Agano Jipya 2023
Mpangilio wa Kufundisha


“Mpangilio wa Kufundisha,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano Jipya 2023 (2022)

“Mpangilio wa Kufundisha,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2023

Picha
vijana wakisoma maandiko

Mpangilio wa Kufundisha

Kila muhtasari katika nyenzo hii hufuata mpangilio wa kualika kushiriki na kufundisha mafundisho. Mara nyingi, unapofundisha, vipengele vya mpangilio huu vinaweza kuingiliana au kutokea kwa utaratibu tofauti. Kwa mfano, fikiria kuwa kushiriki na wengine ni fursa ya kufundisha mafundisho, na kufundisha mafundisho kunapaswa kuhusishe mialiko ya kushiriki. Ruhusu marekebisho katika mpangilio huu yatokee kiuhalisia, ukifuata ushawishi wa Roho ili kukidhi mahitaji ya watoto unaowafundisha.

Alika Kushiriki

Kama sehemu ya kila darasa, waalike washiriki wa darasa kushiriki na wengine umaizi na uzoefu waliokuwa nao wiki iliyopita walipojifunza maandiko wao binafsi na kama familia na kutendea kazi kile walichojifunza. Wasaidie washiriki wa darasa kuona kwamba kujifunza kwao binafsi nje ya darasa ni muhimu. Uongofu wao binafsi kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo hautakuja kwa njia ya kujifunza Jumapili pekee bali pia kupitia matukio yao ya kila siku. Wakati washiriki wa darasa wanaposikia uzoefu wa kila mmoja na ushuhuda juu ya Yesu Kristo na injili Yake, wanakuwa na uwezekano wa kutafuta uzoefu sawa na huo wa kwao wenyewe.

Si kila mmoja atakuwa ameshasoma sura za kila somo, na hata baadhi ya wale waliosoma wanaweza wasijisikie vizuri kushiriki na wengine. Hakikisha kila mshiriki wa darasa wanajiona kuwa wao ni sehemu ya thamani ya darasa, bila kujali wana kitu cha kushiriki na wengine au la.

Fundisha Mafundisho

Wewe na washiriki wa darasa lako mnapaswa kufokasi katika Yesu Kristo na mafundisho Yake—ukweli wa milele wa injili—unaopatikana katika vipengele vya maandiko vilivyotolewa. Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia inaweza kukusaidia kuelewa vizuri zaidi mafundisho ambayo utawafundisha watoto. Unapojadili mafundisho kutoka kwenye maandiko, ni mistari ipi, nukuu zipi, uzoefu upi, maswali yapi, na nyenzo zipi za ziada ungeweza kushiriki na wengine? Ungewezaje kutumia nyenzo hizi kuwasaidia washiriki wa darasa kugundua na kuelewa kanuni za injili? Je, unawezaje kuwasaidia kujenga imani yao kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo?

Chapisha