kwa ajili ya kupata nafuu kutokana na udhaifu wa kimwili lakini anahisi sala hii haijibiwi? Fikiria kuwaalika washiriki wa darasa kutafakari swali hili wanaposoma kimya kimya 2 Wakorintho 12:5–10. Kisha wangeweza kuelezea umaizi wao kutoka kwenye mistari hii ambao ungeweza kusaidia katika hali kama hii. Wangeweza pia kushiriki na wengine uzoefu ambapo, kwa njia ya neema ya Yesu Kristo, walipata nguvu katika udhaifu wao. Je, ni kwa namna gani jambo hilo linaathiri maisha yao? Kwa nini ni muhimu kutumaini katika ratiba ya Bwana?

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Tunaweza kunyoosha njia yetu ya kuishi injili.

Rais Dieter F. Uchtdorf alifundisha:

“Akina kaka na akina dada, kuishi injili hakuhitaji kuwe kugumu.

Ni dhahiri kabisa. Ingeweza kuelezeka hivi:

  • Kulisikia neno la Mungu kwa umakini kunatuongoza kumwamini Mungu na kutumaini ahadi Zake.

  • Kadiri tunavyomwamini Mungu, ndivyo mioyo yetu inavyojawa na upendo Kwake na kwa kila mmoja wetu.

  • Kwa sababu ya upendo wetu kwa Mungu, tunatamani kumfuata Yeye na kutenda mambo yanayoendana na neno Lake.

  • Kwa sababu tunampenda Mungu, tunataka kumtumikia Yeye, tunataka kubariki maisha ya wengine na kuwasaidia maskini na wenye shida.

  • Kadiri tunavyotembea katika njia hii ya ufuasi, ndivyo tunavyotamani kujifunza neno la Mungu.

“Na ndivyo iendavyo, kila hatua inatuongoza kwenye hatua nyingine na kutujaza ongezeko lisilo na mwisho la imani, matumaini na hisani.

“Ni rahisi sana, na inafanya kazi vizuri sana.

“Kaka zangu na dada zangu, kama uliwahi kufikiria kwamba injili haifanyi kazi vizuri kwako, ninakuomba rudi nyuma, yaangalie maisha yako kutoka juu, na rahisisha mwenendo wako wa ufuasi. Zingatia katika mafundisho ya msingi, kanuni na matumizi ya injili. Ninawaahidi kwamba Mungu atawaongoza na kuwabariki katika njia zenu za maisha ya kuridhisha, na injili itafanya kazi vizuri kwenu” (“Inafanya kazi vizuri sana,” Liahona, Nov. 2015, 22).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fanya kazi pamoja na washiriki wa familia. “Watu ambao wana ushawishi mkubwa kwa mtu binafsi—kwa wema au ubaya—kawaida ni wale walio wa nyumbani mwake. Kwa sababu nyumbani ni kituo cha kujifunza na kuishi injili, juhudi zako za kumuimarisha mshiriki wa darasa zitakuwa za ufanisi zaidi wakati unapofanya kazi pamoja na … wanafamilia” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,8).

Chapisha