Agano la Kale 2022
Desemba 27–Januari 2. Musa 1; Ibrahimu 3: “Hii Ndiyo Kazi Yangu na Utukufu Wangu”


“Desemba 27–Januari 2. Musa 1; Ibrahim 3: ‘Hii Ndiyo Kazi Yangu na Utukufu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: Agano la Kale 2022 (2021)

“Desemba 27–Januari 2. Musa 1; Ibrahimu 3,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Shule ya Jumapili: 2022

Picha
picha za nyota katika anga

Desemba 27–Januari 2

Musa 1; Ibrahimu 3

“Hii Ndiyo Kazi Yangu na Utukufu Wangu”

Unaposoma Musa 1 na Ibrahimu 3, weka akili zako na moyo wazi kwa misukumo kutoka kwa Roho. Atakutia msukumo kwa mawazo na fikra ambazo zitakusaidia kujiandaa kufundisha.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Washiriki wa darasa lako wanaweza kuwa wamepata uzoefu wa kupendeza waliposoma Musa 1 na Ibrahimu 3 nyumbani. Utawapaje washiriki wa darasa fursa za kushiriki uzoefu huo? Inaweza kuwa rahisi kama kuuliza maswali sawa na haya: Nini kilikuvutia ulipokuwa unasoma maandiko wiki hii? Nini kilikushangaza? Nini kilikufanya usimame na kufikiri? Nini kilikusaidia uhisi karibu zaidi na Baba yako wa Mbinguni na Yesu Kristo?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho

Musa 1:1–10, 37–39; Ibrahimu 3:22–26

Kama watoto wa Mungu, tuna takdiri takatifu.

  • Kweli zilizofunuliwa katika maono ya Musa na Ibrahimu zinaweza kuwa na ushawishi wenye nguvu kubwa kwenye chaguzi zetu na kwenye uwezo wetu wa kushinda changamoto za maisha. Jinsi gani unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa lako kugundua kweli hizi katika Musa 1 na Ibrahimu 3? Wazo moja ni kuligawa darasa katika makundi na pangia kila kundi moja ya vifungu vifuatavyo: Musa 1:1–10; Musa 1:37–39; Ibrahimu 3:22–26. Kila kundi lingeweza kutafuta majibu kwa maswali kama vile “mimi ni nani?” “Kwa nini nipo hapa?” na “Mungu anataka mimi niwe nani?” Baada ya muda wa kutosha, makundi yanaweza kushiriki majibu yao. Jinsi gani majibu haya yanaweza kushawishi matendo yetu ya kila siku?

    Picha
    Yesu Kristo miongoni mwa nyota

    Kristo na uumbaji, na Robert T. Barrett

Musa 1:12–23

Tunaweza kupinga ushawishi wa Shetani.

  • Makabiliano ya Musa na Shetani, yanayopatikana katika Musa 1:12–23, yanashikilia masomo ambayo yangeweza kusaidia washiriki wa darasa lako wanapokabiliwa na majaribu au udanganyifu kutoka kwa adui. Tunaweza kujifunza nini kutokana na majibu ya Musa? Video “I am a Son of God” (ChurchofJesusChrist.org) inaweza kusaidia washiriki wa darasa kujadili moja ya mbinu za Shetani—kutujaribu kuwa na wasiwasi na uzoefu wetu wa Kiroho (ona pia “Nyenzo za Ziada”). Inaweza kuwa na maana kama washiriki wa darasa walishiriki mawazo na msukumo kusaidiana kila mmoja kugundua na kupinga juhudi za Shetani.

  • Somo moja kutoka uzoefu wa Musa ni kwamba Shetani anatujaribu kwa kuiga ukweli na uwezo wa Mungu. Ili kuwasaidia washiriki wa darasa kupata taswira ya hili, ungeweza kuleta darasani baadhi ya vitu ambavyo ni tafsiri za uongo za vitu vingine, kama vile mmea wa bandia au mwanaserere. Tunawezaje kuelezea kwamba hivi ni bandia? Nini baadhi ya vitu vya kuiga Shetani anatumia leo kutujaribu? Jinsi gani tunaweza kuvitambua na kuvikataa? (Kujifunza jinsi Musa alivyofanya hili, ona Musa 1:13–18.) Jinsi gani Bwana anatusaidia katika juhudi zetu? (ona Luka 1:24–26).

Ibrahimu 3:22–28

Maisha haya ni fursa yetu kuonesha kwamba tutafanya kile Mungu anachoamuru.

  • Jinsi gani unaweza kuwasaidia washiriki wa darasa kuona maisha yao kama fursa ya kuthibitisha uaminifu wao kwa amri za Mungu? Unaweza kuanza kwa kuwaomba kueleza kuhusu uzoefu walipotakiwa kuonesha uhodari katika ustadi—kwa mfano, shuleni, kazini, au kwenye timu ya michezo. Wanaweza kuelezea kuhusu kile walichotakiwa kufanya kujithibitisha wenyewe. Jinsi gani uzoefu huu ni sawa na kile kilichoelezwa katika Ibrahimu 3:24–26? Jinsi gani ni tofauti? Jinsi gani tunamjumuisha Baba wa Mbinguni na Mwokozi katika juhudi zetu za “kujithibitisha” wenyewe? (Ibrahimu 3:25). Jinsi gani kujua kwamba tupo hapa kujithibitisha wenyewe kuwa watiifu kunaathiri jinsi tunavyopokea changamoto za maisha?

  • Nini kingine tunajifunza kutoka Ibrahimu 3:22–28 kuhusu maisha kabla ya kuja duniani, au “hali zetu za mwanzo”? (mstari wa 26). Kwa nini kweli hizi ni muhimu kwetu?

Picha
ikoni ya nyenzo za ziada

Nyenzo za Ziada

Usiwe na wasiwasi na kile kilichofunuliwa kwako.

Mzee Jeffrey R. Holland alifundisha hili kuhusu uzoefu wa Musa katika Musa 1: “ujumbe wa Musa kwako leo ni: Usiache kujilinda. Usisadiki kwamba ufunuo mkubwa, baadhi ya maajabu, wakati wa kuangaza, ufunguzi wa njia ya kuvutia, ni mwisho wake. … Kama awali kumekuwa na mwangaza, kuwa mwangalifu dhidi ya majaribu ya kurudi kutoka kitu kizuri. Kama ilikuwa sahihi ulipoomba na kuamini na kuishi kwa hilo, ni sahihi hata sasa. Usikate tamaa wakati shinikizo linapokuwa kubwa. Kwa hakika usikate tamaa kwa kiumbe yule ambaye ameazimia uharibifu wa furaha yako. Kabiliana na mashaka yako. Shinda woga wako. ‘Kwa hivyo, usitupe ujasiri wako.’ [Waebrania 10:35]. Baki katika njia na uone uzuri wa maisha ukifunuliwa kwa ajili yako” (“Kwa hivyo Usitupe Ujasiri Wako,”,” Ensign, Machi. 2000, 7, 9).

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie wanaojifunza kugundua kweli katika maandiko. Kabla ya kuwaomba washiriki wa darasa kusoma vifungu vya maandiko, unaweza kuwapa kitu fulani mahususi kutafuta na kufikiria. Kwa mfano, wangeweza kutafuta kitu fulani wanachojifunza kuhusu Mwokozi au kitu fulani ambacho wangetaka kushiriki na mwanafamilia. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 21.)

Chapisha