Agano Jipya 2023
Novemba 20 –26. 1 na 2 Petro: “Furahini kwa Shangwe Isiyoelezeka na kwa Utimilifu wa Utukufu”


“Novemba 20– 26. 1 na 2 Petro: ‘Furahini kwa Shangwe Isiyoelezeka na kwa Utimilifu wa Utukufu’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2021)

“Novemba 20–26. 1 na 2 Petro 2–16,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
Yesu Kristo akifundisha injili katika ulimwengu wa roho

Kristo Akihubiri katika Ulimwengu wa Roho, na Robert T. Barrett

Novemba 20–26

1 na 2 Petro

“Furahini kwa Shangwe Isiyoelezeka na kwa Utimilifu wa Utukufu”

Kumbuka kwamba lengo lako ni kufundisha watu, na si tu kuwasilisha somo. Unaposoma Nyaraka za Petro, fikiria juu ya mshiriki mmoja mmoja wa darasa lako. Ni kanuni gani zitawasaidia kujenga imani yao?

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Andika vichwa vya habari 1 Petro na 2 Petro ubaoni. Wape washiriki wa darasa muda wa kurejelea sura hizi, na waalike kuandika chini ya vichwa hivi maneno au vifungu vya maneno kutoka kwenye sura ambavyo wameona kuwa ni vya muhimu. Kisha tumia orodha hiyo kuwaalika watu kushiriki utambuzi wao.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

1 Petro 1:3–9; 2:19–24; 3:14–17; 4:12–19

Ninaweza kupata shangwe katika nyakati za majaribu na mateso.

  • Njia mojawapo ya kurejelea ushauri wa Petro katika 1 Petro 1:3–9; 2:19–24; 3:14–17; na 4:12–19 ni kwa kuwaalika washiriki wa darasa kufikiria kuhusu mtu fulani ambaye wanamjua anayepitia majaribu. Wape muda katika darasa kuandika barua kwa mtu huyo, ikijumuisha kweli kutoka mistari hii ambazo zingeweza kumtia moyo mtu huyo (ona pia Mafundisho na Maagano 121:1–8; 123:17). Kisha washiriki wa darasa wangeweza kuongea kuhusu ukweli ambao waliuchagua.

1 Petro 1:13–20; 2:1–12

Tumeitwa kuwa “taifa la Mungu.”

  • Mafundisho ya Petro katika 1Petro 1:13–20 na 2:1–12 yanaweza kuwa kumbusho lenye kuwashawishi juu ya jinsi Bwana anavyotuona sisi—watu Wake—na kile anachokitarajia kwetu. Labda ungewaalika washiriki wa darasa kuipekua mistari hii wakiangalia maelezo ya inamaanisha nini kuwa “taifa la Mungu” (1 Petro 2:10) na kisha wajadili wanachokipata. Unaweza kueleza kwamba neno “mzao mteule” katika 1 Petro 2:9 maana yake “aliyenunuliwa” au “kuhifadhiwa” (ona tanbihi f). Hii hutufundisha nini kuhusu jinsi gani Mungu anahisi kuhusu sisi na jinsi gani Yeye anataka sisi tuishi?

1 Petro 3:18–20; 4:6

Injili inahubiriwa kwa wafu ili kwamba waweze kuhukumiwa kwa haki.

  • Waraka wa Kwanza wa Petro unayo moja kati ya marejeo machache katika Biblia ya matembezi ya Kristo kwenye ulimwengu wa roho baada ya kifo Chake—tukio ambalo ufunuo wa sasa hutusaidia kuelewa kwa ukamilifu zaidi. Ili kuweza kuwasaidia washiriki wa darasa kuelewa kwa kina juu ya ulimwengu wa roho, ungeweza kuwaalika kusoma maandiko yafuatayo na kuandika ubaoni kile wanachojifunza: Yohana 5:25; 1Petro 3:18–20; 4:6; Alma 40:7–14,21; Mafundisho na Maagano 138:11–32 (ona pia “Nyenzo za Ziada.”) Kwa nini ni muhimu kujua kuhusu Mwokozi kutembelea ulimwengu wa roho? Ni kwa jinsi gani ufahamu huu unaathiri jinsi tunavyohisi kuhusu Mungu na mpango Wake wa wokovu?

2 Petro 1:1–11

Kupitia nguvu ya Yesu Kristo, tunaweza kukuza asili yetu ya kiungu.

  • Ili kuwahimiza wale unaowafundisha katika jitihada zao za kuwa zaidi kama Yesu Kristo, ungeweza kuwaalika kuzitambua sifa kama za Kristo zilizoelezewa katika 2 Petro 1:1–11. Fikiria kuandika sifa hizi kwenye ubao na kuwaomba washiriki wa darasa kuzielezea. Kisha washiriki wa darasa wangeweza kujadili jinsi gani kukuza sifa moja hutupeleka katika kukuza sifa zingine. Toa muda kwao kutafakari sifa gani wangependa kuikuza kikamilifu zaidi.

Picha
kitambaa kilichofumwa kwa ustadi mkubwa

Kila sifa ya Kristo tunayoiendeleza hutusaidia kufuma kitambaa cha kiroho cha ufuasi.

Picha
ikoni ya nyenzo

Nyenzo za Ziada

Kazi ya kuwakomboa wafu hushuhudia kuhusu misheni ya Mwokozi.

Mzee D . Todd Christofferson alifundisha:

Je, ni nini hatima ya mabilioni yasiyohesabika ya walioishi na kufa bila uelewa juu ya Yesu? Pamoja na Urejesho wa injili ya Yesu Kristo umekuja uelewa wa jinsi gani waliokufa bila kubatizwa wanakombolewa na jinsi gani Mungu anaweza kuwa Mungu ‘mkamilifu, Mungu mwenye haki na Mungu mwenye rehema pia’ [Alma 42:15].

“Akiwa bado yu hai, Yesu alitoa unabii kwamba Yeye angewahubiria wafu pia [ona Yohana 5:25]. Petro anatuambia kwamba hii ilitokea katika kipindi kati ya kusulubiwa kwa Mwokozi na Ufufuko [ona 1 Petro 3:18–19]. Rais Joseph F. Smith alishuhudia katika ono kwamba Mwokozi alikwenda kwenye ulimwengu wa roho [ona Mafundisho na Maagano 138:30,33]. …

“Shauku yetu ya kukomboa wafu, na muda na rasilimali tunazoweka nyuma ya ahadi hii, ni, na zaidi ya yote, ni onyesho la ushahidi wetu kuhusu Yesu Kristo. Inajumuisha kauli yenye nguvu ambayo tunaweza kuitengeneza kuhusu sifa Yake ya kiungu na misheni Yake takatifu. Hushuhudia, kwanza, kuhusu Ufufuko wa Kristo; pili, juu ya ufikiaji wake usio na mwisho wa Upatanisho Wake; tatu, kwamba yeye ni chanzo pekee cha wokovu; nne, kwamba Yeye ameweka masharti ya wokovu; na, tano, kwamba Yeye atakuja tena” (“Ukombozi wa Wafu na Ushuhuda wa Yesu,” Ensign, Nov. 2000, 9–10).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Fundisha kipengele cha “kwa nini.” “Wakati mwingine wanafunzi—hasa vijana—hujiuliza ni kwa jinsi gani kanuni za injili zinavyohusiana nao au ni kwa nini wanapaswa kutii amri fulani. Hata hivyo, ikiwa wataelewa mpango wa milele wa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya furaha ya watoto Wake, sababu ya kanuni za injili na amri huwa wazi zaidi na motisha ya kutii huongezeka” (Kufundisha katika Njia ya Mwokozi20).

Chapisha